Naombeni mwongozo

Naombeni mwongozo

kumbuka mdada namlipa mshahara, kila mwezi, kama ambavyo mimi nalipwa mshahara na bosi wangu na kwenye mshahara wangu sipewi hela ya airtime. ninapopata dharura kupigia ndugu/jamaa na marafiki huwa natumia mshahara wangu. nilitegemea yeye pia akitaka kuwasiliana na ndugu zake atumie mshahara wake. ile ninayompa mimi ni kwa ajili ya kuwasiliana nami

Rafiki that doesnt work....hawa wasichana wa kazi ni kukubaliana tunkwamba vitu vinginr tukubali kuliwa...mfano kwetu anatumia simu yake ila vocha hatumuwekei anatumia hela hizo hizo za matumizi ya kawaida maana huwa tumamwachia hela ya matumizi...ila ndo mpaka tumpigie sisi!
 
nafikiri hujanielewa,

kwa uzoefu wangu mabinti wa kazi hata umetengee 50000 ya simu itaisha pasikupigiwa tena atakua anazirusha hadi kwa wenzie.

cha msingi kama bint ana simu, basi asimpe yake iwe ya kuwasiliana na wenzie yake inatakiwa iwe ya matumiz ya nyumbn kwake

Bado tatizo ni lile lile

Madam,wasichana wa kazi sio vilaza kiasi hiki,hata kama wapo vilaza basi sio wote kwasababu huwezi kumkabidhi mtu nyumba na unaondoka asubuhi na pia unamuachia watoto wako na unarudi jioni unakuta watoto wapo salama na usafi kafanya na mambo mengine kafanya halafu useme ni kilaza kiasi kwamba hajui kupanga matumizi

Zipo familia nyingi sana hawa wasichana ndio wanaobajeti matumizi ya nyumbani huku wanawake wa nyumba husika wakifanya mambo mengine,kwakifupi kwenye familia hizi wasichana wa kazi ndio ambao wanafanya kila kitu ukija kwenye suala la kuibajeti hela ya matumizi na mambo mengine

Huwezi kutaka kuwaaminisha watu kuwa hawa wasichana ni vilaza kiasi hicho,hilo nakataa,kama kunammsichana kilaza hivyo wala hutaweza kukaa nae kwamuda mrefu kwasababu hataweza kutimiza majukumu yake ya kawaida tu,kinachotokea hapa ni hali ya kutaka kuwafanya hawa wasichana wa kazi waonekane kama ni wasiojua wanalolifanya wakati sio kweli kabisa

Kuna wasichana ambao ni bora hata kuliko wamama wa familia husika,kulikana hili ni kuukana ukweli na ndio maana kuna wakati wanaume wa nyumba husika wanasema kuwa ni bora ingefanyika substitution mke akawa HG na HG akawa mke

Ninachotaka kukuambia hapa na huyu mtoa mada ni kuwa hili alilolileta hapa sio halali na halikubaliki kabisa,huwezi kumpa msichana sh 1000 aitumie na ikaisha kabla ya siku utakayompa tena kwenye wiki halafu uje JF kuanzisha uzi

Haikubaliki kabisa na nasema ni unyanyasaji

Kama huyo msichana ni kilaza kwa style unayoileta wewe hafai hata kuwa HG!
 
mkuu mabint adha zao wajua wamama, huyu hata ukimuunga kifurushi cha elfu 10 kwa wiki, itaisha ndani ya siku mbili, kazi hazifanyika, ye anapiga kila atakayembip huko kwao na vijana wa mtaani ndo anawapigia yeye,kifupi hata mtoto hataangaliwa maana anauwezo wa kuongea na simu hata saa 2 na zaidi mfululizo. hapa namsemea msaidizi wangu .cjui ka na huyu yupo hivyo

Huu uongo tafuteni wa kuwalisha lakini mimi hapana

Hawa wasichana wa kazi wanapata wakati mgumu sana huko wanakofanya kazi,kitendo cha kuwazushia mambo ya hovyo kama haya ni kuendelea kujipaka matope

Kama una msichana wa aina hiyo anawezaje kutimiza majukumu yake? Au unataka kujidai kuwa unamvumulia ili uonekane kuwa una huruma?

Sorry,i don't buy that!
 
