Naomba ushauri kuhusu dini

Naomba ushauri kuhusu dini

Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaid ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mktisto mama yangu ndiyo muislam, bahat mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielew kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasabu dini ya kiislam naijua nimesama madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zaman nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.

Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipend kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumban na natumia maji ya baraka wakat mwingi nahis kabisa yananisaidia, halaf nikiwa kanisani nina aman zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubir ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumban redio nasikiliza redio maria tu na naifurahia.

Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sahiv ndiyo nazid kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu nataman waanze mafundisho, au kuna sehem sijielewi?
Ukifuatilia historia yako...
Umezaliwa kwenye Familia ya Kiislam na kupata ile basic knowledge ya kusoma ( kama Nursery) ambapo kule ni mambo basic na pale ambapo ungetakiwa Usome Quran na kuelewa kilicho andikwa na kilichokusudiwa namaanishwa kuanzia umri wa miaka 13 hivi (ukiwa matured) ukawa umeenda kwenye Shule ya Kikatoliki
Ulipo kwenda sekondary ya wakatoliki, hapo ndio uliweza kupata Mafundisho ya Dini (Kikatoliki) ambapo ukawa ndio mwanzo wako wa kupata mafundisho ya Dini kwa undani na kuelewa kwani pale umekua (matured). Nimeandika hivyo ili ujue kuwa, hakuna kitu cha ajabu sana hapo.
Kwa mtu mwenye hekima nilitegemea uulize kuwa; nimepata mafundisho ya kikatoliki shuleni na natamani Kusoma Elimu ya Kiislam tofauti na ile ya Chekechea ya Kufundishwa/ku kremu kusoma na kuandika; namaanisha mwanafunzi wa Chekechea hawezi kujisifia eti na yeye ameelimika kisa tu amejua kusoma na kuandika
Kwa kufanya hivyo ungeweza kusoma indetail sio ile ya kukremu hata mimi nilisoma hiyo pia ila baadae nikajiona nilipata pengine kama 6% ya nilichotakiwa kujua; baada ya hapo ungeweza kufanya uamuzi sahihi
KWA ELIMU YAKO YA UISLAM LEVO YA CHEKECHEA USIJIWEKE KWENYE KUNDI LA WATU WANAOJUA UISLAM; SOMA!
 
Ukifuatilia historia yako...
Umezaliwa kwenye Familia ya Kiislam kwa jina ila hukupata msingi wowote wa dini ya Kiislam zaidi ya kupewa jina la kiIslam.
Ulipo kwenda sekondary ya wakatoliki, hapo ndio uliweza kupata Mafundisho ya Dini (Kikatoliki) ambapo ukawa ndio mwanzo wako wa kupata mafundisho ya Dini. Kwa kuwa hukuwa na Elimu yoyote ya dini uliyozaliwa nayo kwa vyovyote vile uta amini kile unachofundishwa (katoliki) kuwa ndio dini bora kuliko zote
Nimeandika hivyo ili ujue kuwa, hakuna chochote cha ajabu hapo na sijui kwa nini unashindwa kuelewa such a simple logic.

Kwa mtu mwenye hekima, nilitegemea uulize kuwa nimepata mafundisho ya kikatoliki shuleni na wazazi wangu hawakutimiza wajibu wao wa kunipatia foundation ya Kiislam; ni wapi naweza kupata mafundisho ya Kiislam ili niweze kufanya uamuzi sahihi ya Dini ipi niifuate.
Ila kiujumla unaonekana kuwa na unaudhaifu katika kufanya maamuzi sahihi na inawezekana sio kwenye dini pekee!
Sio kweli. Ye kasema kasoma madrasa na vitabu vyote kasoma maana yake misingi ya kiislam anayo. Apo naona alikiwa ajapewa jini la kumfanya kuwa mwislamu
 
Hahahahaha! Unaleta katuni??? Haya poke ushauri nakupa mimi. Nenda kawe kafiri wla hamna shida!
 
Yaani sisi binadamu ni watu wa ovyo,hivi wewe unayeona dini yako ndo iko sahihi kuliko ya mwenzako unakuwa na maana gani?unajihesabiaje haki wewe? mi nachojua Ibrahim ndo baba wa imani kwa wakristo,waislam na Juda
"Judaism,Christianity and Islam can all be tied to the same individual simply because Ibraham is the common parent to all three"
Utofauti unaletwa na ubinafsi wa watu na kujifanya wafia dini
Ushauri wangu we nenda pale moyo wako unakutuma
 
Sio kweli. Ye kasema kasoma madrasa na vitabu vyote kasoma maana yake misingi ya kiislam anayo. Apo naona alikiwa ajapewa jini la kumfanya kuwa mwislamu
Hivyo vitabu vyote ukimwambia sasa hivi akutajie vitano tu itabidi akavi-Google akuletee. Muongo huyo hajasoma uislam
 
Wewe siyo MUISLAMU.
Hata mimi nimeliona hili, angalia comment zake kwa wasio kua waislam anazipokea vyema ila ushauri unaotoka kwa waislam anautolea maneno yasiyofaa.
Ikiwa amesema kua anaujua uislamu vyema ili swala angepeleka kwa wenye elimu zaidi viongozi wake wa kiimani, au angeswali hata rakaa mbili kumwomba Allah amuonesha njia iliyo sahihi. Mtume muhamad s.a.w alituusia kuiiomba dua hii yaa muqalib, ....... Ewe mwenyezi Mungu zithibitishe nyoyo zetu ktk dini yetu ya haki. Mbali zaidi aya za mwenyezi Mungu zinatuonesha pia kumuomba Allah asiziache nafsi zetu kupotea baada ya kuamini.
Inaumiza kuona muislam tena uliezaliwa ukisema maneno hayo.
Nakushauri katafute elimu zaidi.
Hakika dini ya Allah ni uislamu na kamwe sitojutia kuwa muislam. Allah aniongoze mimi na wewe ktk haqqi mpka mwisho wetu na siku ya kiyama atujalie tuwe miongoni mwa wale watakao pokea kitabu chake kwa mkono wa kulia. Amiin
 
Mkuu!Mimi naamini katika UZIMA WA MILELE kama alivyo ueleza Yesu mwenyewe:-

Yohana 17:3

Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
Inatosha, upo vizuri labda tu tuongeze kitu hapa ili kuelewana:

Ukisikia Mkristu anasema Yesu ni Mungu usidhani amemuondoa Mungu kwamba hayupo. Huku kuna fundisho la utatu, lakini huo utatu ni 'mmoja'. Akili yako ikiweza kuyachukulia haya ndio utaelewa kuwa wakristu pia tunamtambua Mungu mmoja na hakuna Mungu mwingine isipokuwa yeye.

Mfano familia fulani inamiliki gari moja.
Sentesi A. Tunalo gari jeusi, zuri linalotumia petroli na linakimbia kwa kasi sana.
Sentensi B. Tuna gari linalokimbia

Tunaruhusiwa kusema sentensi B na sentensi A ni moja. Tunaruhusiwa pia kusema sentensi B ni mwana wa sentensi A na wakati tulisha sema ni moja na hatujachanganyikiwa! Kosoa hii logic kwanza kama iko na makosa. Kama haifai niambie nitumie miduara[cocentric circles labda tutaelewana
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Mzungumzaji mbona tayari ulishabadili dini kitambo unatafuta ushauri gani kaka wa mie???

Kulingana na islamic theology, Kitendo tu cha wewe kwenda kuombea, kuwapeleka wanao Kanisani na kuitakidi kwako unajisikia amani kanisani kuliko kwingine WEWE TAYARI NI MKIRISTO.....


Wataka wajumvi ILA KWA KADRI NINAVYOJUA IMANI ya KIISLAM WEWE TAYARI ULISHATOKA KITAMBO NA WALA SIYO MUISLAM
 
Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaid ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mktisto mama yangu ndiyo muislam, bahat mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielew kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasabu dini ya kiislam naijua nimesama madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zaman nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.

Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipend kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumban na natumia maji ya baraka wakat mwingi nahis kabisa yananisaidia, halaf nikiwa kanisani nina aman zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubir ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumban redio nasikiliza redio maria tu na naifurahia.

Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sahiv ndiyo nazid kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu nataman waanze mafundisho, au kuna sehem sijielewi?
Rafiki upo SEHEMU sahihi,ukristo haitoshi tu Bali taka kuwa ndani ya yesu kristo mwenyewe,aingie ndani yako atawale maisha yako.

Kinacho weza kukuokowa na hukumu ya Mungu ya milele kwenye ziwa la moto ni yesu kristo pekee ,si zehebu au mapokeo.

Historian Iko hivi

Ukristo=umepitia Kwa uzao wa Sara, mke mkubwa

Uislam= ni Kwa yule mjakazi bimdogo

Ko Mungu alimuahidi Ibrahim agano lake ni Kwa uzao wa bimkubwa, mpaka akazaliwa yesu.
Ahadi ya Mungu ikatimia.

Ko hapo ni sawa na kusema umetoka ule upande wa bimdogo ukaja upande wa bimkubwa .
 
Mkuu dini sio kabila kwamba huwezi kubadili. Kingine hizi dini tumeletewa na zote zinamuabudu Mungu mmoja. Sali dini ambayo inakupa amani ya moyo. Maisha mafupi na magumu sana kuanza kuumiza kichwa uwe dini gani wakati tayari umeshaoneshwa dini sahihi ya kuifata.

Kuhusu watoto ningependa kufahamu baba yao (mumeo) ni dini gani?
Hazimuabudu Mungu mmoja. Mungu wetu waislam hajazaa na wala hana mtoto
 
Watoto wasiokuwa na msimamo wa dini yoyote ndilo jambo zuri, wachague wenyewe wanayotaka kwenda wakiwa watu wazima wenye akili zilizokomaa.
Familia yeyote, ikisikia Baba dini hii Mama dini hii, tegemea kupata watoto wasio kuwa na msimamo na dini yeyote.

Maana tangu kuzaliwa kwao kutoka kwa wazazi wasioujua Msikiti wala Kanisa, hawana mafundisho yanahusu dini.

Hivyo alieleta mada hii hapa ni zao la ndoa ya kwa mkuu wa Wilaya. Tena afadhari huyu anaetafuta dini akiwa mtu mzima na Watoto wake, naamini hajui kitabu chochote siyo Bibilia wala Qurani.
Mwenye kujua chochote hawezi kuja kuuliza wapi pa kwenda hapa JF.
 
Bado sijafanya maamuzi japo nasukumwa sana na moyo wangu ila sielewi nifanye nini? Nibak ambapo nimezaliwa au niende moyo wangu unapopataka? Itakuaje??
Yesu ndiye njia ya kufika mbinguni mkuu, niamini nikuambiacho. Fanya maamuzi ya kumfuata Bwana Yesu, hutojuta. Utapata uhakika wa maisha haya na yale yajayo!


YESU NI BWANA NA MWOKOZI
 
Ni ipi ilikuwa ‘Aqidah na Manhaj yako huko zamani?

mmmh!

mmh!

Nina maswali mengi. Ila ngoja nikae kimya.

cc Kisai Kazakh destroyer naombeni muweke neno hapa.

رَبَّنَا لَا تُزِغْ قُلُوبَنَا بَعْدَ إِذْهَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً ۚ إِنَّكَ أَنتَ ٱلْوَهَّابُ

“Our Lord, let not our hearts deviate after You have guided us and grant us from Yourself mercy. Indeed, You are the Bestower.” (Qur’an 3:8)


Ewe Mwenye kuzigeuza Nyoyo, uthibitishe Moyo wangu katika Dini yako.
Anasema kuruan hahahahahahaha na kusali?? Hahahahahahaah huyu mtu bhana
 
Tuache upumbavu
Wewe ulishawahi kupewa nafasi na wazazi wako uchague dini au ulikuta wazazi ni waislam nawe ukawa huko? Tuache huo ujinga wa kudhani dini fulani ina haki sana mbele za Mungu. Mungu angelitaka angefuta na kubakiza dini 1 ulimwenguni. Mimi mwenyewe nimezaliwa familia ya kiislam, na nina ndugu zangu ni maulamaa ukienda kwetu Bukoba, lakini siongei maneno makali kwa watu wa imani tofauti na mimi.
Swadakta. Yaani islam ingekuwa dini ya haki kama wanavodai ingekuwa inatawala dunia, na mungu asingeruhusu dini nyingine itawale
 
Swadakta. Yaani islam ingekuwa dini ya haki kama wanavodai ingekuwa inatawala dunia, na mungu asingeruhusu dini nyingine itawale
Je alivyoweka wanyama, vyakula, vinywajink akasema kuleni hivi na msile vile ni kwa nini? Alivyokua adamu bustanin akaambiwa asile lile tunda ni kwa nini?
Jibu ni kukujaribuni je mtamtii katika maamrisho yake au mtakwenda kinyume. Hivyo uwepo wa dini mia au mia mbili ipo iliyosahihi na ni uislamu kazi kwako ukubali au ukatae au ulete unlogical argument skwa maarifa na ujuzi aliokupa wewe. Na ili kuwataini watakaofaulu na watakaoshindwa ndio maana kutakua na kiyama ambapo wapo watakao fuzu watapewa mm pepo waliyoahidiwa na watakao feli basi mafikio yao yatakua ni motoni, allah atujalie pepo yake na atuepushe na adhabu ya moto
 
Familia yeyote, ikisikia Baba dini hii Mama dini hii, tegemea kupata watoto wasio kuwa na msimamo na dini yeyote.

Maana tangu kuzaliwa kwao kutoka kwa wazazi wasioujua Msikiti wala Kanisa, hawana mafundisho yanahusu dini.

Hivyo alieleta mada hii hapa ni zao la ndoa ya kwa mkuu wa Wilaya. Tena afadhari huyu anaetafuta dini akiwa mtu mzima na Watoto wake, naamini hajui kitabu chochote siyo Bibilia wala Qurani.
Mwenye kujua chochote hawezi kuja kuuliza wapi pa kwenda hapa JF.
Aliposema tu amesoma vitabu vyote vya uislam nkajua huyu ni muongo. Nlipoona tu anazungumzia "Kuruan" nkajua huyu anataka kutufanya watoto
 
Back
Top Bottom