Namna nilivyonusurika kufa kwenye ajali ya gari, Bongo unakufa huku unajiona

Umemuomba mungu afya njema yeye akakujalia ajali halafu kwa uwezo mshangavu akakuponya na wadau wanamshukuru hapa.
 
Hii ya kusema kung'ang'ania brake ndio imekuvunja mguu ni kweli. Jamaa yangu mmoja nae hivyo hivyo ule mguu ulioshikilia brake baada ya kishindo ukasukumwa juu ukapachuka kwenye hip hapo sema mambo ya hela yakasaidia akaenda India wakamuweka sawa
Bora angeacha asukumiziwe mbele au sio? Ukigongwa tokea nyuma lazma utengeneze opposing force nahisi ndio ilimuumiza zaidi jamaa
 
Hii nchi kwenye huduma bado saaaaana tena sana, hospitali na polisi ni mtihani hasa ukiwa masikini Mungu atusaidie.Pole sana stori yako imenihuzunisha sana japo am happy u r ok
Na awamu hii ndo itakuwa NECTA kabisa maana ni zaidi ya mtihani!
 
Mkuu pole Mimi binafsi nilifiwa na baba mzazi pale reception tulifika akiwa bado mzima na anaongea wakaanza kujadiliana wampokee au raha wakafikia maamuzi yao tushakaa saa moja bila huduma na mzee aliaga dunia hapo nimemlaza mapajani mwangu kisa walihisi ni covid case. RIP father.
Inauma sana yani
 
Pol

Pole ndugu Kwa masaibu.. unashangaa ungetembea speed kubwa Wala usingpata ajali. Maisha ni fumbooo
Eeh mambo ya kuzubaa zubaa barabarani hayo sio mazuri mkuu! Katika kuendesha gari nimejifunza mambo makuu matatu.

1.Kutokukaa nyuma ya boda boda, bajaji wala lorry ama kwa mda mrefu. Huwa nazikimbia kwa namna yeyote ile.

2.Naepuka kuongozana mtu ambaye hana maamuzi katika uendeshaji aidha anafunga funga breki hovyo, hawashi indicators. Huwa nampita kisha nanyoosha kibati mpaka nifike mita kadhaa mbali toka alipo ambapo nakuwa mwenyewe njia nyeupe mbele na nyuma.

3.Kuchukua hatua haraka napoona mbele kuna upumbavu umefanyika ghafla ambao ungenihatarishia kupata ajali. Aidha mtu kachomeka kijinga, au daladala inasimama ghafla mbele yangu n.k au mtu anazubaa wakati taa zimeruhusu!
 
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
Pole sana mkuu.
Hii story yako inasikitisha sana. Kwa bahati mbaya sana, story kama hii watu wengi sana huwa wanapitia, na wengine huishia kufariki. Naiangalia story yako kwa upana zaidi, imeibua mambo kadhaa kwenye fikra zangu...
1.Mfumo wetu wa afya uko vibaya sana kwenye ku "respond" katika ajali... Yaani pale ajali inapotokea; Watanzania wengi hawajui nini cha kufanya baada ya ajali kutokea, na ucheleweshaji huanzia pale. Pia, lingine linaloendana na hili ni watu wengi kutokua na basics za huduma ya kwanza (first aid) vitu kama nini cha kufanya kuzuia au kupunguza damu kuvuja kwa majeruhi, nini cha kufanya kwa majeruhi, na kadhalika. Kuna tafiti nyingi ambazo zimeonyesha karibu asilimia 50 ya vifo vinavyotokana na ajali kwenye nchi za dunia ya tatu,vingeweza kuepukika kama wangepatiwa huduma ya kwanza kwa haraka.
2.Mfumo wetu wa afya una mapungufu makubwa pia kwenye namna ya kuwapokea, na kuwahudumia majeruhi wa ajali kwa uharaka unaostahili... Huu utaratibu unaitwa triaging... Yaani kuweza kujua mgonjwa huyu anahitaji huduma ya haraka, huyu anaweza akasubiri kidogo, yule anatakiwa apate huduma ndani ya lisaa limoja la sivyo atafariki. Hapa ni stage ya pili ambapo ucheleweshaji wa huduma kwa majeruhi wa ajali unatokea, na kupelekea pia vifo zaidi vya majeruhi hata baada ya kufikishwa hospitali; Hili linakwenda sambamba pia na mfumo mbovu wa rufaa ambao pia umeonekana wazi kwenye huu mkasa wako, ambao ulipelekea ucheleweshwaji wa masaa kadhaa kutoka hospitali ya wilaya hadi kufikishwa hospitali ya taifa. Yote haya yanasababisha idadi kubwa ya vifo kutokana na ajali ambavyo vingeweza kabisa kuzuiwa.
3.Uelewa na umahiri wa watoa huduma kwa majeruhi wa ajali-Hili pia limekua wazi kabisa katika mkasa wako, watoa huduma kutojua nini cha kufanya eidha kwa makusudi kabisa (kwa sababu ya kukosa motisha, au kutokujali tu au kutaka rushwa), au saa zingine ni kweli kabisa wanakua hawajui nini wanatakiwa kufanya kwa mgonjwa gani... Kama ambavyo umeshuhudia kuwa ulikuta interns/wanafunzi hapo emergency ambao hawakuonyesha kujali sana, labda kwa sababu ya kukosa muongozo kutoka kwa senior anayeelewa. Je, ni kwa nini emergence pajae wanafunzi/interns bila kuwepo seniors wa kutosha kuwaongoza? Ni kwa sababu ya upungufu wa watoa huduma? Au ni kutokujali tu?

