Nani mkali kati ya Diblo Dibala na Dally Kimoko

Umemuacha SHESHE KALONDA msikilie kwenye ile ABISINA YA PEPE KALE


Tuko pamoja mkuu wangu hawa jamaa walikuwa wanatupa vitu adimu sana lakini hata hapa nyumba kulikuwa na wakali wa mpini wa mpini wa solo enzi hizo ambao kwa uchache naomba niwataje. Mose sengo Fan Fan,Nguza Viking [Babu seya],Supreme Ndala Kasheba na gita lake la nyuzi kumi na mbili,Kawale Motimwana na Mbaraka Mwinshee Mwaruka.

muziki wa kizazi kipya hauna fursa za kuwa na wakali wa ala mbali mbali za muziki kazi zote zinafanywa na computer badala ya utundu wa wasanii.Hali ikiachwa iendelee kwa muda mrefu uenda tutakuja kuwa na kizazi cha wanamuziki wasiojua kutumia ala za muziki.
 
Another great work by Franco....Simaro ndio mtunzi...Marquiz yetu ilijaribu kuiga hii kitu na wimbo wa 'HUBA' aloimba Assosa lakini wapi bwana....OK JAZZ forever

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=OAQuXaO7nCw&feature=related[/ame]
 
Kakuruvi,

Line up hapa(toka kushoto) Djo Mpoyi,Pape Ndombe Opetum,Madilu(kalikuwa katooto,just joined) na mtu wangu 'Josky' Kiambukuta Londa

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=OAQuXaO7nCw&feature=related[/ame]
 
Hapana...just happened to like music na historia yake pia....lakini nyaisanga ni mmoja wa resource people wangu...sadly hayupoten R1 maana ijumaa nilikuwa sikosi HIZI NAZO a program from 9 to midday...hawa alowaachia wanavurunda tu...
 
Hapana...just happened to like music na historia yake pia....lakini nyaisanga ni mmoja wa resource people wangu...sadly hayupoten R1 maana ijumaa nilikuwa sikosi HIZI NAZO a program from 9 to midday...hawa alowaachia wanavurunda tu...

Kuna kipindi kingine RFA alhamisi kuanzia saa 4 usiku nacho kinakumbusha mbali. Nyaisanga anawajua utafikiri amesoma nao.
 
Nawasalimu Great Thinkers,

Kama kuna watu waliojaliwa vipaji na wamevitumia ni hawa jamaa wawili Diblo Dibala na Dally Kimoko, hawana utani wanapokamata mpini, mfano Diblo Dibala (Extra Boy), Dally Kimoko (Liza), si mchezo achilia mbali bendi zao za kazi ila wamekuwa wakitumiwa na bendi nyingine kurecord, kama kuna mwenye nyimbo walizopiga mpini leteni humu tusikie mambo, nani zaidi kati ya hawa magwiji wa mpini?

- Mkuu saafi sana I like this, ngoja nitairudia later!

Respect.


FMEs!
 
Nawasalimu Great Thinkers,

Kama kuna watu waliojaliwa vipaji na wamevitumia ni hawa jamaa wawili Diblo Dibala na Dally Kimoko, hawana utani wanapokamata mpini, mfano Diblo Dibala (Extra Boy), Dally Kimoko (Liza), si mchezo achilia mbali bendi zao za kazi ila wamekuwa wakitumiwa na bendi nyingine kurecord, kama kuna mwenye nyimbo walizopiga mpini leteni humu tusikie mambo, nani zaidi kati ya hawa magwiji wa mpini?

- Mkulu ni kweli hawa wakulu wamekuwa magwiji sana wa solo huko Zaire, ingawa wote wawili wanatumia style zilizopitwa kidogo, lakini bado naamini kwamba Dally Kimoko anaweza kuwa na edge, kwa sababu Diblo siku zote amekuwa akipiga na wanamuziki wasiojulikana sana kama Kimoko, ambaye amepiga sana na Le` Grande Monsieur Pepe Kale au kwa jina maarufu kule Bukavu, Kabasele ya Mpanya na bendi yake ya Emperior Bakuba, ingawa Diblo naye aliwahi kupiga naye, lakini sio kwenye album nyingi kama mwenziwe yaani Kimoko.

