Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

Naomba ushauri: Mume wangu ananiachia majukumu

Ndoa za siku hizi ni material based kuliko mapenzi...mtu unampenda unashindwa kumhudumia....mtu unampenda huwezi kujenga nae nyumba, kisa kimeandikwa jina lake!

Hapo kweli hamna ndoa bali ni mmeungana kwa ajili ya kupumzishana tu, Ila kila mmoja wenu anasafiri!???
 
Hapo tatizo lenu kubwa siyo kujenga wala jina la mtu kwenye kiwanja. naona wengi wanashauri kubadilisha majina ya kiwanja, thats not a good enough solution. hata mkiandika kiwanja ni paka au mbwa wenu huku ndani hamuaminiani bado hamtajenga.
hofu kubwa ninayoiona kwako siyo kujenga wala kiwanja kuwa cha mme wako, hofu kubwa kwako ni mume wako kuonekana siyo mwaminifu, au wewe kutomuamini mumeo, ndo maana all the time unaona unaibiwa.
ushauri wangu,
1. inawezekana unakimbia kivuli chako mwenyewe, rudi utafakari mlivyokutana na kuoana, inawezekana hayo mazingira ndo yanakusumbua.
2. inawezekana uko kwenye ndoa lakini una plan B ya maisha, sasa kila kukicha plan B inakuwa very stron in you such that it controls even your emotions

anyway, mwanamke mpumbavu hubomoa nyumba kwa mikono yake mwenyewe
 
Masuala ya ndoa yanategemea mila na desturi au tuseme uzoefu tunaokuwa nao kabla ya kuingia katika hili dude liliotamu kupita kiasi na lenye uchungu uliopitiliza yaani NDOA. Aidha anayejua ndoa ni yule ambaye ameonja tamu na shubiri ya ndoa. Aliye na uzoefu wa tamu bila shubiri ya ndoa hawezi kutoa ushauri wa maana katika masuala ya ndoa: vile vile mwenye uzoefu wa ndoa ya shubiri tu bila tamu hawezi. Mshauri mzuri ni yule aliyeonja pande zote mbili za ndoa. Wengi wetu ni nadharia tu.

Kwa wanandoa wapya wanategemea wazazi wao walikuwa na maisha yepi. Je ni ndoa ya mguu mmoja ndani kwa mume na mwingine kwao au miguu yote kwa mume. Kama uzoefu wa wachumba ni huo hata siku moja kuaminiana hakutakuwepo nao watakufa maskini hata bila ya kibanda cha mbavu za mbwa. Mleta mada anaonyesha kama ni mguu mmoja ndani na mwingine nje == sababu ya kukosa imani na kufikiri ipo siku kila mtu atachukua chake. Ndoa ni RISK na kuamini kuwa hakuna kutengana.
 
bhikola
Napata point yako mkuu, but hukuweka possibility that the man might indeed be kwenye route ya kutaka kunitumia na sio fears za "mwanamke mpumbavu" tu! Kwani hatujayaona haya kwenye jamii yanatokea? Asante kwa ushauri wako
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu kampelewele Sikuanza hivyo ila kuna viashiria nilivyoviona vikawa vinanipa cold feet. Hivi ni kwa nini mwanaume mwenye uwezo wa kutunza familia yake adanganye hana uwezo ili mkewe amtunzie wanawe wanne wakati yeye akila bata tu?

Baada ya hapo nategemewa nisiwe na wasiwasi wowote kwenye proposal ya ku invest pamoja? Kama ndo huo mguu nje unakuja kwenye mazingira haya mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mjenge kiwanja chake au chenu? Kwani ni yeye aliyesema mjenge kiwanja chake, au ni wewe umeamua kukiita chake? Yeye anakiitaje? chake au chenu?
anakiita "chetu" but ni "chake" legally! La sivyo mbona hataki kukiweka "chetu" kimaandishi?
 
kamwe usijenge kwenye hiko kiwanja utasaga meno,
abadilishe jina na mwanaume aliyezaa na mwanamke mwingine wana matatizo sana kuna leo na kesho,haelewi somo kuwa mjinga kaa kimya kwani viwanja sh ngapi bana?utanunua chako utawajengea wanao.
Watoto ni wake si wakwako so jiongeze

Haya mambo wanaume ndio wanasababisha kwa kiasi kikubwa, mwanamke anaweza kuumia kwa mgongo wa kujenga ndoa na kuitwa wife material kumbe mbwembwe tu.

