Daktari Augustine. Wacha huu upuuzi wa CCM tusiupuuze kdg. Kuna upuuzi wa kupuuzwa, mwingine unapaswa kujadiliwa ili uzidi kuonekana na kuwekwa wazi ni upuuzi wa kiwango gani na walioutoa wazidi kupuuzwa na kuonekana daraja la kutojua kwao ni la ngapi!
Aiseee this is very serious.
Imefikia hatua chama tawala hakiwezi tena kuzungumzia shughuli za maendeleo, hakiwezi kusema sera zake (zimeshindwa) zimefikia wapi, hakiwezi kusema kwa wananchi kuwa in next 50 or so years sera hizo zitalifikisha taifa mahali gani, hakiwezi kusema hadi sasa kimefanyika 1, 2, 3 (tangible)...this is getting more serious.
Kwamba CCM imefikia mahali haiwezi kabisa hata kuzungumzia topical issue (zilizoko) kwenye maisha ya kila siku ya wananchi, zinazohusu maendeleo yao, mathalani hata kuzungumzia namna rasilimali za nchi zinavyoporwa na uhusiano huo kwa ugumu wa maisha unaowakabili wananchi, mismanagement ya uchumi na athari zake kwa ugumu wa maisha unaozidi kudhihirika kupitia 'mkate' wa kila siku na masuala mengine kama usafiri!
Kila wakilala, wakiamuka, wakikutana, kila wakisema, kila wakipayuka, ni CHADEMA, CHADEMA, CHADEMA, CHADEMA...dude! Who are these CHADEMA ambao wanaweza kuifikisha serikali ya CCM kwenye defensive mechanisim ya kichovu kama hii ambayo inaashiria serikali kusarenda na chama tawala kujiandaa kuondoka, ofcoz baad ya kumwaga damu za watu kwa kujaribu kuzuia 'mvua kunyesha!'.
Imefikia mahali CCM wakishinda hata kitongoji au kijiji, wanalazimika kukimbiza mwenge kutangaza kuwa wamewashinda CHADEMA mahali fulani! Haikuwahi kutokea. Inatokea sasa na hali hii inaonekana kuchemka kadri zinavyosogea siku.
Vitu kadhaa tungependa Nape's na Kinana's crew huko waliko kwenye ziara ambao wanazidi kushuhudia namna ambavyo wananchi wamewaasi sirini na hadharani, wenzao wengine walioko sehemu zingine na ndani ya serikali, wajue;
1. CHADEMA haitafanya siasa kwa hisani ya CCM. Hii ni kwa sababu kauli za Nape kama zilivyonukuliwa na jamaa zao hawa kuanzia jana na leo, mbali ya kutaka kupotosha, zinalenga upotoshaji huo ufanyiwe kazi na vyombo vya dola (kwa maelekezo) kama walivyozoea. Itaendelea kufanya kazi za kisiasa kama wajibu na haki ya kikatiba. Period.
2. Hizi kauli za kila siku za Nape ambazo hazina ushahidi hata wa kimazingira, hasa akiwataja viongozi wakuu ili eti apate attention yao, hatafanikiwa. Let him mark my words, viongozi makini wa taasisi makini kama CHADEMA hawataweza kupoteza muda na mtu wa sampuli hii.
Kwa kushirikiana na Watz wengine wenye moyo na akili njema za kujenga nchi yao, wanayo mambo mengi ya msingi kwa ajili ya kufikiria next 50-100 years ya taifa letu. In its store, CHADEMA has a lot to fit Nape. Tena ajiandae, asishangae siku moja atajibiwa na mabalozi wa nyumba kumi kumi.
Maana tunajua amekuwa akifanya makusudi kwenye kila kauli yake anayotoa lazima ataje Dkt. Slaa au Mwenyekiti Mbowe...hatafanikiwa. Bila shaka na watu wao wanaowatumia kuandika stories kama hizi watatusaidia kujua hili vizuri. Eti walimtafuta Mbowe na Dkt. Slaa kwa ufafanuzi...wa kauli za Nape?!?!? What a waste of time for Mwenyekiti Mbowe or Dkt. Slaa responding to Nape!