Thank you rafiki....
Unajua namwelewa sana Eiyer anaposema haya sababu ni mwanaume......
Mimi pia enzi zangu kabla sijawa na nyumba na kuanza kuishi na hawa watu nilikuwa nawaza kama Miss Kim ninapotembelea kwa ndugu zangu wenye mahg, na sasa nina mwelekeo tofauti kabisa na wa enzi zile

Ni jambo gani linaweza kuhalalisha umpe HG sh 1000 wiki nzima kwaajili ya vocha na ikiisha kabla ya hiyo wiki unalalamika hadi hapa JF?
 
Rafiki, tunawaachia hawa wasaidizi nyumba zetu, watoto wetu na mali nyingine chungu nzima ndani ya nyumba zetu. Wanatupikia na kufanya kazi nyingine mbali mbali ili kutusaidia katika maisha yetu ya kila siku. Hivyo inabidi tuwathamini na kuwaona kama ni part and parcel ya familia zetu badala ya kuwaona kama ni watu baki na hivyo kuwawekea sheria lukuki, sheria ambazo kama wangekuwa ni ndugu zetu wa damu zisingekuwepo kabisa.

Kama hutaki kubadilisha wasaidizi wako kila baada ya miezi michache basi wasome kwa makini sana akina Miss Kim, Toria na Eiyer na ufuate ushauri wao. Pia badala ya kusubiri mdada akupigie wewe jitahidi katika kila saa kutafuta dakika tano kumpigia ili kujua hali nyumbani ni shwari. Hawa watu ukiwazingua sana kwa sheria lukuki basi wanaweza kabisa kufanya lolote lile ili kukukomoa na kubaki na majuto ni mjukuu.

Good day 🙂🙂🙂

Asante sana mkuu!!
 
Eiyer anaongea points sana...
Kuna watu wanajifanya hawamuelewi...
This man is brave and Bright...
akina mama msikilizeni huyo jamaa...he is having a point to be taken there,kuwa mwanamke sio kujua kila kitu kuhusu hawa beki tatu...!

CC gfsonwin Fixed Point etc..
 
Last edited by a moderator:
Eiyer anaongea points sana...
Kuna watu wanajifanya hawamuelewi...
This man is brave and Bright...
akina mama msikilizeni huyo jamaa...he is having a point to be taken there,kuwa mwanamke sio kujua kila kitu kuhusu hawa beki tatu...!

CC gfsonwin Fixed Point etc..

Mkuu hawa dada/mama zetu wakati mwingine wanatupa kazi sana kuwaelewesha

Lakini taratibu watatuelewa tu

Pamoja saana ..!!
 
Mkuu hawa dada/mama zetu wakati mwingine wanatupa kazi sana kuwaelewesha

Lakini taratibu watatuelewa tu

Pamoja saana ..!!

Mke wangu mwenyewe ana itikadi hizohizo...hii tabia inanikera kuliko zote duniani...!

Wanasahau maisha ya wanafamilia yapo mikononi mwa beki 3,anaweza akawapoteza wote wakati wowote...

Lazima tuishi nao kibinadamu...!
 
weka vocha kwenye simu hata km anatumia simu yake we nunua simu kwa ajili ya nyumban na uwe unaweka vocha let say 1000/= then unamwambia naomba hii vocha itumike kwenye mambo muhimu tuu na nikikuta imeisha bila sababu maalum jua waz kamshahara kako kanakatwa ...yani kisoda kwa kisoda ..bendera chuma mlingoti chuma
 
Mtoa mada wewe lazima utakuwa kabila la mchaga 1000 tu ndo mishipa inakutoka ivo tena kwa wiki,khaaaa iv hzo hela zako zinaweza kulea mtoto,kudek,kufanya kaz zote,"MAN POWER"ni kitu cha thaman kuliko hela tuwathamini wafanyakaz wetu wanatulelea vijana wa Taifa la keshooo!
 
My dada; one thou a week na ikiisha hutaki akubeep ni mtihani

opt1.. 2500 mon-frdy mwekee jero jero. opt2.. hiyo buku iwe ni ya kukubeep kila kunapotokea tatizo

Hii mishahara ya ma hg ni midogo mnoo jaman ukilinganisha na mahitaji ya mwanamke mnawabana sana ndo mana wanafanyaga makasheshe at the end
My mdogo, unajua namlipa shilingi ngapi?
Ukinisoma kwenye post yangu nimesema huwa napiga sana simu nyumbani, yaani kwa siku napiga zaidi ya mara 3, kwa hiyo inaweza tokea mwezi mzima asiwe na hiyo dharura ya kunipigia, au hata miezi miwili, lakini hiyo haimaanishi kuwa sitampa hiyo buku sababu hakukuwa na dharura.
sasa kinachonichosha ni ile ya kushindwa kuwasiliana nami inapotokea dharura kisa hana airtime na wakati anawasiliana nami mara chache sana baada ya miezi kadhaa
 
mkuu mabint adha zao wajua wamama, huyu hata ukimuunga kifurushi cha elfu 10 kwa wiki, itaisha ndani ya siku mbili, kazi hazifanyika, ye anapiga kila atakayembip huko kwao na vijana wa mtaani ndo anawapigia yeye,kifupi hata mtoto hataangaliwa maana anauwezo wa kuongea na simu hata saa 2 na zaidi mfululizo. hapa namsemea msaidizi wangu .cjui ka na huyu yupo hivyo
You know mabinti wa kazi very well.
Hao wakijiunga ni wanahakikisha sms zote ziishe na airtime, ndo mambo mengine yaende.
 
Fixed Point!
Fixed Point!
Fixed Point!

Back 3 ni binadamu kama binadamu wengine!

Wanainterests and/or mahitaji kama walivyo binadamu wengine!

Na ni wafanyakazi kama wafanyakazi wengine (like you!)

Ivi kwa mujibu wa maelezo yako hapo reds, Unamtofautisha vipi back 3 na Mtumwa?

Ivi unakubali wafanyakazi wote watritiwe kama maelezo yako ya second red?

In treatment, unawatofautisha viki wafanyakazi wa ndani na wafanyakazi wengine?

Plz Fixed Point treat your back 3 like your children in reasonable manner!
Hako karesearch ulikokafanya ndio kanakutia matatani dhidi ya hao/huyo back 3 wako thus why unaquestion vocha ya Buku 1 kwa wiki dhidi ya back 3 wako!

Change your mind! Treat them like a human, im sure utakuja kuleta ushuhuda hapa!
umeni-judge kwa vitu nisivyovifanya......
hayo maandishi meusi ambayo umeyakimbia ndo nimesema mimi huwa nafanya, hayo mengine ni maelezo tu na nimeweka clear kuwa sifanyi hayo
 
Mie huwa sijitii headache na maid hata siku moja. Kwa suala hili uliloleta hapa, nakushauri ununue mobile fone ya mezani. Nenda voda hapo wanakupa lisimu la mkonge, ukiwa nyumbani unawaka halijafutwa vumbi. Hicho kimobile ndo kwanza unampigia yuko mtaa wa tatu na anakujibu niko home, hali shwari!

but anyways, kukaa na msichana ukimfanya comfortable utafaidi wewe. Mpigie wewe, tena mruhusu akutumie msg ya tafadhali nipigie kama ana shida yoyote. Tena jumapili kaa na wanao, muache dada akabarizi kwa maboifrendi. jirani wa kakangu alikuwa mkali hapo UDSM, hgal haruhusiwi kupiga picha hata na mwanae wala wanae hawaruhusiwi kwenda kwa jirani. Siku mwanae alikuwa anaharisha, kina dada wakakaa kimya tu na sie tuko home tunaangalia tv tu. By the time mama mtoto anarudi saa moja usiku, anakamata mwanae kwenda hospitali, mtoto anafariki!

mtoto anaweza kuungua ama kuumia mbele yako na usiweze kumlinda. Relax
 
well, sijui ni kwasabb ya uzee ama??
binfs napenda sana kuona mtu anaheshimiwa lkn nikionacho kwa waajiri wengi wa beki 3 hushindwa kutofautisha kati ya beki 3, na mtu mwingine hapo nyumban. sababu kubwa ni kwamba huona kama beki 3 anatakiwa kubembelezwa na atritiwe kama yai jambo ambalo pia hawawez kulifikia.

beki 3 anatakiwa apewe majukumu yake na atambue kwamba yupo kazin na alipwe kulingana na mapatano, mpaka uwepo kati yake na mwajiri wake kazi zake zirasimishwe kama wafanyavyo wahindi mbona hua wanakaa muda mrefu na kw nidhamu sii wabongo kwa kujtia umalaika ndo tunakutanaga na haya.
well said rafiki.....
 