I had a friend ameolewa yeye na mumewe ni waajiriwa serikalini ila mke anamzidi Mme kipato, wakaanza kujenga, make anatoil kweli pesa yake yote inaishia hapo. wakativmwingine anamkabidhi mmewe cash kwamba anaenda site kumbe Mme anaishia kwa vimada.
mwishowe Mme ameoa make mwingine na alisha mwonesha the same site lkn nyumba bado haujakamilika binti wa watu ni kulia kila siku...
inaudhi aisee.
Dada akili kichwani mwako, dalili njema na mbovu unaziona mwenyeewe sisi wengine ni washauri tu n a we are not part of the story.
 
hizi ndoa hizi...........mbali na huo ubinafsi wenu, hamjitambui mko wapi na mnaelekea wapi..... hicho kiwanja alinunua wakati gani?kabla au baada ya hiyo ndoano.......kama ni kabla sawa kabisa ni chake..... ila kama ni baada ya ndoano,,,, ni cha familia,,,..... ongeza watoto ili na wewe uwe na 4,,,,...
 
Asante mkuu. Sikuanza hivyo ila kuna viashiria nilivyoviona vikawa vinanipa cold feet. Hivi ni kwa nini mwanaume mwenye uwezo wa kutunza familia yake adanganye hana uwezo ili mkewe amtunzie wanawe wanne wakati yeye akila bata tu? Baada ya hapo nategemewa nisiwe na wasiwasi wowote kwenye proposal ya ku invest pamoja? Kama ndo huo mguu nje unakuja kwenye mazingira haya mkuu
Hili la mguu mmoja ndani na mwingine nje ni kwa wote. Si ajabu na yeye anadhani ipo siku mtaachana hivyo kama akina Mentor walivyosema ni bora mkajenga uhusiano wa kwenu kwanza. Sijui ni salama au si salama kujianika hapa, ingalikuwa ni salama ungenieleza unatoka pande ipi ya TZ na kama ndoa yenu ni ya mseto maana haya masuala ni mazito.
 
Wanaume tuwe na tabia ya kuzihudumia familia zetu. Yani una kipato lakini mke anatoa matumizi tangu 01.01...hadi 31.12....wewe unakula tu huoni aibu.? Kwa hili namuomba maulana anisaidie asee!

And now yo talking

Mkuu atoto karibia nilie mwenzio... tafadhali usinicheke katika kipindi hiki kigumu kwangu, nina mawazo kibao. Kama una ushauri naomba mkuu

Mie sijakucheka wewe mpendwa, nilicheka mentor aliposema nisipite hapa, kwakweli sikushauri mjenge ktk kiwanja hicho, either kibadilishwe jina ama mnunue kipya, na hakikisha hakutegei tena katika ujenzi.
 
anakiita "chetu" but ni "chake" legally! La sivyo mbona hataki kukiweka "chetu" kimaandishi?

Jengeni na usiweke moyoni kwamba iko siku mtatengana. Kuhusu watoto, wote wanne watakuwa na percentage kwenye urithi. kuna watakaorithi kwa baba pekee na kuna watakaorithi kwa baba na mama ambao ni wanao.
 
Kila kinachonunuliwa ndani yandoa ni chenu nyote, haijalish nan kanunua ni chawote, ukisema tujenge kiwanja chake unamaanisha unapanga kuachana nae? amini mtakuwa pamoja milele, jengeni kwamanufaa ya familia yenu, au unahofia watoto 2 wamume?

Hata babayao angekufa leo mmiliki halali niwewe maana ndo mke wake, hatakama msingekuwa nandoa kuishi pamoja kwa miaka 2 nindoa halali nakila rasilimali niyawote, hata kama mama ungekuwa wanyumbani tu hujaajiriwa una haki 100% kumiliki kila kitu, nahata mkitaka kuachana mtagawana nusu kwanusu.

Jenga tu dada yangu, pia mwombee mume wako.
 
Jaribu kufafanua vizuri maelezo yako ili usaidiwe je? Hiyo ndoa ya kanisani au kiislam napia kabla ya kuingia kwenye ndoa alikuwa mtoaji? Au ulikuwa unamuhonga why nauliza hivyo! Sababu wadada wengi siku hizi wako tayari kuhonga wanaume ili waolewe! Mwisho kabisa vipi huyo mama alozaa nae ameshaolewa? Au bado wanaendelea na mahusiano?
 
asante mdau iryn Nadhani kwa aliyewahi kukumbwa na tatizo hili anajua ugumu wa suala lenyewe hata kulizungumzia tu kwa kuwa masuala ya properties kwenye ndoa ni sensitive.

Lakini naamini hii haimaanishi mwanamke atoe tuuuu hatakama anaumia ili ajenge ndoa! Leo nasikiliza zaidi maana kuna wenye uzoefu zaidi yangu labda wanaweza kunipanua mawazo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom