Naomba ushauri kuhusu dini

Naomba ushauri kuhusu dini

Familia yeyote, ikisikia Baba dini hii Mama dini hii, tegemea kupata watoto wasio kuwa na msimamo na dini yeyote.

Maana tangu kuzaliwa kwao kutoka kwa wazazi wasioujua Msikiti wala Kanisa, hawana mafundisho yanahusu dini.

Hivyo alieleta mada hii hapa ni zao la ndoa ya kwa mkuu wa Wilaya. Tena afadhari huyu anaetafuta dini akiwa mtu mzima na Watoto wake, naamini hajui kitabu chochote siyo Bibilia wala Qurani.
Mwenye kujua chochote hawezi kuja kuuliza wapi pa kwenda hapa JF.
 
NAOMBA KWANZA ICHUNGUZE MISINGI ZA IMANI HIZI 2 KAMA ZINAVYOJIELEZA.

UKRISTO
- Ni kuamini katika UTATU yaani Mungu,Mwana wa Mungu na Roho Mtakatifu.
-Kuamini kusulubiwa,kufa na kufufuka kwa Yesu.
-Kuamini hakuna maombi yanayoweza mfikia Mungu bila kupitia kwa Yesu.
-Kuamini kuwa Yesu pia ndiye Mungu mwenyewe mkuu.


UISLAMU
-Kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja na hana wa kufanana naye Duniani na Mbinguni.
-Kuamini kuwepo kwa Malaika na utendaji wao.
-Kuamini Vitabu vyake vyote Mwenyewe Mungu vikiwemo Torati,Zaburi,Injili na Quran.
-Kuwaamini Mitume wote walitumwa na Mwenyezi Mungu akiwemo na Yesu.
-Kuamini katika Qadar yake Mwenyezi Mungu,yaani matokeo yote ya kheri na Shari ni katika ruhusa yake.
-Kuamini kuwepo kwa siku ya mwisho,siku ambayo watu wote watafufuliwa kwa ajili ya hesabu ya matendo yao.


Mkuu!Ukijikita katika kuchunguza MISINGI hiyo ya IMANI,nina hakika utapata majibu ya wapi ufuate japo kwa kuanzia.Asante.
 
Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaid ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mktisto mama yangu ndiyo muislam, bahat mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielew kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasabu dini ya kiislam naijua nimesama madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zaman nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.

Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipend kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumban na natumia maji ya baraka wakat mwingi nahis kabisa yananisaidia, halaf nikiwa kanisani nina aman zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubir ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumban redio nasikiliza redio maria tu na naifurahia.

Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sahiv ndiyo nazid kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu nataman waanze mafundisho, au kuna sehem sijielewi?
Ibrahimu aliambiwa atoke nchi yake ya Uru kwenda Kaanani akiwa mtu mzima kuzidi wewe. Jambo la muhimu kuwa kama kweli ni Yesu kakuchagua Yeye mwenyewe atakuonyesha njia. Hapa JF utaambulia upotoshwaji tu.
 
Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaid ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mktisto mama yangu ndiyo muislam, bahat mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielew kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasabu dini ya kiislam naijua nimesama madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zaman nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.

Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipend kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumban na natumia maji ya baraka wakat mwingi nahis kabisa yananisaidia, halaf nikiwa kanisani nina aman zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubir ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumban redio nasikiliza redio maria tu na naifurahia.

Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sahiv ndiyo nazid kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu nataman waanze mafundisho, au kuna sehem sijielewi?

Fanya kile kinachokupa Amani ya moyo wako…
 
Mo
Bado sijafanya maamuzi japo nasukumwa sana na moyo wangu ila sielewi nifanye nini? Nibak ambapo nimezaliwa au niende moyo wangu unapopataka? Itakuaje??
Moyo wako unao wewe nafsi yako ni wewe kama huko mbele kutakuwa na la kuulizwa utaulizwa wewe mkuu siyo wazazi wako na hili wengi hatulijui tunajikuta tunakufa na tai shingoni kisa wazazi wetu wapo hivi wapo vile.

Haiwezi kuwa from no where tu iwe hivi kuna kitu kinakusukuma omba Mungu akuongoze ktk njia sahihi japo bado hajakuacha
 
Kwanza nakupa pole sana,umesema umesoma madrasa na unaijua Dini ya kiislamu?kwa mtu anayeijua Dini ya Kiislam hawezi kuja kuomba msaada hapa jukwaani,naamini wewe ungekuwa msaada kwa wengine kuwaingiza kwenye Uisilamu.

Kama kweli ulichokifanya unakijua na malipo yako utakuwa unayajua baada ya kufa kaburini na siku ya kiaama.Kibaya zaidi unadiriki hata kuwapotosha watoto zako unawaingiza kwenye Ukafiri wakati wazazi wako wamekupa kheri zote? Nimejaribu kuandika lakini nashindwa kuuendelea,angalia wanaokupotosha wanakwambia Dini zote ni sawa,wapi na wapi? Nenda kwa wazazi wako ukawaambie kuhusu msimamo wako nazani watakusaidia zaidi
Kwa yanayoendelea duniani ktk hiyo dini hata ningekuwa mimi humo nisingekaa.

Jana tu nilikuwa nabishana na wenye hiyo dini humu kuhusu waislam huko Nigeria kumchoma moto akiwa hai bint wa Kikristo kisa kadhihaki sijui mitume,yaani utu hamna kabisa bora shauri mtu awe atheist usizidi kumpoteza
 
Mkuu dini sio kabila kwamba huwezi kubadili. Kingine hizi dini tumeletewa na zote zinamuabudu Mungu mmoja. Sali dini ambayo inakupa amani ya moyo. Maisha mafupi na magumu sana kuanza kuumiza kichwa uwe dini gani wakati tayari umeshaoneshwa dini sahihi ya kuifata.

Kuhusu watoto ningependa kufahamu baba yao (mumeo) ni dini gani?
Muislam
 
YESU NI MUNGU!NA BILA KUPITIA KWA YESU MUNGU,HUTOMFIKIA MUNGU!.

Maajabu kweli hayata kwisha hapa duniani.
Ukibakiza hivi vitu kama vitu 'concrete' hutaelewa, mpaka uvipeleke viwe 'abstract' zaidi ndo utaelewa; We hushangai tunaposema Yesu ni Mungu, na hatusemi Mungu ni Yesu......... hushangai kwamba tunatambua na kuamini Yesu ni Mwana wa Mungu hapohapo?
 
Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaid ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mktisto mama yangu ndiyo muislam, bahat mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielew kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasabu dini ya kiislam naijua nimesama madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zaman nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.

Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipend kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumban na natumia maji ya baraka wakat mwingi nahis kabisa yananisaidia, halaf nikiwa kanisani nina aman zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubir ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumban redio nasikiliza redio maria tu na naifurahia.

Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sahiv ndiyo nazid kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu nataman waanze mafundisho, au kuna sehem sijielewi?
Wewe siyo MUISLAMU.
 
Mo

Moyo wako unao wewe nafsi yako ni wewe kama huko mbele kutakuwa na la kuulizwa utaulizwa wewe mkuu siyo wazazi wako na hili wengi hatulijui tunajikuta tunakufa na tai shingoni kisa wazazi wetu wapo hivi wapo vile.

Haiwezi kuwa from no where tu iwe hivi kuna kitu kinakusukuma omba Mungu akuongoze ktk njia sahihi japo bado hajakuacha
Asante sana!
 
siku za binadamu aliyezaliwa na mwanamke ni chache Sana za kuishi duniani.
CHAGUA KWA USAHIHI USIJE UKAJA KUSEMA LAITI NINGEJUA.
 
Ukibakiza hivi vitu kama vitu 'concrete' hutaelewa, mpaka uvipeleke viwe 'abstract' zaidi ndo utaelewa; We hushangai tunaposema Yesu ni Mungu, na hatusemi Mungu ni Yesu......... hushangai kwamba tunatambua na kuamini Yesu ni Mwana wa Mungu hapohapo?
Mkuu!Mimi naamini katika UZIMA WA MILELE kama alivyo ueleza Yesu mwenyewe:-

Yohana 17:3

Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.




Lakini sarakasi nyingine sizihitaji hata.
 
Back
Top Bottom