Tuje kwenye huu uzushi wake ambao kama alivyosema Mohamed, ulishakuwa pre-empted. Mwanzoni walipanga anukuliwe mtu mmoja aliyehamiwa kwao miaka zaidi ya miwili iliyopita. Akutane na watu wao, wawalishe maneno. Kisha stori iwe kwamba huyo mtu aliwahi kuwa mjumbe eti wa kamati ya ulinzi ya chama (sijui imeanzishwa lini) hivyo wakati akiwa bado CHADEMA waliwahi kukaa kikao na kupanga mipango...ilivyokuwa preempted, wakaahirisha.
Wakaamua kutoka leo kivingine kidogo. Kutokea jukwaani.
Itoshe tu kuonesha vitu kadhaa, ambavyo viko kwenye kauli hizi hii ambavyo vitamfanya aliyezitoa azidi kuonekana kwamba ni mpuuzi na alichosema ni maneno yao ya siku yote ya kutunga eti ikiwa ndiyo mikakati ya timu mpya ya sekretarieti kupambana na wimbi kubwa la mabadiliko.
Wakati wa shughuli za mikutano ya M4C Morogoro, Mwenyekiti Mbowe kwa sehemu kubwa alikuwa bungeni, kabla ya kusafiri kikazi kwenda nje ya nchi. Siku ya mapokezi yaliyovurugwa na polisi kwa maelekezo ma faida ya CCM, kisha polisi wakamuua ndugu Ally Singano Zona, Mwenyekiti Mbowe hakuwepo kabisa Dar es Salaam. Kusema kuwa alikuwa Dar es Salaam ni uongo. Mtu kijana hawezi hata kutafiti kidogo kabla hajasema. Akiwa muongo kwenye umri wa namna hii, sijui akizeeka itakuwaje...
Katibu Mkuu, Dkt. Slaa alikuwepo kwenye M4C ya Morogoro. Wakati polisi wakimuua yule kijana kwa kitu kizito chenye ncha kali, Dkt. Slaa alikuwepo Morogoro. Na baadae siku hiyo hiyo baada ya polisi kuvuruga mapokezi, alihutubia mkutano mkubwa sana wa kihistoria mjini Morogoro, ambao ulikuwa na simanzi ya kumpoteza binadamu mwenzao kwa hujuma za CCM inayoogopa mikutano na operesheni za CHADEMA kwa kiwango kisichofananishwa!
Hakukuwa na maandamano yoyote siku hiyo. Kulikuwa na mapokezi ya wanachama wa CHADEMA wa Morogoro pamoja na wananchi wengine kuwalaki viongozi wengine waliokuwa wanatokea Dar es Salaam kwenda Morogoro. Polisi wakaingilia. Wakapiga mabomu, wakafyatua risasi za moto. Wakajeruhi. Mtu mmoja akafa. Wakajichunguza wao, wakajiundia mashtaka, wakajisikiliza na kujifutia tuhuma za mauaji ya huyo mtu mmoja. Lakini hadi leo wananchi wanajua walioua ni polisi.
Kuna mtu yeyote anaweza kuwaambia Watz kuwa CHADEMA walivunja sheria ipi au kifungu kipi cha katiba kuwapokea viongozi wao kisha waende kwenye mkutano wa hadhara uliokuwa umeshatolewa taarifa polisi kama inavyotakiwa?
Sasa kwa nini mtu aseme uongo kiasi hiki unaomfanya aonekane ni mtu wa kupuuzwa hata na mtu aliye tabulalasa!
Hivi ni lini CCM waliwahi kukiri hadharani (tunajua wanafanya hivyo sirini) kuwa umaarufu wa CHADEMA umekua? Kama hawajawahi kukiri hivyo au kusema hadharani, sasa wanapata wapi uhalali au ujasiri wa kusema umaarufu wa CHADEMA umepungua?
Hofu yao inayowafanya watunge maneno kama haya inadhihirisha namna wanavyotishika na umaarufu huo wa CHADEMA ambao wanaukiri kwa kusema kinyume chake hadharani na kuusema kwa dhati wakiwa kwenye vikao vya ndani.
Mipango ya operesheni kwenye miji gani sijui (labda maana ya mji ni nyingine) maana labda kijiji cha Ruaha kimepewa hadhi ya kuwa mji, Ilula nayo siku hizi imekuwa mji, Makambako nayo siku hizi ni mji? Songea.
Hakujapangwa kufanyika shughuli rasmi za chama kuhusisha ngazi ya taifa. Lakini mamlaka nyingine kama kanda za chama (mikoa, wilaya, majimbo, kata, vijiji, matawi na misingi) zinayo mamlaka ya kufanya siasa na kusimamia utendaji wa chama katika maeneo husika kwa kila siku. Wanaweza kufanya shughuli za kisiasa wakati wowote, mahali popote, kama wajibu wao na haki yao ya kikatiba.
Inajulikana. Wananchi wa Ruaha wamekataa dhuluma wanayotaka kufanyiwa na utawala wa CCM. Kusimikiwa kiongozi asiyetokana na matakwa yao. Wanao ujasiri wa kusema hapana. Ndiyo maana walimuuliza maswali Katibu Mkuu wa CCM juu ya tuhuma za "weka mbali na tembo", wakiwa pamoja na Nape, wakafunga mkutano na kukimbia, wakisema wananchi wale wametumwa na CHADEMA.
Wananchi wa maeneo mengine vivyo hivyo wanaweza kuwa na harakati zao za kudai haki, maana dhuluma za CCM sasa ni kila mahali. Nape asiwatishe.
Kama CCM wangelikuwa wanawajali wnananchi, au basi wangejali maisha ya Watanzania, wakiwemo hao wa Songea ambao leo wanajifanya eti kuwapatia tahadhari, basi angehakikisha Michael Kamuhanda aliyesababisha watu kadhaa wa mji huo, wakiwemo vijana, wapigwe risasi na kufa papo hapo, anawajibishwa ikiwemo kufukuzwa kazi na kushtakiwa.
Mtu huyo huyo amekwenda Iringa na kusimamia mauaji ya Daudi Mwangosi. Kwa sababu ya kutekeleza kwa ufanisi kazi ya mauaji anayotumwa kutokana na mipango ya CCM, juzi Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Kikwete kampandisha cheo!
Waache uongo. Watu wanawajua na kuwaona. Hiyo huruma wanaotaka kujipachika hawana. huo ubinadamu wananoyaka kuigiza, ulishawatoka. Hawana. Wangeanzia kwa kuhakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali zao. Wangeweza basi kuwahurumia tembo wanaokatiliwa maisha kwa ukatili wa hali ya juu na na twiga wanaokunjwa shingo na kuwekwa kwenye ndege.
Wangeweza hata kuepusha vifo vya watu vinavyosababishwa na serikali hii hii na chama hiki hiki, kila mahali sasa! Kuanzia kwenye elimu, kilimo, mifugo, viwanja, afya, maji machafu, barabara mbovu, uvunjwaji wa sheria, ukiukwaji wa katiba, kulindana!
Kama wana ujasiri wa kuweza kusema kuna hata tukio moja la mauaji limesababishwa na CHADEMA, kwa nini Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza walau hata kujibu barua ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbowe, juu ya azimio la Kamati Kuu, kumtaka Rais aunde Tume Huru ya Kimahakama/Kijaji kuchunguza matukio yote, walau walitajiwa matano, likiwemo moja lililomhusisha kiongozi wa CCM kule Ndago, Iramba, Singida?
.