Rafiki yangu
BAK, hakuna sehemu nimesema sitaki aongee na ndugu zake..... aongee nao tu any time, sina shida na hilo.
Sijui naeleweka hapa au la; huyu mtu nampa 1000 kwa wiki kwa ajili ya kunipigia endapo dharura itatokea nyumbani, ni kiasi cha kutoa taarifa tu. Siku hizi bongo simu ni very cheap kupiga, yaani mimi hata sms naonaga uvivu kutuma. napiga kwenye mtandao wowote, muda wowote, ni cheap sana. huyu mdada anaweza kaa mwezi mzima asinipigie simu ya dharura, inawezekana hata miezi mi3 au mi4, kila siku huwa anapokea tu simu zangu. lakini sasa ikija tokea kumetokea dharura na anahitaji kuwasiliana nami anasema hana airtime, unadhani hiyo ni fair?
Kuhusu wababa kusaidia kuangalia wadada endapo mama hayupo hilo halina mjadala, wababa wote wanafanya hilo. Ila naweza kukushangaa sana rafiki mkeo yupo sitting room wewe upo busy kumwelekeza dada jinsi ya kufanya kazi pale nyumbani, utakuwa unafanya kazi si yako.
Have a good day as well:smile-big::smile-big: