Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Ninapofikiria kupost chochote kile huku kwenye jukwaa la mahusiano mara nyingi huwa namfikiria Lizy. Nalazimika kuipitia kazi yangu mpaka mara kumi hata iwe ndogo vipi, sababu ya kufanya yote hayo ni kujiandaa na changamoto ninazoweza kuzipata kutoka kwa Lizy. Duh, yaani huyu dada namuogopa sana labda anikosoe kwa maandishi haya ambayo nimeamua kuandika bila kuyakagua. Yote kwa yote huwa najiuliza huyu dada kama ni mke wa mtu inakuwaje huko kwa mumewe?
Kweli kutongoza ni kazi ngumu huyu jamaa kaanzia mbaali ili dada Lizy am-PM amuondoe woga alafu ile kwake. Dada Lizy jiangalie sana na gia ya huyu jamaa nakumbuka nikiwa chuo nilishawahi kumkamua mtu kwa gia hii hii nilimuambia kwamba namuogopa sana namuona kama ni mkali sana baadaye akaanza kujitahidi kuni-prove wrong kwa ukarimu, then ikala kwake