Naombeni mwongozo

Naombeni mwongozo

Usijali rafiki.....
Pamoja sana

Fixed Point!
We differ on how we understand and how we translates!

Maandisi yakiekewa red yanamaana yake!
Nilichojibu niliegemea kwenye maandishi yako mwenyewe! Kwa lugha nyepesi 1 (first red) + 1 (second red) = 2 (nilichokujibu) instead of 5 (ya maelezo yako underline) that is how lawyer makes inference from specific to general!

Hiyo haina maana kwamba ndivyo ufanyavyo! Hiyo ni tafsiri tu! Sikujui, hivyo sina uwezo wa kukujudge! Naomba unielewe kwa hilo!

And if umehisi nimekukosea naomba unisamehe!
Love you so much my dada!

I like the way you argue!
Pamoja sana!
 
simu ya nyumbani ndo ambayo anaitumia, in case hana yake, na tatizo bado ni lile lile.
Ukweli kati ya watu wanaopiga simu nyumbani mara kwa mara ni mimi, na ndo maana anaweza kukaa wiki nzima hajanipigia. lakini sasa inatokea umepiga tu baada ya muda kukatokea dharura, labda mgeni kaja au chochote kile ambapo dada inabidi anitaarifu; sheshe ndo linaanzia hapo.

Weka bando ya wiki, tena kama ni airtel sh elfu ngapi hyo tosha kabisa, halafu vocha uwe unaweka mwenyewe kwenye hiyo simu, kama ni simu yake aweke kwa pesa yake mwenyewe, wewe weka hiyo yako ya nyumbni hiyo vocha.
 
Watu wanadhani ma hausgel hawatakiwi kuwa na social life kama watu wengine
Uuwwwiiiiii, wewe ndo umekuja na mjadala mwingine kabisaaaaaaa, nje ya nilichoombea mwongozo.....
kama wewe ndo Spika, tunapiga kura ya kutokuwa na imani nawe
 
Weka bando ya wiki, tena kama ni airtel sh elfu ngapi hyo tosha kabisa, halafu vocha uwe unaweka mwenyewe kwenye hiyo simu, kama ni simu yake aweke kwa pesa yake mwenyewe, wewe weka hiyo yako ya nyumbni hiyo vocha.
Asante kwa mwongozo.....
Pamoja sana
 
Me nadhan hili tatizo ni gum kulizuia...just imagine hata wewe ukiwa ofisini ukitaka labda kuprint cv/picha au kutuma personal email do you go to the Internet cafe?..si unatumia ya ofisi?...mfano mwingn ni simu ya ofisi,lazima kuna siku utajiibaiba and make personal calls....my point is umueleweshe tu huyo mdada kwamba awe anabakisha walau ela ya msg au ku beep
 
najua kinacho kupa mashaka hasa ni usalama wa nyumbani kwako hasa ukiwa na mtoto, vocha mpe ila kiboko ya njia funga cctv pasipo yeye jua pia gharama yake ni kama laki nne ivi kwa maana ya kwamba utapata full matukio kama yafuatao
1. kama mtoto ana mtrit vibaya utajua
2.kama ana tabia ya kuleta vinjemba na kugeuza nyumba yako lodge utajua haraka
3.utajua matumizi ya simu yake kwa kusikia anaongea nn
4.kama mr anamkamua beki 3 nayo itakusaidia
5.kama anatabia ya upashukuna wa kuleta marafiki kwako utamjua
faida yake hata kama una panga chumba kimoja utapata taarifa za uhakika na kuzichukulia hatua fasta, nimefanya ivo adi beki tatu anaisi mie ni mchawi.....

Akili za usiku...!
 
Uuwwwiiiiii, wewe ndo umekuja na mjadala mwingine kabisaaaaaaa, nje ya nilichoombea mwongozo.....
kama wewe ndo Spika, tunapiga kura ya kutokuwa na imani nawe

Nimeelewa ulichosema ndo mana nikaongeza point hapo
 
anajua kutumia bundle ila sasa hela yooote inaishia kupiga simu zake anazozijua

ndugu zangu, simu ni sumu kwa beki 3. kuna 1 nilimtoa huko kijijini alikuwa ametulia lakini baada ya kumpa simu imekuwa balaa. ameshoboka na hivyo vivulana mpaka natamani nimnunulie land line ya ttcl. akiwekewa salio halichukui muda kuisha na ameingiza caller tunes kwenye simu sijui hata nani kamfundisha--nadhani vitakuwa hivyo vivulana vyake.

sasa simuwekei salio lolote kwenye simu. majina ya 'mama' na 'baba' nimeyasevu kwa kutumia kanuni ya TAFADHALI NIPIGIE. ikitokea emergency akipiga simu hata kama haina salio napata ujumbe kwenye simu yangu ninampigia. nimefunga (bar) all outgoing calls na nataka niende Vodacom wafunge incoming SMS (SMT) kuzuia wavulana wake wasimtumie sms ili atulie alee mtoto--najua hawawezi ku-afford kumpigia daily. nadhani hii itasaidia.
 
Asante rafiki.
Ila sasa nikiiblock kupiga namba nyingine si nitakuwa namwonea? akitaka kuongea na wazazi wake au ndugu wengine itakuwaje?

akitaka kuongea na ndugu asubiri ukitoka kazini awapigie kwa simu yako. hao 'ndugu' unao-entertain ndio watamfanya akose umakini wa kufanya kazi kwa ufasaha.
 
Bwana tpaul hii picha yako inanipaga burudani sana... Ukiona mwanaume amelia hivyo... ni hataree aiseee!!!

simu ya home ndiyo hiyohiyo ya beki 3 au wewe unaongelea simu ya home ipi?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
wanawake wengi wapo hivo....unaweza mtumia vocha ya elf 5 akakuandikia msg moja tu ya 'thanx'. baada ya hapo husikii chochote mpaka vocha uliyompa iishe ndo atabeep then anaomba vocha

MAJANGA! Tena wakati anakuomba airtime ndipo utasikia akikuita 'BABY' baada ya kumtumia vocha hakuna cha babe wala mjusi. Hawa viumbe wewe waone hivohivo, hawafai kabisa!
 
Marufuku kumpa vochaaa cjui umenielewa wewe weka utaratibu Wa kumpigia at least Mara kwa Mara uwapo kazini na ikitokea kuna tatizo mfundishe jinsi ya kutuma pliz kol mi basiiii maana ukimpa vocha atapigia watu anaojuana nao yeye sasa ikitokea ndg zake wanashida nae wampigie au Siku nyingine unatumia simu yako kuwasalimia then unampa nae asalim tuuu hapo utaishi freshhh na huyo muguro mpya ila ukiendekeza vocha utalia. yalishanikuta ndo maana nimeweka sheria mpya. So jaribu kama utaipenda.nawasilisha

hahaha! umenikumbusha mbali na hiyo terminology ya MUGRO. hiyo term tumeitumia sana tukiwa chuoni-- kampasi ya mazimbu (now Solomon Mahlangu Campus).
 
Mmh!
Mi nadhani tukiwachukulia wafanyakazi wa ndani kama wafanyakazi tu, matatizo hayataisha!

Either tunapaswa kuwachukulia kama wenetu and/or rafiki zetu!

From my point of view, haipendezi kumlimit beki 3 kwenye mambo ya mawasiliano eti kisa tu simu umempa wewe and/or umemuekea vocha ya buku kwa wiki 1!
...
Jamani nimeongea hayo kiroho safi na nadhani nimeeleweka!

mkuu inaonekana huwajui mabeki 3 wewe--huna uzoefu nao hata kidogo. ngoma usiyoijua, usiicheze!
 
Wewe endelea na utaratibu wa kupiga simu mara kwa mara,inapotokea dharura achukue hela akupigie,I hope pamoja nakuhakikisha kila kitu kipo ndani kuna ka hela unaacha kwa dharura mbalimbali basi achukue hapo na jioni anakupa mrejesho wa matumizi. Au kama kuna duka hapo karibu unamuomba mwenye duka kama dharura imetokea ampatie vocha asimpe chochote bila ya kuwasiliana na wewe.

Mimi hutumia njia hizi na hamna tatizo kabisa,nahakikisha hela ya dharura kama buku 5 haikosekani na jioni namuomba anipe mrejesho wa matumizi yake.

swadakta! hii njia nayo iko poa sana. au unaweza kuwa unamwachia hata 1000 kwa ajili ya hiyo dharula--maana yake ni kwamba hiyo itaendelea kuwepo hadi dharula itakapojitokeza, kuliko ukiiweka kwenye cm halafu beki 3 anaitumia kuwasiliana na vibuzi vyake badala ya kuzingatia kazi.
 
ha haaa, last week nilisafiri, nilihakikisha ndani kuna kila kitu ila nikaacha elfu 10 ya dharura. niliporudi nikaona watu hawanipi mrejesho, nikaomba wanipe mrejesho, walikuwa wadada wawili. Unajua walichonifanyia?
waliniandikia walinunua pads box 3, eti wote walianza period...... nilibaki nacheka tu.

unaona sasa? ngoja wale wanaodhani beki 3 wanaonewa waone shughuli yao ilivyo pevu. mnaona mambo haya?
 
Huyo mfanyakazi hana ndugu?Tuseme dharula unazo wewe tu ila yeye hana dharula?Wewe umewekewa masharti ya kutumia simu na nani na shilingi ngapi kwa wiki?

elewa somo kwanza kabla ya kutema povu. hakuna mtu aliyemzuia kuwasiliana ila aweke fedha zake, asitumie vibaya mali ya mwajiri.

imagine umemtumia mwanao karo halafu amechukua amekula yote kisha akarudishwa home. unapomuuliza anakuambia alichukua pesa ya karo akachezea kamari! utamuelewa?
 
Back
Top Bottom