Naomba ushauri, kila nikipanga mipango haitimii

Naomba ushauri, kila nikipanga mipango haitimii

Ahsante kwa ushauri wako mzuri
KWENDA KWA MGANGA NI KUMKABIDHI shetani MAISHA YAKO.

MUOMBE MUNGU TOBA, MWAMBIE UMEMKOSEA YEYE ALIYE PEKEYAKE MKUU NA MTAKATIFU... Kisha Muombe Akufanikishe katika njia zako.

Kiufupi kaka upo kwenye vita kubwa sana, ila Mungu bado anakupenda ndio maana unapata hizo ndoto za kukuonyesha upo shule.. na bado leo amekupa neema ya kukutana na ujumbe huu.

Wewe tubu kwanza na uirejeze nafsi yako mikononi mwa Mungu? Maana kwa sasa unamilikiwa na ufalme wa giza. Tubuuuuuuuuuu
 
Sijui Kama nikikushauri utanielewa ila ninachojua hata Mimi nilishapitia situation Kama yako ila nilitumia mjani (weed) nlitumia Kwa wiki tu Mambo yote yalikuwa shwariii nadhani mjani unaweza ukawa suluhisho japo usiutumie Kwa pupa coz hata mm natumia occasionally! Nkitumia Leo naweza pitisha mwez au wiki tatu mpk kutumia tena

Note: mjani una cure ya maradhi mengi ya ulimwengu wa kimwili na kiroho
 
Habari za muda ndugu zangu.
Hope weekend yenu imekaa njema
Wacha nisipoteze muda niingie kwenye mada.

Mimi ni kijana ambae nimekuwa nikihangaika sana kwenye mambo yangu lakini huwa sifanikiwi inshort huwa nina mipango mizuri mno lakini haijawahi kufanikiwa, unaweza kuongea na mtu akakuahidi jambo fulani ila mwisho wa siku atakuja kukukataa tu.

Yaani Jambo nalianza vizuri but mwisho wa siku huwa ni kufeli tu mpaka huwa najiuliza huwa nina mkosi gani, hata kwenye mahusiano nimekuwa ni mtu wa kuhangaika tu. Maana sijawahi kutulia kwenye mahusiano na mtu hata kwa mwezi mmoja.

Kuna mtu akaja kunishauri niende kwa wataalamu basi nikaenda kwa mtaalamu mmoja akaniambia nyota yangu imechukuliwa ndio maana kila nalofanya haliendi.

Nikamuuliza bei akaniambia nimpe 120k, nikampa hiyo hela akanipa madawa nikaogea nikamaliza but sikuona mabadiliko mpaka sasa mambo yangu bado magumu halafu mara nyingi huwa ninasumbuliwa na ndoto za kuwa shuleni tena primary na classmate wangu niliomaliza nao kitambo kile. Sasa sijui nina shida gani ndugu zangu naombeni ushauri nini nifanye ili mipango yangu iweze kwenda maana naona kama nina nuksi.
Nilikuwa na tatizo kama lako sasa nimeshakuelewa kinachokusumbua.
Kabla sijaanza kukupa somo nahitaji kujua wewe ni kabila gani?
Hapo kuna matatizo ya aina mbili yanayohusiana na hiyo shida yako.
1.Mizimu ya kwenu
2.Mambo ya majini/masheitwan
Ukinipa background yako ndio nitaconfirm kinachokusumbua

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
don't underestimate the power of salt, especially stone salt (kidding), namaanisha chumvi ya mabonge.

Halafu kuna mti mmoja siufaham jina, kesho nikikumbuka nitapiga picha nipost maana upo hapa hapa ninapoishi. Mzizi wake noma kwa kusafisha nyota.

