Nani aliyemuumba Mungu?

Nani aliyemuumba Mungu?

😂 unalazimisha kua ninaamini uchawi kwa sababu naamini hewa ipo? We jamaa mbona una reasoning mbaya hivyo?

Siamini uwepo wa mungu wala uwepo wa uchawi na si kwa sababu sivioni, ni kwa sababu hakuna njia ya kuprove sio kwa macho wala sense nyingine zozote. Hewa ina njia nyingi sana za kuprove kua ipo, nakushangaa wewe hadi utumie macho ndiyo unajua kua kitu kipo? Hehe kuna pua zinanusa, ngozi inahisi, sikio linasikia, sauti mbona huioni ila unasikia? Hahaha we jamaa, kuna vitu hatuwezi sense kwa sensor tulizonazo ndiyo maana tunatengeneza sensor kwa kutumia sayansi sio kukaa na kusema tenganisha maji yakaachana.

Hahaha watu mnaoamini mungu mnachekesha, njoo na argument nzuri hiyo uliyotoa hapo ni bs
Maelezo yako yanaonyesha wazi ya kuwa :
1. Humjui Mungu unae kataa kuwa yupo
2. Huwezi kuthibitisha hilo ya kuwa Mola hayupo

Sasa nina swali la msingi umejuaje kama Mola hayupo na unawezaje kumjadili usie mjua ? Huu ujasiri unaupata wapi ?
 
Hata hiyo bible bado ina mapungufu mengi mbona ... Science inapokuja na tafiti za kuhusu jambo Fulani bado inatoa uwanja kwa watu wengine kulichunguza jambo hilo na kulitoa kasoro ..hii ni tofauti na masuala yenu ya kiimani "katika vitabu vyenu ukisoma maswala ya imani unapaswa kua mini tu bila fact ukianza kuhoji utaambiwa kuwa unalaana .huna akili umekengeuka etc .. Science haiko hivyo mkuu ndio maana kuna aliyegundua gari kisha akaja mwingine akagundua wipers na kuziweka katika gari hilo hilo .....

Halafu mbona huwa mnaiongelea science vibaya when it comes katika competition za dini na science wakati huo huo sisi wote dunia nzima tuna itumia science katika ili tuweze kuishi kuendana na mazingira ya kiulimwengu " hapo ulipo unatumia simu na kutype jf kitu ambacho kimesababishwa na science lakini hizo dini zenu zimeshindwa hata kuunda uma na kijiko still hamtaki kuipa science kipaumbele ....??

Sent using Jamii Forums mobile app
Mapungufu ya vitabu vya Dini ni uhai au usahihi au uhalisia wa NENO kutoka kwa mtamkaji kwenda kwa msikilizaji na hatimae muelezeaji-Communication break down.
Miaka elfu mbili ya NENO ni mingi sana.
Neno au Thought ni kitu kilichoumbwa na Chenye Nguvu-Kinaishi.Kitaishi milele ikiwa mwenye kuumba hilo neno anayo nguvu iliyoenea na hilo NENO liwe linajitegemea.Lina simama.

Kuhusu kuhoji Neno au dini wala haijakatazwa kuhoji tena ni muhimu kwa maendeleo ya binadamu.

Science ni Gods intelligence,kumjua Mungu ndani ya Science ni muhimu na inafaa.

Science inachambuliwa kila Siku Ndo maana hata Virus iliondolewa kwenye kundi la micro organism,hili lilitokea miaka ya 1998.
 
Mungu muweza wa yote

Mwenye upendo kwa wote

Huyu mungu anaye hubiriwa hivi katika vitabu hajawahi kuexist .. Kwa sababu wote tunashuhudia kuwa anajinadi kwamba ana uwezo wa yote lakini ana shindwa kuijua hata future ya viumbe wake .... So hauoni kuwa hapo kuna contradiction ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Weka ushahidi usicheze na maneno na kuzunguka mbuyu. Unajuaje kama Mola hayupo ? Thibitisha hilo usilete dibaji.

Hakuna contradiction hapo, hapo unatakiwa kuilaumu akili yako kuwa ndogo na kushindwa kung'amua jambo husika.
 
Ili mtu ajibiwe swali la namna hii inabidi kwanza kujua imani yake
 
1. Mbona unarudia swali nimekujibu kwamba uthibitisho una definition ndani yake.

Wewe unajua kanuni za kuanduka insha, kwamba kitu cha kwanza kuandika ni definition ya subject yako?

Kama hujui kwamba katika proof kuna definition, kwamba huwezi ku prove kitu ambacho hakina definition, basi una matatizo makubwa zaidi.

Define Mungu ni nini.

Thibitisha Mungu yupo.



Sent from my typewriter using Tapatalk
Kama uthibitisho una definition ndani yake kwanini wewe unaniambia ni define mungu ni nini kisha unaniambia nithibitishe? Huoni kuwa hivyo ni vitu viwili vilivyotengana?

Ingekiwa uthibitisho una definition ndani yake basi usingetaka upewe definition na kisha uthibitisho badala yake ungedai uthibitisho maana definition ipo ndani yake.
Ndio maana nikasema kama kitu hukijui huwezi kudai uthibitisho kwanza.
 
Mungu hayupo, mwanzoni ilianza kama story za hadithi tu, sema mabadiliko yanavyotokea falme nyingine zikaanza kutumia dini kama njia ya kucontrol watu, watu walivyo vilaza wakashika wanayoambiaa 100%, mwanzoni kulikua na miungu kibao ila muda unavyozidi kwenda falme yako kama ina nguvu zaidi watu wanaishia kukubali kua mungu wako ni sahihi kuliko wa kwao, huyu mungu wa wakristo wa sasa amekua very popular kuliko miungu mingine sababu tu alibebwa sana na falme kubwa kama za waroma. Ila yeye naye ni story tu hakuna lolote.

Ukitaka kuamini kua miungu yote imetungwa tu na haipo in reality soma vitabu vyao tu, anza page moja unafunua uone upuuzi uliojaa, very inconsistent, hapa unaambiwa alifanya hiki tarehe 1 page ya pili unaambiwa hakufabya hicho alifanya kingine 😂 muumba ulimwengu hawezi kua kilaza namna hiyo hajui hata kuandika kakitabu kuelezea story yake.

So at the end of the day mungu hayupo, hakuna aliyewahi kumuona, hakuna aliyeona muujiza wowote zaidi ya coincidences au kuchezewa mazingaombwe, wengine wana-hallucinate tu alafu wanakuja kusema ni mungu 😂 😂 dumb.
Ukiomba proof badala ya kuja na kitu kinachoweza kuprove wanakuja na kifungu kutoka kwenye kitabu chao feki, sio njia ya kuprove hiyo, ukitaka kuprove huwezi tumia kitu ambacho tunakipinga tumia source nyingine au tuambie tutengeneze experiment flani itakayofanya tuprove kua mungu kweli yupo.
Sio kila mwenye kusema Mungu yupo anaamini vitabu vya dini, hivyo hoja yako ni nyelesi sana.
 
Huu ni uzi mwingine tena sijaona bado mtu aliyeweza kudhibitisha mungu yupo.
Kwa nini mnashindwa kuthibitisha mungu yupo? Shida inakuja wapi?
Shida ni kwamba watu hawamini kwa sababu kuna uthibitisho Bali kuamini kuna taratibu zake ambazo ndio humfanya mtu aamini, sasa wewe ukija kumwambia akupe uthibitisho we ndio unakuwa na tatizo na kuelewa imani.

Suala la Mungu ni la imani hivyo shida inaanzia hapo unapoanza kutaka mtu athibitishie Mungu wakati ni imani.
 
Yaani Hawa jamaa sijui wana matatizo gani ' miaka nenda miaka rudi wanashindwa kuthibitisha kile wanacho kiamini kama kipo halafu walivyo kuwa hawana haya bado wana endelea kukiabudu hicho kitu ambacho wao mwenyewe wameshindwa kuthibitisha uwepo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani aliwahi kuthibitisha anachokiamini? Unaongea vitu visivyo na uhalisia hebu mumwambie atheist mmoja hapo ajaribu kuthibitisha kitu kimoja anachokiamini.
 
Kama uthibitisho una definition ndani yake kwanini wewe unaniambia ni define mungu ni nini kisha unaniambia nithibitishe? Huoni kuwa hivyo ni vitu viwili vilivyotengana?

Ingekiwa uthibitisho una definition ndani yake basi usingetaka upewe definition na kisha uthibitisho badala yake ungedai uthibitisho maana definition ipo ndani yake.
Ndio maana nikasema kama kitu hukijui huwezi kudai uthibitisho kwanza.
Nakwambia hivyo kwa sababu wewe ni slowpoke.

A moronic slowpoke at that.

Define Mungu ni nini.

Thibitisha yupo.


Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Hata hiyo bible bado ina mapungufu mengi mbona ... Science inapokuja na tafiti za kuhusu jambo Fulani bado inatoa uwanja kwa watu wengine kulichunguza jambo hilo na kulitoa kasoro ..hii ni tofauti na masuala yenu ya kiimani "katika vitabu vyenu ukisoma maswala ya imani unapaswa kua mini tu bila fact ukianza kuhoji utaambiwa kuwa unalaana .huna akili umekengeuka etc .. Science haiko hivyo mkuu ndio maana kuna aliyegundua gari kisha akaja mwingine akagundua wipers na kuziweka katika gari hilo hilo .....

Halafu mbona huwa mnaiongelea science vibaya when it comes katika competition za dini na science wakati huo huo sisi wote dunia nzima tuna itumia science katika ili tuweze kuishi kuendana na mazingira ya kiulimwengu " hapo ulipo unatumia simu na kutype jf kitu ambacho kimesababishwa na science lakini hizo dini zenu zimeshindwa hata kuunda uma na kijiko still hamtaki kuipa science kipaumbele ....??

Sent using Jamii Forums mobile app
Bora masuala ya kiimani hujulikana ni imani na husisitizwa hilo ila kwenye sayansi huwa jambo halielezwi kama kama maoni au mtazamo wa wakati huo Bali huchukuliwa ndio ukweli wenyewe kwamba limefanyiwa utafiti wa kisayansi ila ajabu baadaye unakuja utafiti mwengine na kuonesha ule ukweli wa kisayansi haukuwa kweli maana una makosa.
 


Mkuu Zurri, Mimi sina uadui na wewe na wala sitaki tuwe maadui, jambo lolote utakaloliweka hapa na liwe jema, naapa, nitakupongeza. Kinyume chake kamwe sitakupongeza bali kukuasa kistaarabu. Sisi sote ni wana jamii forum na tupo hapa kuelimishana na kukosoana kistaarabu, anayejua zaidi ni Mungu pekee. Basi tuwe wastaarabu ili tulinde heshima zetu.
 
Nakwambia hivyo kwa sababu wewe ni slowpoke.

Define Mungu ni nini.

Thibitisha yupo.


Sent from my typewriter using Tapatalk
Sawa mie ni slowpoke ila hoja yangu iko palepale kuwa huwezi kudai uthibitisho kwa kitu usichokijua, umewezaje kuona kuna uhitaji wa kutaka uthibitisho wa kitu kabla ya kukijua?
 
Sawa mie ni slowpoke ila hoja yangu iko palepale kuwa huwezi kudai uthibitisho kwa kitu usichokijua, umewezaje kuona kuna uhitaji wa kutaka uthibitisho wa kitu kabla ya kukijua?
Kitu kipi sikijui, na unajuaje sikijui?

Define Mungu ni nini.

Thibitisha yupo.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Kitu kipi sikijui, na unajuaje sikijui?

Sent from my typewriter using Tapatalk
Sijakukusudia wewe binafsi nazungumzia kiujumla kuwa huwezi kudai uthibitisho wa kitu ambacho hujakijua.

Halafu sijajua kwanini unaniambie nithibitishe Mungu!
 
Sijakukusudia wewe binafsi nazungumzia kiujumla kuwa huwezi kudai uthibitisho wa kitu ambacho hujakijua.

Halafu sijajua kwanini unaniambie nithibitishe Mungu!
Wewe kwanza nyoosha Kiswahili chako.

Unapoongelea kiujumla, halafu unarudia tena kuandika "huwezi" kwangu mimi, unaonekana hujui kutumia mantiki na hujui lugha.

Na kama hujui mantiki na lugha, hatuwezi kuelewana.

Kama hunizungumzii mimi binafsi, unazungumzia kiujumla, unachotakiwa kuandika ni "Mtu hatakiwi kudai uthibitisho". Siyo "huwezi kudai uthibitisho".

Unaelewa tofauti?

Sasa nitajadiliana nawe vipi falsafa ya dini wakati hata Kiswahili na mantiki hujui?

Unaelewa tofauti ya kuuliza "May I help you?" na "Can I help you?".

Naona unanipaka shombo la mawazo tu kubishana nawe.

Inawezekana unatakiwa kuoga kiakili kwanza kabla ya kujadiliana nami.

Moron.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Labda ushawahi kuuona uchawi au hujawahi lakini mimi Sijawahi na naamini upoo na watu wote wanaamini upo na wewe ukiwemo. Wewe toka umekuwa umnaamini kuna Hewa lakini kamwe hujawai kuiona so sio kila kitu lazima ukione ili Uamini kipo lakini kaa Ukijua MUNGU YUPO na isingekuwa Mungu leo hii usingekuwa na jeuri ya kuandika ulichoandika.
Mzee kuhusu wachawi mimi siamini na hakuna mtu wa kuniroga mimi..
Kuhusu hewa ambayo kwa kingereza inaitwa air ambayo by definition ni mixture ya gases kama nitrogen , Oxygen na carbondioxide hatuwezi kuiona sababu ni colorless lakini kuna tests za kutest hizo gases na mtu una unakubali kabisa.. na personally nimetengeneza oxygen na nikaitest , nimeshuhudia carbondioxide nikaitest.. sasa unataka ushahidi gani kuhusu hewa.?
 
Back
Top Bottom