Easy Chair Mark III
JF-Expert Member
- Aug 19, 2019
- 897
- 1,373
Nina mshkaji wangu..
Ni best sanaa, tulikutana ajirani serikalini...
Baada ya kuona maisha ya ajira HAYAENDI tuliamua kuacha kazi na kufanya yetu, Mimi niliamua kwanza kwenda shule na yeye alianza kufanya yake (kujiajiri)...
Sasa nilivyo maliza chuo na kuanza na Mimi misele nilimkuta yupo mbali na kwa rehema za Mungu nilimkuta ana Mali kiasi (ukilinganisha na tulivyokua ajirani)....
Maisha yalisonga akaoa..
Ila Tabuu inakuja hapa...
Ndoa yao inamiaka mitatu na shemeji (mkewe) kapeleka ombi mahakamani la Talaka, kwa taarifa chini ya carpet "X wake wa China (alienda kusoma) karudi, then anataka kuhamia kwa X"...
Na anataka Mali zotee wagawane "MPAKA ZILE ALIZOMKUTA NAZO MSHIKAJI""
Rafiki yangu ye anasema "WATAGAWANA ZILE WALIZOCHUMA KWENYE NDOA YAO" ila alizomkuta nazo kama mashamba (Zaidi ya eka 50), nyumba ya biashara na ana miti mingii kapanda Njombe HATAKI WAGAWANE ila shemeji KAKOMAA ANATAKA 50 - 50..
NIMELILETA KWENU MJARIBU KUMSAIDIA...
Mwenye kujua anipe hata SECTIONS na ARTICLES za LAW niweze KUMSAIDIA MSHIKAJI WANGU.
Yaani ni MY BEST FRIEND BALAA..
TUMETOKA MBALI, NAMUONA KABISA ANAPOTEA KWA STRESS
Bia hazipandi tena..
Kitimoto ndio kabisa hataki...
Zile outing za kwenda kula nyama kwa wamasai ukimletea NOWDAYS anahisi kama unamng'ong'a....
Mtu pekee anayeweza Kuongea nae kwasasa ni Mimi tu wengine wotee hataki...
Yaani mpaka baadhi ya biashara zake nimechukua ili NIZIOKOE...
Sasa AMBAO MLIPITIA HAYA au MNAJUA HAYA MAMBO, TAFADHALINI "NAOMBA MNIPE DIRECTION NIMUOKEA MY BEST BROTHER IN THE WORLD""
#ASANTE
#YNWA
Kesi kama hizi bado zitaendelea kutokea tu huko nyumbani Tanzania??
Wanaume wenzangu bado tu hamjifunzi kuhusiana na mambo haya??
Namna pole yake sana.
Lakini nina maswali haya ya kumuuliza huyo rafiki yako:-
A: KUHUSU FAMILIA
1.Je amezaa naye watoto? Wangapi?
B: KUHUSU MASHAMBA NA ARDHI:-
2.J e mashamba hayo yamepimwa??
2.1 Kama jibu ni ndiyo, yamepinwa lini?
2.2 Anazo nyaraka zozote kuhusiana na upimaji huo, eg. ramani za upimaji, voucher za malipo ya gharama? nyaraka za kampuni iliyopima hayo mashamba/ardhi?
2.3 Kana mashamba/ardhi hiyo haijapimwa, je mashamba hayo aliyapataje?
2.4 Aliyapata lini hayo mashamba?
2.5 Aliyanunua?Alipewa kama zawadi?Aliyarithi?Kutoka KWA nani?
2.6 Kuna nyaraka zozote za kumiliki hayo mashamba?
2.7 kama nyaraka zipo, zina majina ya nani? Za lini/date?
2.8 Kama alinunua, je mashahidi walikuwepo? Kama walikuwepo, he bado wapo hai mpaka Leo??
C: KUHUSU MAJENGO:-
3.Je hizo nyumba alizijenga lini?
3.1 Alijenga kabla au baada ya ndoa?
3.2 Je mwanamke alipoolewa NA huyo jamaa yako alizikuta hizo nyumba tayari zimekamilika kujenga? Alizikuta ziko tayari?
3.3 Je anazo risiti/stakabadhi za manunuzi ya vifaa vya ujenzi KWA hizo nyumba?
3.4 Kama hana hizo risiti, Je ana kitu gani/ushahidi gani wa kuthibitisha kuwa nyumba hizo alizijenga yeye mwenyewe binafsi KWA gharama zake bila ya ushiriki wa huyo mwanamke?? Ana ushahidi wowote ule??
3.5 Je mafundi ujenzi wa hizo nyumba bado wapo hai mpaka Leo hii?
3.6 Kama mafundi ujenzi waliojenga hizo nyumba bado wapo hao, Je wapo upande UPI ktk kuthibitisha uhalali wa umiliki wa hizo nyumba?? Upande wa mwanamke au mwanaume??
D: KUHUSU MALI ZINGINE ZINAZOHAMISHIKA
4.Je hizo Mali alizipataje? Alizinunua ?
4.1 Kama alizinunua, Je bado anazo risiti/stakabadhi za manunuzi?
4.2 Alizinunua lini?
4.3 Anao ushahidi wa kuthibitisha kuwa alizinunua akiwa peke yake bila ya ushiriki wa mwenza wake??
4.4 Kama hana nyaraka zozote, anaweza akanicheki Pm KWA ushauri zaidi,
E: HITIMISHO NA USHAURI WA BURE
5.KWA WANANDOA WATARAJIWA WOTE
KWA Watu wote wenye Mali ambao bado hawajaingia kwenye ndoa {Aidha Mwanamke au Mwanaume),
MNASHAURIWA KUSAJILI MALI ZENU ZOTE KISHERIA KABLA HAMJAINGIA KWENYE NDOA ILI ZISIJUMUISHWE KWENYE MALI ZA NDOA (MATRIMONIAL PROPERTY) MARA BAADA YA MHUSIKA KUINGIA KWENYE NDOA ILI KUEPUKA KUINGIZWA KWENYE JANGA LA UTAPELI WA MAPENZI