- Diblo amefahamika sana akiwa na Soukous ambao hawakuwa na ubavu mbele ya Pepe Kalle, ingawa na yeye akiwa na hawa Soukous ameweza kufanya sana maajabu internationally. Kwa hiyo an edge ya Kimoko over Diblo, inachangiwa zaidi na kushiriki kwake sana na Le Grande Pepee! Mungu amlaze pema peponi. Ingawa pia Lokassa ya Mbongo naye alikuwa na enzi zake, siku hizi anaishi sio mbali sana na ninapoishi, anaonekana anakula pension tu na ni very humble man!

Respect.


FMEs!
 

Tuko pamoja mkuu wangu hawa jamaa walikuwa wanatupa vitu adimu sana lakini hata hapa nyumba kulikuwa na wakali wa mpini wa mpini wa solo enzi hizo ambao kwa uchache naomba niwataje. Mose sengo Fan Fan,Nguza Viking [Babu seya],Supreme Ndala Kasheba na gita lake la nyuzi kumi na mbili,Kawale Motimwana na Mbaraka Mwinshee Mwaruka.

muziki wa kizazi kipya hauna fursa za kuwa na wakali wa ala mbali mbali za muziki kazi zote zinafanywa na computer badala ya utundu wa wasanii.Hali ikiachwa iendelee kwa muda mrefu uenda tutakuja kuwa na kizazi cha wanamuziki wasiojua kutumia ala za muziki.


- Mkuu saafi sana yaani ile enzi ya kina Kasaloo na ndugu yake Kyanga, Mafumu Bilali, Mzee Mwema Mudjanga, Hatibu Itei Itei, Fataki Masumbuko ya dunia, Kanku Kelly na Mzee Kikumbi Mwanza Mpango, ahggarrrrrr halafu pale kwa Mbaraka kulikuwa na dogo mmoja kwa jina Charles Kasembe, ilikuwa moto wa kuotea mbali sana, hasa mtindo wa Masika Zole Zole!

- Uzuri mmoja mkuu wabongo washitukaji, siku hizi wamewagomea hawa bongo-Flav bila ya kua na bendi hawaendi, sasa wote siku hizi wanaanzisha bendi kabisaa, saafi sana!

Respect.


FMEs!
 
ila tusiende mbali Joseph Mulenga na Selemani Mwanyiro walikuwa na balaa miaka ilee mtu alikuwa anaitwa computer...si balaa hilo.
 
kuna hii kitu nyingine pia ilikuwa balaa Dali Kimoko

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=G9tjVG_ANXE"]http://www.youtube.com/watch?v=G9tjVG_ANXE[/ame]
 
Wadau,

Kwanza nianze kusema kuwa LOKETO haikuwa BENDI gorup.
Hawa jamaa walikuwa na bendi zao za kila siku na time to time wanaamua kukutana na kula good time pamoja. Ndiyo maana safu zao siku zote zilikuwa zinabadilika ingawa kuna jamaa siku zote walikuwa hapo.

Loketo ama KIUNO walipata sifa kubwa sana kwa muda mfupi kwani walikuwa ni watu wanafahamu nini wanataka na kukifanya kwa umahiri mkubwa na hamna eti MTU WA KUJAZIA. Mwanzo walianza na Diblo Dibala aliyetoka kwa Kanda Bongo Man na kuanzisha kundi lake mwenyewe baadaye. Baadaye wakawa na Dally Kimoko. Moja ya watu mashuhuri aliyekuwa kwenye kundi hili ila siku hizo hafahamiki ni Awilo Longomba.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=QBCCcH-QJWY[/ame]
(Ukianzia 4:00 utamsikia Awilo akiimba/Rap na mbele kidogo mama anasema Dally Kimoko).

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=UNXVIXcpbUo[/ame]

(Ukianzia 3:15 utasikia wakitaja jina la Awilo Longomba ambaye siku hizo ni Mpiga drums unazosikia kwenye wimbo hapo juu).


Ki ufundi, Diblo Dibala alikuwa akipiga gitaa ki-Afrika zaidi yaani nyuzi moja moja. Dally Kimoko alianza kuweka zile sauti za gitaa kama za Rock Musics yaani ufundi wa akina Slash wa Gun N' Roses au Mzee Jimmy Hendrix. Ila wengine pia walianza baadaye kuiga kama akina Zaiko langa langa na Waafrika tuliipenda maana walikuwa wakiweka sauti tu ila upigaji unabaki ule ule.
 
- Ooh yeah, halafu kina Bitchuka, Cosmas Chidumule, Marijani Rajabu, George Mpupua, Hemedi Maneti, Juma ubao na kina Wema Abdallah! na Western Jazz na Saboso, kina Remmy na Segere Matata!

Respect.


FMEs!
 
Wadau,

Kwanza nianze kusema kuwa LOKETO haikuwa BENDI gorup.
Hawa jamaa walikuwa na bendi zao za kila siku na time to time wanaamua kukutana na kula good time pamoja. Ndiyo maana safu zao siku zote zilikuwa zinabadilika ingawa kuna jamaa siku zote walikuwa hapo.

Loketo ama KIUNO walipata sifa kubwa sana kwa muda mfupi kwani walikuwa ni watu wanafahamu nini wanataka na kukifanya kwa umahiri mkubwa na hamna eti MTU WA KUJAZIA. Mwanzo walianza na Diblo Dibala aliyetoka kwa Kanda Bongo Man na kuanzisha kundi lake mwenyewe baadaye. Baadaye wakawa na Dally Kimoko. Moja ya watu mashuhuri aliyekuwa kwenye kundi hili ila siku hizo hafahamiki ni Awilo Longomba.

http://www.youtube.com/watch?v=QBCCcH-QJWY
(Ukianzia 4:00 utamsikia Awilo akiimba/Rap na mbele kidogo mama anasema Dally Kimoko).

http://www.youtube.com/watch?v=UNXVIXcpbUo

(Ukianzia 3:15 utasikia wakitaja jina la Awilo Longomba ambaye siku hizo ni Mpiga drums unazosikia kwenye wimbo hapo juu).


Ki ufundi, Diblo Dibala alikuwa akipiga gitaa ki-Afrika zaidi yaani nyuzi moja moja. Dally Kimoko alianza kweka zile sauti za gitaa kama za Rock Musics yaani ufundi wa akina Slash wa Gun N' Roses au Mzee Jimmy Hendrix. Ila wengine pia walianza baadaye kuiga kama akina Zaiko langa langa na Waafrika tuliipenda maana walikuwa wakiweka sauti tu ila upigani unabaki ule ule.


- Hapo Mkuu umenikumbusha enzi za Nyoka Longo, ninayo DVD yake moja akiwa mdogo sana na bendi yake wanapiga nje pamoja na Dindo Yogo akiwa mdogo sana,

- Si unajua enzi hizo Zaire ni lazima uanzie kupiga nje, after a while ukishaonekana na ile kampuni ya bia Primus au sigara Marlboro, ndio wanaku-sponsor unaanza kupiga ndani ya ukumbi, sasa unakuwa umeuchinja for good!

- Halafu pia kuna DVD nyingine ya kina Jibe Mpyana, Allain Makaba, Blaize Bulla, Werason, Dominguez, Philipo, Sekeminyo Manyata, Allein Mpella Afande, Generale Kweik, na Atalaku Robero na Wenge BCBG original wakiwa wanapiga mtaani, enzi hizo wanasoma shule saafi sana.

Respect.


FMEs!
 
FMES naona siasa za Tanzania zimekuchosha maana uko anga za huku siku hizi huchomoki - Merry Xmass.
 
Back
Top Bottom