Hata usalama wa mali zako zote uko mikononi kwa hgal. Kuna siku nilirudi home mapemaa, nikakuta dada hayupo. Nikaingia ndani, nikalala. By 6pm naamka nyumba iko kimya kabisa. Ndio nagundua dada hayupo. Angeweza kuamua kuacha nyumba wazi ama kubeba apendacho. Lakini hadi change za dukani nilikuta mezani, alipika na kuacha hapo kabisa.

ndo maana mimi husema mwanaume akitembea na hgal anaweka familia nzima vulnerable. Akiamua kufanya wivu wa mapenzi humo ndani, hakutasalia hata panya
Mke wangu mwenyewe ana itikadi hizohizo...hii tabia inanikera kuliko zote duniani...!

Wanasahau maisha ya wanafamilia yapo mikononi mwa beki 3,anaweza akawapoteza wote wakati wowote...

Lazima tuishi nao kibinadamu...!
 
ha haaaaa, nimecheka sana........
tatizo nililoliona kwako na kwa baadhi ya watu ambao wamejibu swali langu kwa hisia ni kutokuelewa nilichokiandika. Jamani, watu wengi wanafeli mitihani siyo sababu hawajui kitu katika topic husika, ila sababu anajitahidi kuelezea vitu ambavyo havipo kwenye swali. Hata kama umeambiwa discuss, haimaanishi uandike kila unachokijua kwenye hiyo topic, chagua vitu muhimu ambavyo vimeulizwa.
Kaa tena na hao uliowaita, mshauriane swali linahusu nini, specifically, then uje utoe mwongozo.
Acha kujibu kwa hisia
Kabla haujaliona hilo kama tatizo na kuja kuomba muongozo ulipaswa kwanza kujichunguza ili ugundue kikwazo ni kipi.
Pili yakupasa kuelewa kwamba mdada wakazi na yeye pia ana maisha yake anahitaji kuwa huru kufanya baadhi ya mambo yake ambayo hayatavunja misingi ya kazi yake, katika hili swala lako yapo mambo mengi sana ya kuyatazama kiundani zaidi, umedai mara kwa mara huwa unapiga simu sitaki kuuamini kwamba hizo dharura huwa zinategea na kutokea wakati ambao haupigi simu.

Tatizo liko kwenye mitazamo yenu na jinsi mnavyo wachukulia hao wadogo zetu wanapokuja kuwafanyia kazi huko majumbani kwenu, kwanza kabisa kiasi cha pesa mnachowalipa hakiendani kabisa na majuku mnayowatwisha, na pia hauwezi kugharamia mahitaji yake yote, haiitajiki kuchukua maelezo yako mengi ili mtu akusome jinsi unayoishi na binti yako wakazi, kwa maelezo hayo tu inaonesha na wewe ni mmoja kati ya watu wanaoishi na wadada wandani kwa kuwaendesha kama magari mabovu huku mkiwalipa kiasi kidogo cha pesa.

Nafikiri ungekuwa unamlipa kiasi kizuri cha pesa hata usingekuwa unatoa hiyo 1000 kwaajili ya simu, angeweza kulimudu hili kwa vile na yeye mawasiliano kwake ni muhimu kwa ndugu na jamaa zake. kama kweli kiasi cha pesa unachomlipa kinamtosheleza na hiyo 1000 unayotoa, swali la kujiuliza ni kwamba je, ni mzembe kutoa taarifa inapotokea dharura? kama jibu ni hapana, na sababu ni simu haina vocha basi tunarudi kule kule kwenye malipo unayomlipa ni kidogo.

Kweli pesa ni ngumu, na hakuna pesa ndogo, pia ukidharau mia hauwezi kupata 1000, hivyo bajeti ni muhimu swala la msingi ni je kiasi cha bajeti yako kinatosheleza mahitaji ya dada wa nyumabani?...

Swali la kizushi..

Ikitokea huyo mdada wako wa kazi akawa anakupigia simu mara kwa mara hata kama dharura haijatokea na mara nyingine awe anakurushia salio hata 1500, wakati huo wewe huwa unamuachia 1000 kwa wiki, utajifikiria nini juu ya huyo mdada? na utachukua hatua gani?

CC; kiwatengu , The Boss , Mrigariga, ICHANA , Nokia83 , dyuteromaikota , hips.com , Caroline , danzi , Munambefu , Mashaxizo , everlenk , Joseph , Bulldog , Eiyer, Mr mgeni, stroke, byb sac, gfsonwin, Honey Faith, bornagain, thinky, isha, Miss Kim, frank wa moyo, Chauro, Mbu, Escardo-bird, Natanguliza samahani kwa usumbufu kwa kuwakusanya hapa, kilichonifanya niwakusanye hapa naomba muwe watazamaji atakacho nijibu Fixed Point
 
Back
Top Bottom