Leo nimemkuta Posta Mpya, ni mchafu anadandia mabasi. Anawahi siti kupitia madirishani ili wenye kuhitaji siti wampatie ujira wa sh. 500.
Tulikutana naye mwaka 2004 tukiwa form 5.
Tulipendana naye napenzi ya dhati, kama gari na matairi ndivyo tulivyokuwa.
Form six tulipoingia, kuna dada mrembo sana, kwa kuwa boyfriend wangu huyu alikuwa na uwezo sana darasani wasichana wengi wakawa wakimfuata ili awafundishe huku moyoni wakiwa na yao. Miongoni mwa waliokuwa wakimfuata boyfrend wangu ni pamoja na mgeni huyu aliyehamia. Sijui alitumia mbinu gani, akamnyakuwa wangu wa moyo. Nilipigwa kibuti assemble, my boyfriend was head prefect. Akautangazia umma wa wanafunzi kuwa ameniacha. Niliumia sana, nikamwachia Mungu.
Tukiwa kwenye likizo ya kusubiri majibu, nikasikia eti my ex boyfriend kapelekwa jela kwa wizi. Sista duu alikuwa anahitaji mambo makubwa, ambayo ili my ex ayamudu ilimbidi aibe na kukwapua. Bahati mbaya za mwizi arobaini, akakamatwa na kufungwa kifungo cha miaka mitatu. Majibu yakatoka, alikuwa amefaulu vizuri sana, one ya point nne PCB.
Sikuwahi kumuona tena ndio namuona leo akiwa ni teja, hana mbele wala nyuma.
Nyie wasichana wa siku izi kwa umbea na kutunga mmetisha ya kama mdogo wake Shigongo