Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

Ukiwa na mume mwenye watoto uliowakuta utakuwa na amani sana ukiwajumlisha kwenye idadi ya watoto ulonao..
Otherwise ni mara kumi usikubali kuolewa na mwanaume mwenye watoto..
Kwani hamuwezi ku afford kuwa na watoto 4 au ni ligi kwa kuwa si wako?
 
Wanaume siku hizi ni wachache sana aisee....

Inakuwaje unakula tu bila hata kushtuka.....

Wakati wanaume wa enzi za Asprin akikuta umeleta gunia la mchele tu inabidi ujieleze....maana anjua majukumu yake


Wanaume tuwe na tabia ya kuzihudumia familia zetu. Yani una kipato lakini mke anatoa matumizi tangu 01.01...hadi 31.12....wewe unakula tu huoni aibu.? Kwa hili namuomba maulana anisaidie asee!

Hapo hata wakianza ujenzi kuna dalili huyu dada ndie atakayejenga....mwanaume atanyuti tuliiiiiiiiiiiiiiiii

Kuna haja ya kupeleka wanaume wa kizazi hiki jandoni...porini hukooooo wakafunzwe
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu kampelewele Sikuanza hivyo ila kuna viashiria nilivyoviona vikawa vinanipa cold feet. Hivi ni kwa nini mwanaume mwenye uwezo wa kutunza familia yake adanganye hana uwezo ili mkewe amtunzie wanawe wanne wakati yeye akila bata tu?

Baada ya hapo nategemewa nisiwe na wasiwasi wowote kwenye proposal ya ku invest pamoja? Kama ndo huo mguu nje unakuja kwenye mazingira haya mkuu.
Mwanamke ana uwezo mkubwa kumrejesha mwanaume katika mstari. Kumbuka kauli yako na supply ya K ni muhimu katika kumrejesha katika mstari. Kuna vitu huwa nyie mnajisahau kama kubase upande wa ndugu zenu. Kama hujali ndugu zake hilo nalo lirekebishe. Angalia wanyama kama kuku, kila wakati yakiwepo madume mawili hata kama majike ni mia yatapigana, hii ni nature ambayo mwanaume ni mbinafsi kwa mkewe. Ngoja nikupe maujanja kidogo, leo ukirudi nyumbani mwambie mume wako kuwa sawa mjenge hicho kiwanja kwa jina lake utaona atakavyofurahi. Nimekuuliza kama ni ndoa mseto yaani kabila x na kabila y, hukujibu ungelinijibu ningekupa akili. Kumbuka katika maisha yako sisi ni vilaza kwa akili ya mwanamke na mwanaume hutengenezwa na mwanamke asikuambie mtu. Cha mwisho wakati wa mahanjumati jaribu kuwa unatabasamu na kuwa karibu naye utaona atabadilika tu. Nakueleza tokana na experience
 
....mmmmmmmmmmmmmmmh


ndugu wewe ndio unamjua mumeo.....

wewe ndio umeona viashiria hatarishi kwa mumeo

fuata moyo wako unavyotaka....

inawezekana akifuata moyo wake atapotea lakini ushauri wako ungeweza kumsaidia.
 
And now yo talking



Mie sijakucheka wewe mpendwa, nilicheka mentor aliposema nisipite hapa, kwakweli sikushauri mjenge ktk kiwanja hicho, either kibadilishwe jina ama mnunue kipya, na hakikisha hakutegei tena katika ujenzi.
Ndoa hii ni kati ya familia ninazosema ni mchanganyiko maana kuna familia ya kwanza ni Baba na wanae wawili alowakuta huyu jamaa yetu; ya pili ni Baba na wanae wa huyu rafiki yetu; ya tatu ni mama na wanawe wawili (biological children) na ya mwisho ni ile ya WOTE sita. Katika hili jina la mtoto au jina la mama ni hatari bora la kiunganishi ambaye ni BABA. Hivi nyumba ni kitu gani mbona tunafiwa na wazazi tunasahau? Jamani hivi vitu vinavyopita visivuruge amani ya familia.
 
