Naomba ushauri: Mke wangu alinificha kwamba ameathirika

Naomba ushauri: Mke wangu alinificha kwamba ameathirika

Kuna jamaa ni Mtoto wa mchungaji akapenda binti kanisani kumbe yule binti ni +
Binti kumbe alikuwa anamoenda Sana mshikaji akauchuna wameoana fresh baadae mimba ikatoka ,tena akajifungua Mtoto mfu jamaa kufwatilia kwa Dctor tatizo Doctor naya akijua jamaa anajua akawa anampa ushauri .

Wee kiliwaka vikao vikaanza jamaa anataka amwache ,kwenda kupima naye tayari +
Wakamtuliza binti akasema historia yake kumbe alizaliwa navyo na alikuwa anampenda Sana jamaa .
Hivi wanaishi pamoja ila jamaa demu yoyote asijichanganye anaye
Anaudhuriaga kwenye sehemu na kumbi za starehe au Mabaa na hoteli anaanza muudumu mmoja baada ya mmoja mpaka watakapo stuka .
Anatumia vinyaji Baridi pombe hagusi ni mkimya Sana na pesa ipo hivyo wananasa kweli na anaafya nzuri tuu.
Yaani ni hatari na nusu .
 
Hiyo ni kadi nyekundu moja kwa moja. Uaminifu ni pamoja na kutoa taarifa sahihi kwa mwenza wako mapema , kusubiri hadi mmepata mtoto ndio akwambie ukweli sio sawa.

Otherwise ni maamuzi yako binafs
 
Kwahiyo na wewe umetuficha majibu? Anyway ugonjwa ni siri ya mgonjwa.
Yani utoke hospital umwambie huumwi chochote yeye akufungukie tu kiwepesi wepesi wakati amekuficha siri hiyo kwa mwaka mzima?
 
Duu pole sana. Huyo ni muuaji. Achana naye kistaarabu na muangalie namna nzuri ya kumlea mtoto na upate uhakika wa afya yake pia.
 
Nimeishi na muathilika ambaye ni mwenza wangu ambaye naweza kusema ni mke wangu sababu nimeishi naye zaidi ya mwaka mmoja lakini kwa muda huo wote alikuwa akinificha kuwa yeye ni muathilika alikuwa akinywa dawa kimya kimya bila mimi kujua na kutokana na nature ya kazi yangu ya kusafiri safiri ilikuwa ni kazi kugundua lakini kuna siku moja nilikuta kuna ARVS kwenye mkoba wake nilipomuuliza aliniambia ni vya mdogo wake ambaye alikwisha niambia zamani kuwa mdogo wake huyo ni muathilika na mdogo wake ni mapepe sana kwa hiyo huwa anakwenda kumchukulia dawa panapobidi hapo niliamini itakuwa kweli lakini wanasema hakuna siri ya milele

Sasa leo nimejisikia homa na dizziness asubuhi nikaisi labda uchovu tu but hadi mchana naona bado hali ile ile ikabidi niende hospital kucheki hali nilipoenda kupima nikaambiwa sina ugonjwa wowote wakanipa dawa ya kutuliza maumivu niliporudi home nikamwambia hali halisi ya hospital yaani nimepimwa nimeambiwa sina ugonjwa wakati mimi bado najisikia homa ndio ikabidi aniambie kwamba yeye ni muathilika wa ukimwi since akiwa mdogo hadi leo ana miaka 24 anatumia dawa

Kwa kweli baada ya kuniambia hivyo nilijihisi kuchanganyikiwa nikarudi tena kupima HIV lakini majibu ya hospital nikaambia mimi niko negative yaani sina maambukizi na ukizingatia tayali tuna mtoto mdogo ana mwezi mmoja hapa namfikiria sana mwanangu bado mdogo na hii situation iliyopo nashindwa nifanye maamuzi magumu sababu huyu mwenzangu alidhamilia kabisa kuniambukiza but Mungu amenilinda.
Hapa ntaka kila mtu ashike njia yake je nitakuwa nimekosea kwa hili???
Heri nusu Shari kuliko Shari kamili


Bora umuache, mtoto peleka huduma tu

NB: Kwa kesi kama hiyo hukutakiwa kuja kuuliza bali ulitakiwa kuja kutoa mrejesho ushamtimua
 
Kuna jamaa ni Mtoto wa mchungaji akapenda binti kanisani kumbe yule binti ni +
Binti kumbe alikuwa anamoenda Sana mshikaji akauchuna wameoana fresh baadae mimba ikatoka ,tena akajifungua Mtoto mfu jamaa kufwatilia kwa Dctor tatizo Doctor naya akijua jamaa anajua akawa anampa ushauri .

