Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,753
- Thread starter
- #121
rafiki salama?Rafiki, tunawaachia hawa wasaidizi nyumba zetu, watoto wetu na mali nyingine chungu nzima ndani ya nyumba zetu. Wanatupikia na kufanya kazi nyingine mbali mbali ili kutusaidia katika maisha yetu ya kila siku. Hivyo inabidi tuwathamini na kuwaona kama ni part and parcel ya familia zetu badala ya kuwaona kama ni watu baki na hivyo kuwawekea sheria lukuki, sheria ambazo kama wangekuwa ni ndugu zetu wa damu zisingekuwepo kabisa.
Kama hutaki kubadilisha wasaidizi wako kila baada ya miezi michache basi wasome kwa makini sana akina Miss Kim, Toria na Eiyer na ufuate ushauri wao. Pia badala ya kusubiri mdada akupigie wewe jitahidi katika kila saa kutafuta dakika tano kumpigia ili kujua hali nyumbani ni shwari. Hawa watu ukiwazingua sana kwa sheria lukuki basi wanaweza kabisa kufanya lolote lile ili kukukomoa na kubaki na majuto ni mjukuu.
Good day 🙂🙂🙂
umenielewa lakini?
sina shaka na treatment zangu kwa wadada, hata kama hunifahamu naomba nikuaminishe hilo.
hapa concern yangu ni moja tu, airtime ambayo nampa anipigie kukitokea dharura, na si kitu kingine.
huyu ni mdada wa nne kukaa naye. wa kwanza nilikaa naye kwa miaka 3 na wa pili miaka 9, mi5 akinisaidia kazi na mi4 nikimsomesha ili akitoka hapa aende akajitegemee akiwa na ujuzi wake, hili pia huna choice zaidi ya kuamini tu, lol!
watatu nimekaa naye miaka miwili na huyu sasa ndo mgeni. Hao watatu wote nilikuwa nimewatoa kijijini kwetu ambapo mpaka sasa wao wenyewe pamoja na wazazi wao tumekuwa kama ndugu, hawaachi kuja kunisalimu nikienda kijijini............
hapa naomba pia asome Miss Kim, Eiyer, Phlagiey, Toria, Mashaxizo na wengine
Last edited by a moderator: