Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,929
Kwa muda wa miaka 10 hadi sasa ulimwengu wa soka umeshikiliwa na magwiji wawili wa soka wanaotesa uwanjani na kuchukua tuzo kubwa ya Ballon d'Or kwa muda wote huo. Lakini sasa kuna vipaji vipya vinaonekana ambavyo vitakuja kutesa kipindi hiki ambacho Messi na Ronaldo wanaelekea ukingoni.
Kuna wachezaji wengi wazuri na wadogo; Hazard, Neymar, Mbappe, Pogba na Dyabala. Hawa wanaonekana kuwa ni moto kwa sasa na watakuja kuchuana vikali sana kwenye tuzo hiyo ya ballon d'or tuzo kubwa kwenye ulimwengu wa soka.
Sasa wapenzi wa Kandanda: Je, kati ya hawa ni nani atakuja kuwatesa wenzake na kuchukua tuzo hii mara kadhaa kuzidi wote hawa? Au kuna mwingine tofauti na hawa ambaye anaweza kuwa mbabe wa tuzo hiyo?
Kuna wachezaji wengi wazuri na wadogo; Hazard, Neymar, Mbappe, Pogba na Dyabala. Hawa wanaonekana kuwa ni moto kwa sasa na watakuja kuchuana vikali sana kwenye tuzo hiyo ya ballon d'or tuzo kubwa kwenye ulimwengu wa soka.
Sasa wapenzi wa Kandanda: Je, kati ya hawa ni nani atakuja kuwatesa wenzake na kuchukua tuzo hii mara kadhaa kuzidi wote hawa? Au kuna mwingine tofauti na hawa ambaye anaweza kuwa mbabe wa tuzo hiyo?