WAFIA DINI TAFADHALI PITENI KIMYA KIMYA
Kuna mti mwingine unaitwa kivumbasi ule majani yake hutumika kama dawa ya mbu pia hutumika kwa kazi ya kusafisha nyota.
Lakini shida ya hizi dawa huwezi kupata suluhisho la kudumu mpaka ujue chanzo cha tatizo lako.
Mimi mwenyewe nilihangaika sana karibu miaka 10 napigwa hela na wataalamu nikaja kugundua mwishoni sana chanzo cha tatizo

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Pale unapoamua kwenda kwa kalumanzila principle kuu ni kwamba bei atakayokutajia mwambie wewe una robo ya hiyo pesa mfano wewe aliposema laki na ishirini ungempa elfu 30 na nyingine mwambie baadae. Akikwambia hata nusu sipokei basi jiondokee huyo ni Tapeli tuu...
Mkuu bado sio dawa,kuna wengine huwa wana mikwara sana ukifika anakwambia mimi sitaji gharama siruhusiwi na mizimu yangu lakini ukishatibiwa ukiondoka shida inarudi tena

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Usipende Sana waganga watakugeuza mteja.
Ukiwa masikini ukienda kwa mganga anachukua nyota yako anawauzia wenye pesa.
Mganga na fundi simu wote ni wezi wa Hard Disc za watu.Fundi simu uchukua kizima ukufungia kibovu Ili kesho urudi.
Muhimu simama kama wewe tafuta vitabu vya mafunzo ya positive power, positive thinking.
Ujitibu mwenyewe tatizo lako.
Tafuta person mentor wakushauri au wafikrie badala yako Ili kufanikisha mambo yako.
Kama ufanikiwi jambo lifanikishe kupitia kwa mtu mwingine unayemuamini.
Waganga hawana msaada.
 
Jam

Jambo moja tu acha zinaa utatoboa,zinaa inaleta ufakiri. Kama huna mke fanya uoe na maisha yako hayo hayo utakuja kuishukuru Siku moja.
Kuchanganya wanawake pia ni sababu mojawapo ya kukumbwa na mapepo au nuksi na ndio maana nahitaji kupata background ya mtoa mada nijue ni wapi anaangukia

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
No muda mwingine unaweza kujiona masikini lakini kumbe hukutakiwa kuwa maskini kuna vitu vinazuia utajiri wako

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
Ooohhh hallelujah!!! Ni kweli usemalo 😁
Itakua niliumbwa niwe tajiri kuna vitu havijakaa sawa nadhani, mfano nikitembea juani naumwa kichwa sana hadi huwa nahisi sikutakiwa kuwa masikini mimi 😂😂
 
Ooohhh hallelujah!!! Ni kweli usemalo
Itakua niliumbwa niwe tajiri kuna vitu havijakaa sawa nadhani, mfano nikitembea juani naumwa kichwa sana hadi huwa nahisi sikutakiwa kuwa masikini mimi
Ukiona unatumia input kubwa sana kupambana halafu output yake ni kidogo sana hapo lazima ujiulize mara mbili mbili,dunia haiko fair

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Yawezekana unawakumbuka sana. Ila kama unaota watu ambao hukua hata na mazoea nayo hilo ni tatizo.
Sidhani, ila huwa nahisi ni ndoto ambayo ina ujumbe ndani yake ila ndio sijawahi kuelewa....na siku nikielewa sitaiota tena
 
Sidhani, ila huwa nahisi ni ndoto ambayo ina ujumbe ndani yake ila ndio sijawahi kuelewa....na siku nikielewa sitaiota tena
Ukinielezea lifestyle yako unaishije naweza kujua tatizo,huwa unaenda mkoani kwenu kutambika?unafanya ibada?ni mlevi au mzinzi?hizo ndio sababu kuu na ya mwisho ni wachawi tu kukuandama

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Kasafishe makaburi ya mababu zako haraka sana. Utakuja kunishukuru baadae.

Usione sisi tunarudi nyumbani kila disemba alafu mambo yetu yananyooka.

Soma sana ,sali sana lakini baadhi ya mila na desturi usiache kamwe.
Kusafisha kama kuwakumbuka na sio kama ibada.
Maana kutambika mizimu ni kumuabudu shetani
 
Back
Top Bottom