Hizo changamoto tatu hapo juu zinasababisha vifo vingi sana vya majeruhi wa ajali ambao wangeweza kupona. Na hii hali haitabadilika hadi zitakapofanyiwa kazi ipasavyo.
 
Ila umezengua bana, sasa umeshindwa nini
Kutaja jina la hiyo hospitali ndogo na kubwa
ili wenye mamlaka wafahamu uozo uliopo, ingekua imesaidia kiasi fulani. Ila pole sana mzee na Ahimidiwe Mungu aliyekuponya.
Then like kitu kilichokwambia uchukue tahadhari huyo ni Roho Mtakatifu. Siku nyingine usimwite kitu ama machale yakanicheza kama wengine wanavyosema. Sio machale wala kitu ila ni Roho Mtakatifu ambaye hutuongoza.
 
Ila umezengua bana, sasa umeshindwa nini
Kutaja jina la hiyo hospitali ndogo na kubwa
ili wenye mamlaka wafahamu uozo uliopo, ingekua imesaidia kiasi fulani. Ila pole sana mzee na Ahimidiwe Mungu aliyekuponya.
Then like kitu kilichokwambia uchukue tahadhari huyo ni Roho Mtakatifu. Siku nyingine usimwite kitu ama machale yakanicheza kama wengine wanavyosema. Sio machale wala kitu ila ni Roho Mtakatifu ambaye hutuongoza.
HOSPITALI KUBWA YA TAIFA NI IPI KAMA SIO MUHI-2 NA MLOGANZIRLA?
 
Unajiita 666 halafu unasema upo karibu na Mungu.
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
 
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo😂😂, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah 😂😂 aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
Pole sana chifu
 
Ebu wapumzisheni wahudumu wa Afya wanafanya mengi kuokoa Uhai na bahati mbaya huwa hawasifiwi yaani huwezi Kuja ukakuta Uzi hapa Jf unasifia mtoa huduma wa Afya ila wakienda kinyume cha matarajio yenu hamuachi kulaumu, nakuhakikishia kama wangekuwa wabaya kwa Kadri mnavyoelezea wagonjwa mahospitalini wasingepona kabisa! ebu tuwapende na kuwasapoti wanafanya kazi kwenye Mazingira magumu Sana na lakini bado wanajitoa kutuhudumia tuweke matarajio yetu pembeni na tuheshimu professionalism.
Acheni kujitetea! Kama ni hvyo kwann sasa mkipewa hela mnachangamka?, Si mngekuwa mnakataa..ni wachache ndo wapo committed na kazi. Hujiulizi kwann wasisingiziwe wengne ..
 
Huko kwenye wodi za wazazi ni balaa tupu, rushwa nje nje na wala hawaogopi!
 
Hospital ya maana kwa mwanza Ni bugando pekee..yaani Kama una pesa yakutosha au bima utapewa huduma ya kiwango Cha lami..
Watu wa emergency pale bugando Ni watu hodari Sana..mtoto wangu aligongwa na bodaboda..walimtibu kwa viwango vya kimataifa kuanzia emergency Hadi wodini..nilimuona nesi mmoja tu mpuuzi wengine wako vizuri..
Boda ni waseng* Sana,hili tusi siwezi kulitoa imelazimika niliandike hapa, baada ya kusoma mwanao aligongwa na boda,
Kuna siku boda boda mmoja alikuwa amebeba madumu mawili ya petrol Lita 20 alafu Yuko speed,wakati Ana over take bila kuangalia mbele yake akagonga gari yetu na ile pikipiki yake ikaanza kuwaka Moto hapo hapo
 
Back
Top Bottom