Huu ujinga sana , Yani unauliza swali alafu kumbe unamajibu mfukoni
Kwa kuwa
Great Bible haikupendwa na watu wengi na
Geneva Bible ilikuwa na maelezo ya pambizoni yaliyotokeza ubishi, iliamuliwa kwamba Biblia iliyosahihishwa itokezwe.
Tafsiri ya
Great Bible ilichaguliwa iwe msingi wa kutafsiri Biblia hiyo. Kazi hiyo ilipewa maaskofu wa Kanisa la Anglikana, na katika mwaka wa 1568 tafsiri ya
Bishops’ Bible (Biblia ya Maaskofu) ilichapishwa.
Ilikuwa buku kubwa lililojaa picha nyingi. Lakini wafuasi wa Calvin waliochukizwa na majina ya kidini ya cheo hawakupenda matumizi ya neno
“bishops” (maaskofu). Kwa sababu hiyo tafsiri ya
Bishops’ Bible haikupendwa sana na watu nchini Uingereza.
Baada ya Mfalme James wa Kwanza kutawazwa kuwa mfalme wa Uingereza mwaka wa 1603,
* aliidhinisha kwamba Biblia nyingine itafsiriwe. Alisema kwamba ili Biblia hiyo isiwaudhi watu, watafsiri walipaswa kuondoa maelezo yoyote yenye kuudhi.
Mfalme James aliutegemeza mradi huo. Mwishowe, wasomi 47 katika vikundi sita vilivyokuwa sehemu mbalimbali nchini humo walitayarisha baadhi ya maandishi yake. Wakitumia tafsiri ya Tyndale na Coverdale, wasomi hao wa Biblia walisahihisha tafsiri ya
Bishops’ Bible.
Hata hivyo, walitumia pia tafsiri ya
Geneva Bible na tafsiri ya Kikatoliki ya
Rheims New Testament ya mwaka wa 1582.
James mwenyewe alikuwa msomi wa Biblia aliyeheshimiwa, na kwa sababu ya mchango wake, tafsiri hiyo ilisemekana kuwa imetolewa kwa heshima ya “James, mkuu aliye na cheo cha juu zaidi na mwenye nguvu.” Akiwa kiongozi wa Kanisa la Anglikana, James alionwa kuwa anatumia mamlaka yake ili kuliunganisha taifa.