Wee kiliwaka vikao vikaanza jamaa anataka amwache ,kwenda kupima naye tayari +
Wakamtuliza binti akasema historia yake kumbe alizaliwa navyo na alikuwa anampenda Sana jamaa .
Hivi wanaishi pamoja ila jamaa demu yoyote asijichanganye anaye
Anaudhuriaga kwenye sehemu na kumbi za starehe au Mabaa na hoteli anaanza muudumu mmoja baada ya mmoja mpaka watakapo stuka .
Anatumia vinyaji Baridi pombe hagusi ni mkimya Sana na pesa ipo hivyo wananasa kweli na anaafya nzuri tuu.
Yaani ni hatari na nusu .
Duuh hatari sana
 
Hiyo ni kadi nyekundu moja kwa moja. Uaminifu ni pamoja na kutoa taarifa sahihi kwa mwenza wako mapema , kusubiri hadi mmepata mtoto ndio akwambie ukweli sio sawa.

Otherwise ni maamuzi yako binafs
Asante sana kwa ushauri
 
Duu pole sana. Huyo ni muuaji. Achana naye kistaarabu na muangalie namna nzuri ya kumlea mtoto na upate uhakika wa afya yake pia.
Asante sana na ushauri wako ni mzuri
 
Kwahiyo na wewe umetuficha majibu? Anyway ugonjwa ni siri ya mgonjwa.
Yani utoke hospital umwambie huumwi chochote yeye akufungukie tu kiwepesi wepesi wakati amekuficha siri hiyo kwa mwaka mzima?
Mbona majibu nimesha sema nimepima nimekutwa -ve but nimepewa PEP nitumie kwa muda wa siku 28 then nirud tena kuchek baada ya siku 28
 
Na leo alipoona ninaumwa but majibu ya hospital nikaambiwa sina ugonjwa ndio akajua tayali ameshaniambukiza ndio maana akafunguka.
Asante sana kwa ushauri wako
Piga chini mapema sana huyo muuaji, maisha bado ni marefu sana hivyo bado una nafasi ya kuanza upya, vinginevyo subiria afanikishe alichokuwa anataka , tiyari Mungu ameshakuonesha hivyo kazi imebaki kwako sasa
 
Kuna haja ya watu kuzingatia kupima kabla yakuwekana ndani, magonjwa ni mengi na ni ngumu sana mtu kuiweka wazi hali yake ya kiafya kwa kuhofia kupoteza.

Pole sana mkuu.
Na kuna uwezekano kama wangepima kabla ya ndoa mwanamke asingekutwa nao sababu yupo kwenye dose labda wangepima kwa kipimo kikubwa ila hiv vya rapid huoni ngo
 
Na kuna uwezekano kama wangepima kabla ya ndoa mwanamke asingekutwa nao sababu yupo kwenye dose labda wangepima kwa kipimo kikubwa ila hiv vya rapid huoni ngo
Kuna kama huyo anaejijua hali yake na akaamua kutokuiweka wazi kwa mwenza wake ila kuna wale wasiojijua kama ni waathirika, kupima ni muhimu.
 
Rudia Kipimo hospital kubwa waambie wakupime Kipimo cha ELISA. Hiki ni kiboko. Kikisema negative basi ni negative. Halafu mpime na mtoto. Ukikuta wewe ni mzima kimbia kama kiboko Dume achana na huyo mwanamke. Mtoto akiwa mzima kimbia naye halafu uende dawati la jinsia na watoto police ukaeleze Shida zako na uombe uruhusiwe ukabidhiwe na mtoto wako kabisa. Watakupekeka ustawi wa jamii na utapewa. mtoto wako official kabisa. Huyo mwanamke muuaji wa kudhamiria.
Funzo kwa wote: Kupima HIV ni Bure kwa hospitali au vituo vyote kwa Kipimo hiki cha kawaida. Ukiwa na mpenzi wa kudumu pima kutumia ELISA test. HIV IPO kwa wingi tu na inafichwa na ARV.
 
Na kuna uwezekano kama wangepima kabla ya ndoa mwanamke asingekutwa nao sababu yupo kwenye dose labda wangepima kwa kipimo kikubwa ila hiv vya rapid huoni ngo
Ni kweli kipindi naanza naye mahusiano alipima akaonekana hana tena VVU naona ukitumia dawa muda mrefu huwa inaonekana kama huna ila ukiacha kidogo tu vinakuja kwa kasi ya 5G
 
Rudia Kipimo hospital kubwa waambie wakupime Kipimo cha ELISA. Hiki ni kiboko. Kikisema negative basi ni negative. Halafu mpime na mtoto. Ukikuta wewe ni mzima kimbia kama kiboko Dume achana na huyo mwanamke. Mtoto akiwa mzima kimbia naye halafu uende dawati la jinsia na watoto police ukaeleze Shida zako na uombe uruhusiwe ukabidhiwe na mtoto wako kabisa. Watakupekeka ustawi wa jamii na utapewa. mtoto wako official kabisa. Huyo mwanamke muuaji wa kudhamiria.
Funzo kwa wote: Kupima HIV ni Bure kwa hospitali au vituo vyote kwa Kipimo hiki cha kawaida. Ukiwa na mpenzi wa kudumu pima kutumia ELISA test. HIV IPO kwa wingi tu na inafichwa na ARV.
Nafikiri hicho kipimo ndio nilipima hospital ya kwanza maana sikijui
Si wanachukuwa damu wanaweka kama kwenye kichupa hivi then wanapeleka maabara??
Je ndio hicho??
 
Back
Top Bottom