Naombeni mwongozo

Naombeni mwongozo

wanawake wengi wapo hivo....unaweza mtumia vocha ya elf 5 akakuandikia msg moja tu ya 'thanx'. baada ya hapo husikii chochote mpaka vocha uliyompa iishe ndo atabeep then anaomba vocha
 
Mwanangu ananifurahisha tukirudi jioni anatoa taarifa ya kila kitu ambacho sio cha kawaida kilichotokea home
hata wangu huwa tunawaita maripota, maana tunahadithiwa kila kitu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Marufuku kumpa vochaaa cjui umenielewa wewe weka utaratibu Wa kumpigia at least Mara kwa Mara uwapo kazini na ikitokea kuna tatizo mfundishe jinsi ya kutuma pliz kol mi basiiii maana ukimpa vocha atapigia watu anaojuana nao yeye sasa ikitokea ndg zake wanashida nae wampigie au Siku nyingine unatumia simu yako kuwasalimia then unampa nae asalim tuuu hapo utaishi freshhh na huyo muguro mpya ila ukiendekeza vocha utalia. yalishanikuta ndo maana nimeweka sheria mpya. So jaribu kama utaipenda.nawasilisha
 
wanawake wengi wapo hivo....unaweza mtumia vocha ya elf 5 akakuandikia msg moja tu ya 'thanx'. baada ya hapo husikii chochote mpaka vocha uliyompa iishe ndo atabeep then anaomba vocha
ha ha ahaaaa, pole sana......
hii ni habari nyingine sasa.
sijui mnawapataga wapi wadada wa hivi?
cc. The Boss
 
Last edited by a moderator:
Marufuku kumpa vochaaa cjui umenielewa wewe weka utaratibu Wa kumpigia at least Mara kwa Mara uwapo kazini na ikitokea kuna tatizo mfundishe jinsi ya kutuma pliz kol mi basiiii maana ukimpa vocha atapigia watu anaojuana nao yeye sasa ikitokea ndg zake wanashida nae wampigie au Siku nyingine unatumia simu yako kuwasalimia then unampa nae asalim tuuu hapo utaishi freshhh na huyo muguro mpya ila ukiendekeza vocha utalia. yalishanikuta ndo maana nimeweka sheria mpya. So jaribu kama utaipenda.nawasilisha
Nimekuelewa sana na natamani nifanye hivyo.
sijui umenisoma huwa napiga sana simu nyumbani. na sms kwangu huwa sizi-treat kama dharura. yaani nikiwa busy sms ikiingina hata sishtuki naweza iona jioni. sasa hiyo please call me inaweza ikakesha kumbe kuna dharura
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nawasalimu wana MMU.
Jamani tuna hawa wadada wanatusaidia kukaa na nyumba zetu. Kama tujuavyo maisha ya siku hizi bila simu inakuwa patashika kidogo. Huwa mdada akija kama hana simu huwa nampa simu ambayo nimeinunua kwa ajili ya nyumbani ili niweze kuwasiliana naye naye awasiliane nami ambapo sipo nyumbani. Na kama inatokea mdada kaja na simu yake basi simlazimishi atumie ile yangu, huwa natumia tu ile namba yake kwa mawasiliano.
Kinachotokea mpaka naomba mwongozo hapa ni kwamba; Huwa nampa sh. 1000 kila wiki kwa ajili ya simu, ili akipata dharura basi aweze kunitaarifu. Mara nyingi mimi huwa napiga simu nyumbani mara kwa mara kwa hiyo inatokea mara nyingi tu ndani ya wiki hajanipigia wala kutuma sms hata moja, na yaweza kuwa hivyo hata mwezi mzima. Kinachonichosha, siku ikitokea kapata dharura wala hapigi, nikiuliza naambiwa simu haina hela.
Wenzangu pia mnakumbwa na hili tatizo? nifanyeje sasa ili hili tatizo liishe? sababu wakati mwingine ni jambo la maana kabisa linatokea lakini hawezi kuniambia kisa hela kwenye simu kamaliza zoote kupigia watu wake, sasa maana yoooteee ya mimi kumpa hela ya simu inakuwa haipo.
Nimepata mdada mpya sasa nataka nianze naye tangu mwanzo sheria ya hela yangu ya simu iweje........

Usiweke hela, piga wewe all the time unataka kujua ya nyumbani. Mfundishe kutuma message tafadhali nipigie. Basi
 
Mwanangu ananifurahisha tukirudi jioni anatoa taarifa ya kila kitu ambacho sio cha kawaida kilichotokea home
Siku atamfungia kwenye friji anapofanya hayo mambo yake ndio furaha yako itaisha maana mabeki 3 wamevurugwa hasa.
 
Mmh!
Mi nadhani tukiwachukulia wafanyakazi wa ndani kama wafanyakazi tu, matatizo hayataisha!

Either tunapaswa kuwachukulia kama wenetu and/or rafiki zetu!

From my point of view, haipendezi kumlimit beki 3 kwenye mambo ya mawasiliano eti kisa tu simu umempa wewe and/or umemuekea vocha ya buku kwa wiki 1!
...
Jamani nimeongea hayo kiroho safi na nadhani nimeeleweka!
 
Mmh!
Mi nadhani tukiwachukulia wafanyakazi wa ndani kama wafanyakazi tu, matatizo hayataisha!

Either tunapaswa kuwachukulia kama wenetu and/or rafiki zetu!

From my point of view, haipendezi kumlimit beki 3 kwenye mambo ya mawasiliano eti kisa tu simu umempa wewe and/or umemuekea vocha ya buku kwa wiki 1!
...
Jamani nimeongea hayo kiroho safi na nadhani nimeeleweka!
ndo ambavyo mimi nimejitahidi sana kufanya......
lakini unaonaje unapompa mwanao simu + airtime kwa lengo la kuwasiliana nawe anapopata dharura halafu inatokea kila anapokuwa na dharura hana airtime kwa ajili ya kukujulisha?
 
Wewe endelea na utaratibu wa kupiga simu mara kwa mara,inapotokea dharura achukue hela akupigie,I hope pamoja nakuhakikisha kila kitu kipo ndani kuna ka hela unaacha kwa dharura mbalimbali basi achukue hapo na jioni anakupa mrejesho wa matumizi. Au kama kuna duka hapo karibu unamuomba mwenye duka kama dharura imetokea ampatie vocha asimpe chochote bila ya kuwasiliana na wewe.

Mimi hutumia njia hizi na hamna tatizo kabisa,nahakikisha hela ya dharura kama buku 5 haikosekani na jioni namuomba anipe mrejesho wa matumizi yake.
 
ndo ambavyo mimi nimejitahidi sana kufanya......
lakini unaonaje unapompa mwanao simu + airtime kwa lengo la kuwasiliana nawe anapopata dharura halafu inatokea kila anapokuwa na dharura hana airtime kwa ajili ya kukujulisha?

Yap! Nikubaliane nawe kwamba sometimes unaweza kutumia rule zote za morality na mtu mkashindwana!

If nimetake all reasonable care kwa mwanangu (kumpatia means za mawasiliano) na akafanya kinyume chake! First step ni kusitisha huduma ili apate funzo, then yule ni mwanangu isifikie mahali nikasema amenishinda! Nitakwenda naye hivyo hivyo!

Hiyo ni tofauti na back 3 ambaye sina ulazima wa kumng'ang'ania! Tukishindwana ni kumuondosha tu!
...
Hapa ningependa ukumbuke kuwa, kutatua tatizo kunaweza kukazaa tatizo! Ila kutatua chanzo cha tatizo ndio suluhu la tatizo! (Mmh unielewa kweli hapo?)

Mf: Serikali imeharamisha abortion, but uzinifu umekatazwa kwa watoto chini ya 18 na kwa wanandoa! Wakati ni ruksa kwa wote waliobaki!

si umeona logic ya hapo?
...
 
Wewe endelea na utaratibu wa kupiga simu mara kwa mara,inapotokea dharura achukue hela akupigie,I hope pamoja nakuhakikisha kila kitu kipo ndani kuna ka hela unaacha kwa dharura mbalimbali basi achukue hapo na jioni anakupa mrejesho wa matumizi. Au kama kuna duka hapo karibu unamuomba mwenye duka kama dharura imetokea ampatie vocha asimpe chochote bila ya kuwasiliana na wewe.

Mimi hutumia njia hizi na hamna tatizo kabisa,nahakikisha hela ya dharura kama buku 5 haikosekani na jioni namuomba anipe mrejesho wa matumizi yake.
ha haaa, last week nilisafiri, nilihakikisha ndani kuna kila kitu ila nikaacha elfu 10 ya dharura. niliporudi nikaona watu hawanipi mrejesho, nikaomba wanipe mrejesho, walikuwa wadada wawili. Unajua walichonifanyia?
waliniandikia walinunua pads box 3, eti wote walianza period...... nilibaki nacheka tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Huyo mfanyakazi hana ndugu?Tuseme dharula unazo wewe tu ila yeye hana dharula?Wewe umewekewa masharti ya kutumia simu na nani na shilingi ngapi kwa wiki?
 
anajua kutumia bundle ila sasa hela yooote inaishia kupiga simu zake anazozijua

Kuna mini kabang ya tigo 3500 tu, unapewa dk 75 sms 2000 na mb 500

Ukiunganisha anakuwa hana sababu nyingine.
 
mkuu hawa beki 3 ni changamoto kwa kweli ukisema umlimit ndo utaumia kabisa hata mtoto anaweza akaugua gafla akashindwa kukupa taarifa chamsingi nunua sim ya mezani alafu unaunganisha laini moja tu ya kwako akipiga sehem nyingine sim haiendi hapo utakua umemkomesha
 
Huyo mfanyakazi hana ndugu?Tuseme dharula unazo wewe tu ila yeye hana dharula?Wewe umewekewa masharti ya kutumia simu na nani na shilingi ngapi kwa wiki?
kumbuka mdada namlipa mshahara, kila mwezi, kama ambavyo mimi nalipwa mshahara na bosi wangu na kwenye mshahara wangu sipewi hela ya airtime. ninapopata dharura kupigia ndugu/jamaa na marafiki huwa natumia mshahara wangu. nilitegemea yeye pia akitaka kuwasiliana na ndugu zake atumie mshahara wake. ile ninayompa mimi ni kwa ajili ya kuwasiliana nami
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mkuu hawa beki 3 ni changamoto kwa kweli ukisema umlimit ndo utaumia kabisa hata mtoto anaweza akaugua gafla akashindwa kukupa taarifa chamsingi nunua sim ya mezani alafu unaunganisha laini moja tu ya kwako akipiga sehem nyingine sim haiendi hapo utakua umemkomesha
asante kwa ushauri
 
  • Thanks
Reactions: BAK
ha haaa, last week nilisafiri, nilihakikisha ndani kuna kila kitu ila nikaacha elfu 10 ya dharura. niliporudi nikaona watu hawanipi mrejesho, nikaomba wanipe mrejesho, walikuwa wadada wawili. Unajua walichonifanyia?
waliniandikia walinunua pads box 3, eti wote walianza period...... nilibaki nacheka tu.
Hahahaha! Changamoto kama hizo zipo unakabiliana nazo,sometimes inabidi uact umafia,mimi mwenyewe nikipewa mrejesho ambao si sawa nakuwa mbogo kwelikweli, hii imesaidia kuleta adabu ya matumizi binafsi,kabla hajatumia lazima anitaarifu kisha ndo nimruhusu atumie au la. Vipi bado uko na hao wasichana wawili nikupe mbinu ya kuishi nao au mmoja kesha ondoka?
 
Back
Top Bottom