Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

inahusu

Member
Joined
Apr 28, 2015
Posts
12
Reaction score
2
Habari zenu,

Ni hivi nimeolewa, mume wangu ana watoto 2 kabla ya ndoa yetu nasi tuna watoto wawili. Wote ni waajiriwa nje ya jiji la DSM. Baada ya kuoana tukaanza maisha nikajikuta naachiwa majukumu ya kutunza nyumba. Jamaa kila nikimuuliza anasema hana hela na haishi sababu ambazo mimi zikawa zinanitia shaka. Nikavumilia nikawa natoa hela maisha yanakwenda kama kawaida pale home.

Ikafika kipindi nikaamua kuchunguza kweli hana hela? Nikawa nakuta deposit slip jamaa ana deposit hela kwenye account yake, nikichungulia wallet yake ina hela wekundu wa kutosha n.k. Nikimuomba hela za kuhudumia home anasema hana, nikamuuliza mbona kwenye wallet yako zipo akasema sio zake! Nikaanza kuhisi naibiwa mchana, nikabana uchumi pale home nikawa napika dona na mlenda, dagaa kwa sana basi jamaa baada ya muda akaanza kutoa hela kidogo kidogo.

Chukua hii nunua mchele na kuku! Hahaha kumbe dona na mlenda inachosha anyway nisiwachoshe, jamaa baada ya kipindi cha miezi kadhaa jamaa akarekebika na tukawa tunaishi vizuri tu. Linalonileta hapa ni kuwa sasa mume wangu anataka tujenge wote nyumba kwenye kiwanja chenye jina lake. Jamani naingiwa na ubaridi. Inakuwaje hapa? Ukizingatia background hiyo hapo juu, huyu mtu kabadilika kweli?

Najiuliza sasa tena tujenge wote kwenye kiwanja chake? Pia mwenzangu ana watoto 4 mie nina wawili, hii inakuwaje? Mama wa watoto hawa yu hai na ana uwezo tu kwanini mie nijinyime nijenge kujengea wanne na baba yao? Jamani nakuwa na roho ya kichoyo au nakaribia kuibiwa mchana? Nimejaribu kuzungumza na mume wangu kumwambia japo tutafute kuwanja cha pamoja tujenge huko ila akahamaki na kuanza kunishutumu nina roho mbaya.
Ni sawa mie kujenga nae hapo?

Naomba ushauri
 
ndio maana yule alokuja na uzi "msimamo wagu" hajakosea.

ni kosa kubwa kutunza familia mwenyewe na mtu kaajiriwa anakosaje hela? mshahara ukitoka wewe hujui tarehe za mshahara au? mi naona nawew ni mzembe hana hela unanyamaza tu salary kapeleka wapi. mtoto umleavyo ndivyo akuavyo .any way labda ndo u wife material uloutaka
 
Ni vema ukatueleza hiyo ndoa yenu ni ya dini gani, Mila, Bomani au.............?
 
Tafadhali atoto usipite hapa!

Back to topic: "..na hao wawili watakuwa mwili mmoja!" Mtazamo wangu ninyi bado hamjawa mwili mmoja aisee. Rekebisheni ndoa yenu kwanza kabla hamjafikiria jambo lolote lile la maendeleo.
 
Last edited by a moderator:
....mmmmmmmmmmmmmmmh


ndugu wewe ndio unamjua mumeo.....

wewe ndio umeona viashiria hatarishi kwa mumeo

fuata moyo wako unavyotaka....
 
Tafadhali atoto usipite hapa!

Back to topic: "..na hao wawili watakuwa mwili mmoja!" Mtazamo wangu ninyi bado hamjawa mwili mmoja aisee. Rekebisheni ndoa yenu kwanza kabla hamjafikiria jambo lolote lile la maendeleo.

Tafadhali fafanua zaidi mkuu ili kupata mawazo chanya

Ni vema ukatueleza hiyo ndoa yenu ni ya dini gani, Mila, Bomani au.............?
Kikristo

nyie wote wawili mnapotezeana muda hamna ndoa hapo ...fanya hivi hiyo hati ya nyumba andikeni majina ya watoto

even though mimi sio mtaalamu wa maswala ya "Mivurugano"

kilaza

Kwa nini unasema hakuna ndoa hapo mkuu? Kwa mawazo yako nini kirekebike ili kuokoa hiyo ndoa?
 
Kaa chini uwaze na kuwazua..! But ningependa kukuuliza jee "unampenda kweli mumeo" koz nadhani kama kuna mapenzi ya dhati baina yenu mambo yangekaa sawia tuu..! Uaminifu unajengwa kwa Mapenzi ya dhati baina yenu no matter how puritan he had been over the past..!
 
Badilisheni jina la kiwanja muweke watoto au komaa mtafute kiwanja kingine ndio mjenge nyumba ya pamoja yenye majina yenu wawili.
 
Tafadhali atoto usipite hapa!

Back to topic: "..na hao wawili watakuwa mwili mmoja!" Mtazamo wangu ninyi bado hamjawa mwili mmoja aisee. Rekebisheni ndoa yenu kwanza kabla hamjafikiria jambo lolote lile la maendeleo.

Hahahahaaaa! Mentor mie hata sijapita kwakweli, duuh kuna wanawake wana mioyo chuma kimesingiziwa.
 
Last edited by a moderator:
Wanaume tuwe na tabia ya kuzihudumia familia zetu. Yani una kipato lakini mke anatoa matumizi tangu 01.01...hadi 31.12....wewe unakula tu huoni aibu.? Kwa hili namuomba maulana anisaidie asee!
 
Mjenge kiwanja chake au chenu? Kwani ni yeye aliyesema mjenge kiwanja chake, au ni wewe umeamua kukiita chake? Yeye anakiitaje? chake au chenu?
 
Haaaaa kuskiliziana ata kwenye ndoa kupo??,,,loooh aya jamani wazoefu kazi kwenu wengine uzoef mwsho kibaha
 
Hahahahaaaa! Mentor mie hata sijapita kwakweli, duuh kuna wanawake wana mioyo chuma kimesingiziwa.

Mkuu atoto karibia nilie mwenzio... tafadhali usinicheke katika kipindi hiki kigumu kwangu, nina mawazo kibao. Kama una ushauri naomba mkuu
 
Last edited by a moderator:
kamwe usijenge kwenye hiko kiwanja utasaga meno,
abadilishe jina na mwanaume aliyezaa na mwanamke mwingine wana matatizo sana kuna leo na kesho,haelewi somo kuwa mjinga kaa kimya kwani viwanja sh ngapi bana?utanunua chako utawajengea wanao.
Watoto ni wake si wakwako so jiongeze
 
Back
Top Bottom