Nani yuko nyuma ya wimbi la mapinduzi ya kijeshi barani Afrika?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111447199000.jpg


Katika kipindi cha miaka minne (2020-2023) bara la Afrika limeshuhudia mapinduzi ya kijeshi katika nchi sita (Burkina Faso, Chad, Guinea, Mali, Niger na Sudan). Wimbi hili limekuja baada ya kipindi kirefu cha utulivu, ambao ulilisaidia bara la Afrika kuwa moja ya maeneo yenye ongezeko la uchumi na uwekezaji. Lakini katika hali ya kushangaza, limeibuka wimbi la mapinduzi ambalo linatishia amani, utulivu na maendeleo ya Afrika.

Ni karibu zaidi ya muongo mmoja sasa umepita tangu majeshi ya nchi za Afrika yaache kutwaa madaraka kwa nguvu, hii ni kutokana na kuwa Umoja wa Mataifa na nchi kubwa za magharibi kukemea vikali vitendo vya mapinduzi ya kijeshi. Hatua hiyo iliungwa mkono na Umoja wa Afrika na jumuiya zake za kikanda, ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikizilaani nchi za magharibi kwa kuwa nyuma ya mapinduzi mengi ya kijeshi.

Kwa muda mrefu sasa vyombo vya habari vya nchi za magharibi vimekuwa vikijenga picha ya Afrika kuwa ni bara lenye migogoro na vita kutokana na kugombea madaraka, lakini mzizi wa migogoro hiyo ukifuatiliwa, kiini chake kinaonekana kwenye nchi za magharibi. Ukweli huu ulidhihirika baada ya nchi za magharibi kutambua kuwa kuchochea migogoro barani Afrika ni kinyume na maslahi yao, na zikaanza kuwa na sauti moja ya kukemea vikali na hata kukataa kushirikiana na serikali zilizoingia madarakani kwa nguvu.

Kuibuka kwa wimbi jipya la mapinduzi ya kijeshi katika nchi za Afrika, na kitendo cha nchi za magharibi kutoyakemea vikali mapinduzi hayo kunaonesha kuyavumilia mapinduzi hayo. Lakini pia baadhi ya wanajeshi walio nyuma ya mapinduzi hayo, ni wale waliopewa mafunzo katika vyuo vya kijeshi vya nchi za magharibi au walio na mawasiliano ya karibu na idara za usalama za nchi za magharibi.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mabadiliko makubwa kwenye siasa za nchi za Afrika. Kwa sasa mwelekeo wa serikali za nchi za Afrika zinazochaguliwa na wananchi, umekuwa ni kwenye kuzingatia maendeleo, maslahi ya wananchi na maslahi ya taifa. Hali hii imezifanya serikali za nchi za Afrika kuwa karibu zaidi na nchi au mashirika ambayo yakidhi mahitaji ya nchi zao. Hali hii haizufurahishi baadhi ya nchi za magharibi, ambazo zimezoea kuwa na ukaribu wa serikali vibaraka.

Kutokana na nchi za Afrika kutambua mahitaji ya maendeleo yake katika mazingira ya sasa, na kuwa na machaguo zaidi ya washirika tofauti na zamani wakati zilikuwa zikitegemea zaidi nchi zilizozitawala, nchi za Afrika zimekuwa zinanufaika zaidi kutoka kwa washirika wake wapya, na manufaa zilizokuwa zikiyapata nchi za magharibi kutokana na kuendelea kwa ukoloni mamboleo yanaendelea kupungua. Hali hii imeweka mazingira yanayofanya nchi za magharibi kuvumilia na hata kukalia kimya mapinduzi ya kijeshi.

Tunapojiuliza ni kwanini nchi za magharibi zimekuwa zikiyakalia kimya mapinduzi haya bila kuchukua hatua au kutoa sauti kali, majibu yanatukumbusha waliokuwa nyuma ya mapinduzi hayo mara kwa mara. Tumesikia jumuiya za kikanda za nchi za Afrika zikikemea vikali mapinduzi ya Niger, Umoja wa Afrika umetoa tamko kali ya kutaka wanajeshi waliopindua serikali kurudisha utawala wa kikatiba ndani ya siku 15 na kumwachia na kumrejesha madarakani Rais Mohamed Bazoum. Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS imesema itachukua hatua ikiwa ni pamoja na vikwazo dhidi ya wanajeshi waliotwaa madaraka, na hata kutumia nguvu kama ikihitajika ili kurudisha utawala wa kikatiba.

Ufaransa, nchi ya magharibi yenye uhusiano wa karibu sana na Niger, imeshangaza jumuiya ya kimataifa baada ya kulaani wananchi wenye hasira wanaotaka kuvamia ubalozi wa Ufaransa, bila kuweka wazi kiini cha hasira ya watu hao dhidi Ufaransa.
 
... China taifa lisilojali ufisadi wa viongozi wa Afrika as long maslahi yake hayaguswi! China taifa linalolinda sana mafisadi na madikteta ya Afrika. China taifa lisilojali demokrasia na utwala bora Afrika!

Hayo ndio kiini cha wananchi kuwachoka viongozi mafisadi na madikteta; wanaotawala nchi zao kidhalimu! Hali hii matokeo yake ni wananchi kuwachoka watawala na hatimaye mapinduzi. Acheni propaganda mfu za mlengo wa ovyo wa ukomunisti uchwara uliofeli.
 
