Namna nilivyonusurika kufa kwenye ajali ya gari, Bongo unakufa huku unajiona

Chai. Kuna viashiria vingi kuwa hii ni chai. Kwa wale wataalam wanaojua makosa wanaofanya wasimulizi wa ''story chai'' wa Bongo watakubaliana na mimi.
Hatuwezi kukubaliana na wewe hadi utoe uchambuzi wako wa Uzi huu
 
Ebu wapumzisheni wahudumu wa Afya wanafanya mengi kuokoa Uhai na bahati mbaya huwa hawasifiwi yaani huwezi Kuja ukakuta Uzi hapa Jf unasifia mtoa huduma wa Afya ila wakienda kinyume cha matarajio yenu hamuachi kulaumu, nakuhakikishia kama wangekuwa wabaya kwa Kadri mnavyoelezea wagonjwa mahospitalini wasingepona kabisa! ebu tuwapende na kuwasapoti wanafanya kazi kwenye Mazingira magumu Sana na lakini bado wanajitoa kutuhudumia tuweke matarajio yetu pembeni na tuheshimu professionalism.
Sawa muhudumu wa Afya tumekuelewa
 
Afrika ni kama njia panda ya kuzimu...kuna mambo ya kipumbavu sana huwezi imagine kabisa

Watu wengi sana wamepoteza uhai kwa makosa ya makusudi ya wenye walau kuweza okoa maisha ya watu...
Ni vile Kuna watu wamezaliwa familia za kimasikini sana na watoto wengi sana kiasi cha kuoneana wivu na kukosa utu kwenye mioyo yao Sasa huko nje familia inawatoto wachache na wote wanapendana hivyo wakiona familia zingine zinashida wanaonyesha Upendo wao na kama ni huduma wanatoa huduma nzuri za kuokoa uhai kwa moyo wa Upendo.
 
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo😂😂, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah 😂😂 aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
Pole kwa madhira hayo yaliyokukuta!
In short kwa nchi yetu ugonjwa wenye uhakika wa kupona ni UTI ! A little complication unaaga dunia!
Pia gharama za matibabu ni kubwa nimewahi kuishi nchi moja ya kiafrika kwa kweli huduma zao za afya ni sawa na bure unalipa Sh. 50 kumuona na daktar na 250 kununua dawa (dawa aina yoyote) na dawa zinapatikana.kwa gharama hizi zinawavutia wananchi kuwahi mapema pind tu tatizo linapoanza na sio kusubiri hatua za mwisho. Thus why I don’t wonder why they have low mortality rate!
Nilishangaa kwenda muhimbili na kuambiwa kama hauna Bima kumuona daktari tu ni elfu 30 mbali na vipimo na dawa! How many can can afford ?
 
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo😂😂, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah 😂😂 aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
Unaimani thabiti sana kwa Mungu wetu,na naamini ndio imekuponya. "Nyanyuka uende zako,imani yako imekuponya". Ukawe shuhuda kwa mataifa juu yake. Kamwe usiiache kwani Mungu anakusudi kwa kila mmoja wetu.Pole sana mkuu,umesisima imara na sasa songa mbele tena
 
Stori yako umenikumbusha siku ya ajali ya Shemeji yangu,mke wa bro..

Alipata ajali ya gari,aligongwa wakati anavuka barabara pale mwenge mida ya saa 3 usiku
Akakimbizwa hospitali ya rufaa pale karibu na makumbusho..Bila bro kuwahi kufika mkewe angekuta ameeshafariki Kwa jinsi Ile hospitali isivyojali wagonjwa mahututi

Taarifa ilipomfikia bro kwamba mkewe amepata ajali na amekimbizwa pale hospitali ya rufaa,fasta anachukua gari akafika,akauliza mgonjwa aliyepata ajali ya gari aliyeletwa km nusu saa hivi yupo ward gani? Cha ajabu akaonyeshwa alipolazwa.Alikuwa amelazwa Chini sakafuni,damu zinamvuja,taya zimevunjika,ulimi umekatika,kichwa kimeanza kuvimba na wahusika hata hawajali..so sad..bro angechelewa kidogo Tu angemkuta mkewe kwenye fridge..Akampakia kwenye gari fasta akamwaisha muhimbili

Ilikuwa ni ajali mbaya sn.Mgonjwa alipopata fahamu akawa anayakumbuka matukio ya mwaka kipindi wanatongozana na mumewe..matukio ya sasa yote hayakukumbuki Ila ya mwaka2005 kurudi nyuma ndy anayakumbuka,na anakumbuka km matukio yaliyotokea jana Tu au juzi na Sisi wengine hatujui kbs,anauliza kwani hawa ninkina Nani ..ubongo ni wa ajabu sn

Mkuu pole sn Kwa yaliyokukuta,ajali ni mbaya Sana,na km Una moyo mwepesi huwezi kutazama
Poleni sana. Shemeji yako alipata kitu imaitwa "Retrodgrade amnesia". Ni complication ambayo ni common baada ya ajali inayohusisha kichwa.
Hope sasa hivi anaendelea poa.
 