Mwanamke ana uwezo mkubwa kumrejesha mwanaume katika mstari. Kumbuka kauli yako na supply ya K ni muhimu katika kumrejesha katika mstari. Kuna vitu huwa nyie mnajisahau kama kubase upande wa ndugu zenu. Kama hujali ndugu zake hilo nalo lirekebishe. Angalia wanyama kama kuku, kila wakati yakiwepo madume mawili hata kama majike ni mia yatapigana, hii ni nature ambayo mwanaume ni mbinafsi kwa mkewe. Ngoja nikupe maujanja kidogo, leo ukirudi nyumbani mwambie mume wako kuwa sawa mjenge hicho kiwanja kwa jina lake utaona atakavyofurahi. Nimekuuliza kama ni ndoa mseto yaani kabila x na kabila y, hukujibu ungelinijibu ningekupa akili. Kumbuka katika maisha yako sisi ni vilaza kwa akili ya mwanamke na mwanaume hutengenezwa na mwanamke asikuambie mtu. Cha mwisho wakati wa mahanjumati jaribu kuwa unatabasamu na kuwa karibu naye utaona atabadilika tu. Nakueleza tokana na experience

hayo hapo ndo mambo nisiyoyataka....we mwanaume kama hajali mke na watoto inamaana hata mama yako mzazi hawezi mpelekea upande wa kanga...leo ukawajali ndugu zake kwa lipi???? unajua siku zote mapenzi, heshima goes both ways...hata siku moja usitarajie kufanyiwa kinyume na unachofanya...huyo mwanaume ni mchoyo..ana roho mbaya na mbinafsi.. anaona bora pesa ya mwanamke itumike na iishe lkn yake ijazane benki...basi na kwenye nyumba atakuja kufanya hvyo hvyo...!!!!
 
hayo hapo ndo mambo nisiyoyataka....we mwanaume kama hajali mke na watoto inamaana hata mama yako mzazi hawezi mpelekea upande wa kanga...leo ukawajali ndugu zake kwa lipi???? unajua siku zote mapenzi, heshima goes both ways...hata siku moja usitarajie kufanyiwa kinyume na unachofanya...huyo mwanaume ni mchoyo..ana roho mbaya na mbinafsi.. anaona bora pesa ya mwanamke itumike na iishe lkn yake ijazane benki...basi na kwenye nyumba atakuja kufanya hvyo hvyo...!!!!
Tatizo la kutopenda kushuka halijengi ndoa kama umeolewa. Kisasi ni sumu ya ndoa. Asipojali upande wa kwako mfundishe kwa kujali upande wa kwake. Jino kwa Jino si ndoa ndugu yangu lazima mmoja ashuke
 
Mnapoanza kuwaza tofauti kimajukumu shida inaanza.
 

Attachments

  • 1431610895456.jpg
    1431610895456.jpg
    61.5 KB · Views: 157
Tatizo la kutopenda kushuka halijengi ndoa kama umeolewa. Kisasi ni sumu ya ndoa. Asipojali upande wa kwako mfundishe kwa kujali upande wa kwake. Jino kwa Jino si ndoa ndugu yangu lazima mmoja ashuke[/QUO

labda kama moyo wake wa nyama wangu ni wachuma...lkn kama yote sawa then hili litakua ngumu...!!!!
 
Mapenzi ya siku hizi bwana yamekaa "kimachale machele" ukifumba tu macho umeibiwa...
back to topic, tengeneza mazingira , mshauri mumeo mnunue kiwanja kisha muandike jina la mtoto wenu kisha mjenge pamoja.
hicho chake mwambie atajenga tu mkimaliza hiyo nyumba ya familia.
 
Stuka!! abadili Title Deed iwe na majina yenu wote vinginevyo senti zako zicheze mbali na gharama za ujenzi wa hiyo nyumba.
 
1. kosa la kwanza ni 'kuoana' badala ya wewe kuolewa na yeye kukuoa,
2. Pili, kama anataka mjenge nyumba ya familia basi ni vyema hiyo hati ya kiwanja iwe na 'joint ownership' yaani mkabadilishe ili rohoni mwenu na nje kwa watu wote na objectively ijulikane ni mali yenu. Kama akikataa, basi mpango huo inabidi uwe hadithi kwani huyo jamaa na hayo majibu yake hamtafika mbali.
 
Ndo maana mnashauriwa muoane ambao mila na desturi zenu zinaendana. Yapo makabila mengi tu ambayo ni jukumu la mke "kuleta pesa". Najua wanaume wengi ambao hawajui chochote kuhusu kula.kuvaa.kusoma kwa watoto nk. Vyote kamuachia mke. Imefikia wakati wake wanalazimika kuwekeza kwa siri na kufanya biashara kwa siri na watu wengine.
 
kamwe usijenge kwenye hiko kiwanja utasaga meno,
abadilishe jina na mwanaume aliyezaa na mwanamke mwingine wana matatizo sana kuna leo na kesho,haelewi somo kuwa mjinga kaa kimya kwani viwanja sh ngapi bana?utanunua chako utawajengea wanao.
Watoto ni wake si wakwako so jiongeze
Mambo ya ndoa raha sana, hasa mwanamke akiachiwa kucontrol familia (kwa kiburi chake) huwa ameonewa na kuhisi kunyanyaswa. Nadhani ushauri wako hakuzingatia maelezo ya upande wa pili ingawa unaweza kuwa sahihi hata kama huna au sina uhakika.

kuna maswali mengi sana ya kujibiwa kabla ya kuanza kushauri kwenye swala hili, je kabla ya kuamua kuishi pamoja taarifa hizi za watoto wa nje ya mahusiano yao zilikuwepo? inahusu alizipokeaje?

Nini makubaliano ya awali kati yao? Isije kuwa inahusu alichangia kuvunja nyumba ya mwanamke mwenzie na sasa uhalisia wake unajidhihirisha kwamba hakuwa na utayari wa kuishi na hao watoto wa mumewe. Nahisi pia kuna uwezekano wa inahusu kumzidi kipato mumewe! na ni ile type ya wadada wanaojifanya kutojali kupanga maswala ya familia na mumewe hasa yanayo husu kipato na matumizi.

Ni rahisi mwanaume kugaili pale anapohisi mkewe anataka kuwa incharge wa kila kitu, anaweza kudhani alibana matumizi na mlenda ugali umemuadabisha mume kumbe nae mume alikuwa anasubili mkewe akwame ili mchango wake uthaminiwe?. Wanawake wana sura nyingi sana za kibaguzi hasa wanapokuwa kwenye ndoa zenye watoto wa mwanamke mwingine kabla yao.

Hivi amu unajua kwamba wanaume huwa ni nadra sana kuwabagua watoto wa wanaume wenzao? labda kama mke atajaribu kutumia nguvu nyingi au upendeleo wa wazi kwa wanae. Nimeona mengi wacha ninywe bia tu weita ongeza moja baridi huku.
 
Habari zenu,

Ni hivi nimeolewa, mume wangu ana watoto 2 kabla ya ndoa yetu nasi tuna watoto wawili. Wote ni

Najiuliza sasa tena tujenge wote kwenye kiwanja chake? Pia mwenzangu ana watoto 4 mie nina
wawili
hapo kuna vitu umechanganya paragraph ya kwanza na ya mwiso mstari wa kwanza each.
 
1. kosa la kwanza ni 'kuoana' badala ya wewe kuolewa na yeye kukuoa,
2. Pili, kama anataka mjenge nyumba ya familia basi ni vyema hiyo hati ya kiwanja iwe na 'joint ownership' yaani mkabadilishe ili rohoni mwenu na nje kwa watu wote na objectively ijulikane ni mali yenu. Kama akikataa, basi mpango huo inabidi uwe hadithi kwani huyo jamaa na hayo majibu yake hamtafika mbali.
mmh hujui tu namna ngoma inavyo wambwa....ukishiriki siku moja utaelewa cha kuongea kwenye ngozi hii.
 
Back
Top Bottom