Chanzo cha migogoro yetu ya afrika Ni upungufu wetu wa akili wa afrika wenyewe na ndugu zao waarabu


Imagine unaongoza watu ambao mwekezaji akipewa mradi wanasema nchi imeuzwa

Imagine unaongoza nchi ambayo rais akipita wanaanza kusema ati huyo ni wa wakikuyu sio wa luo mara ni wa wakamba.

Imagine unaongoza nchi ambayo watu wake wanampigania mungu wao na kulazimisha watu wote wafuate tamaduni zao

Imagine Kiongozi anagombea uongozi kisa amesifiwa kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Alafu katika Nchi hizo zinazopinduliwa utakuta bendera ya urusi inapeperushwa.
 
Lakini, Ufaransa ndiye mtakatifu. Siyo?
... wewe wasema. Huyo aliyeanzisha mada kaanzisha kutaka kuonesha China haina contribution yoyote kwa matatizo ya Afrika wakati ndiye joka no.1 kwa sasa.
 
View attachment 2704333

Katika kipindi cha miaka minne (2020-2023) bara la Afrika limeshuhudia mapinduzi ya kijeshi katika nchi sita (Burkina Faso, Chad, Guinea, Mali, Niger na Sudan). Wimbi hili limekuja baada ya kipindi kirefu cha utulivu, ambao ulilisaidia bara la Afrika kuwa moja ya maeneo yenye ongezeko la uchumi na uwekezaji. Lakini katika hali ya kushangaza, limeibuka wimbi la mapinduzi ambalo linatishia amani, utulivu na maendeleo ya Afrika.

Ni karibu zaidi ya muongo mmoja sasa umepita tangu majeshi ya nchi za Afrika yaache kutwaa madaraka kwa nguvu, hii ni kutokana na kuwa Umoja wa Mataifa na nchi kubwa za magharibi kukemea vikali vitendo vya mapinduzi ya kijeshi. Hatua hiyo iliungwa mkono na Umoja wa Afrika na jumuiya zake za kikanda, ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikizilaani nchi za magharibi kwa kuwa nyuma ya mapinduzi mengi ya kijeshi.

Kwa muda mrefu sasa vyombo vya habari vya nchi za magharibi vimekuwa vikijenga picha ya Afrika kuwa ni bara lenye migogoro na vita kutokana na kugombea madaraka, lakini mzizi wa migogoro hiyo ukifuatiliwa, kiini chake kinaonekana kwenye nchi za magharibi. Ukweli huu ulidhihirika baada ya nchi za magharibi kutambua kuwa kuchochea migogoro barani Afrika ni kinyume na maslahi yao, na zikaanza kuwa na sauti moja ya kukemea vikali na hata kukataa kushirikiana na serikali zilizoingia madarakani kwa nguvu.

Kuibuka kwa wimbi jipya la mapinduzi ya kijeshi katika nchi za Afrika, na kitendo cha nchi za magharibi kutoyakemea vikali mapinduzi hayo kunaonesha kuyavumilia mapinduzi hayo. Lakini pia baadhi ya wanajeshi walio nyuma ya mapinduzi hayo, ni wale waliopewa mafunzo katika vyuo vya kijeshi vya nchi za magharibi au walio na mawasiliano ya karibu na idara za usalama za nchi za magharibi.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mabadiliko makubwa kwenye siasa za nchi za Afrika. Kwa sasa mwelekeo wa serikali za nchi za Afrika zinazochaguliwa na wananchi, umekuwa ni kwenye kuzingatia maendeleo, maslahi ya wananchi na maslahi ya taifa. Hali hii imezifanya serikali za nchi za Afrika kuwa karibu zaidi na nchi au mashirika ambayo yakidhi mahitaji ya nchi zao. Hali hii haizufurahishi baadhi ya nchi za magharibi, ambazo zimezoea kuwa na ukaribu wa serikali vibaraka.

Kutokana na nchi za Afrika kutambua mahitaji ya maendeleo yake katika mazingira ya sasa, na kuwa na machaguo zaidi ya washirika tofauti na zamani wakati zilikuwa zikitegemea zaidi nchi zilizozitawala, nchi za Afrika zimekuwa zinanufaika zaidi kutoka kwa washirika wake wapya, na manufaa zilizokuwa zikiyapata nchi za magharibi kutokana na kuendelea kwa ukoloni mamboleo yanaendelea kupungua. Hali hii imeweka mazingira yanayofanya nchi za magharibi kuvumilia na hata kukalia kimya mapinduzi ya kijeshi.

Tunapojiuliza ni kwanini nchi za magharibi zimekuwa zikiyakalia kimya mapinduzi haya bila kuchukua hatua au kutoa sauti kali, majibu yanatukumbusha waliokuwa nyuma ya mapinduzi hayo mara kwa mara. Tumesikia jumuiya za kikanda za nchi za Afrika zikikemea vikali mapinduzi ya Niger, Umoja wa Afrika umetoa tamko kali ya kutaka wanajeshi waliopindua serikali kurudisha utawala wa kikatiba ndani ya siku 15 na kumwachia na kumrejesha madarakani Rais Mohamed Bazoum. Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS imesema itachukua hatua ikiwa ni pamoja na vikwazo dhidi ya wanajeshi waliotwaa madaraka, na hata kutumia nguvu kama ikihitajika ili kurudisha utawala wa kikatiba.

Ufaransa, nchi ya magharibi yenye uhusiano wa karibu sana na Niger, imeshangaza jumuiya ya kimataifa baada ya kulaani wananchi wenye hasira wanaotaka kuvamia ubalozi wa Ufaransa, bila kuweka wazi kiini cha hasira ya watu hao dhidi Ufaransa.
Unauliza swali au jibu? Ni bwana wao Russia
 
Back
Top Bottom