Pale Muhimbili emergence ni ushubwada sana pale wale watoto sijui ni intern wale.
Na kweli wengi ni Samsung na infinix. Zile za zamani.
Kwangu Mimi, nilikula Mzinga mwaka 2017, nikalala Bochi Mwaka na miezi nane? Aisee nilipitia Mengi ila nilipona kwa uwezo wa Mungu. Sikutoka kitandani mwaka na miezi miwili, miezi sita ilikua yakujitoa muhanga.
Nimewahi kutaka kutoroka kitandani, nakutwa nimedondoka chini siwezi rudi kitamdani, nimefanya physical workouts nilinunua vyuma vya gym nikawa napiga kitandani. Mpaka siku niliwezi kuinuka,
Na nilifanikiwa kupiga show in the same 6 months zakujiweka sawa kashori kangu kamoja. Aisee. Hizi ajari, acha tu.
 
Watu wa daladala wa hovyo sana kuna siku hivyohivyo tupo kwenye gari wanashindana karibu na victoria tushafika kabisa safari yetu morroco jamaa mwengine akahama kaja kwetu ilibaki al manusura tupinduke dereva wetu alijitahidi akapeleka kwenye zile sehemu zakati zinazotenganisha upande yani tuliyumba mara 6 Mungu amuweke yule dereva ..Cha ajabu Magari yote kampuni moja 😂
Umeweka emoj ya kucheka itafikia wakati utashindwa kuwe emoj ,Kama abiria mlishindwa nini kushuka kwenda kumtia mbata huyo dereva mpumbavu?
 
Kwema wadau?

Mwaka huu mwanzoni nikiwa nimetoka kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya na nikiwa nimefanya maombi ya mipango yangu mingi kwa mwaka huu na kumsihi sana Mungu wangu aliye hai anijalie afya, uhai, furaha na amani tu mengine nayaweza hayanisumbui kabisa, basi sikuwa najua siku chache zijazo nitakutana na jambo baya na la kutisha kiasi icho.

Siku ya Tukio;

Nikiwa nawahi zangu kwenye majukumu yangu ya kikazi asubuhi kabisa hapa ndani ya Dar es Salaam tena nikiwa sina hofu wala kuwaza lolote, ile wazungu wanaita "the fear of unknown" kwamba kama kuna jambo baya linaenda kutokea basi kuna ishara flani huwa zinakusumbua kama kukosa amani and so, but mie siku hiyo haikuwa hivyo wala na nilikuwa nawaza tu niwahi kufika ofisini.

Ni asubuhi hio nikiwa ktk mwendo wa kawaida kabisa katika chombo private tu, ghafla kitu kikaniambia "be very careful" na nikaitii hii sauti so nikapunguza kabisa mwendo wa chombo changu na nikawa kawaida kabisa, haikupita hata dk 10 mbele yangu nikaona daladala mbili zinafukuzana kuwahiana abiria, kama kawaida yao hawa mabwana na ujinga wao wa kuwawahi abiria wa mbele zao, so hizi daladala hazikuwa upande wangu zilikuwa kulia kwanguwmie nikiwa kushoto so nilikuwa naziona face to face na nikajua kila mtu ni lazima aheshimu sheria za barabara na kukaa upande wake, sasa haikuwa hivi, yule dereva aliyekuwa anapitwa akafanya kumu overtake mwenzake nadhani bila kuangalia na labda atakuwa ni mjinga wa kuzaliwa wa kweli kweli, na ikumbukwe njia ilikuwa imenyooka so nimeanza kuwaona toka ka distance flani hivi mbele yangu wakifanya huo ujinga na haikuchukua hata dakika tatu tangu nianze kuwaona na kuniletea changamoto mbaya sana, yule dereva mwingine wa daladala alie overtake bila kuangalia nadhani ile gari ilimshinda au sijui kama shetani aliingilia kati ila nilishangaa tu kishindo kanigonga face to face wakuu, aisee nilishangaa sana lakini kuja kustuka naona damu zimejaa chini ya gari langu, airbag na watu wanapiga kelele, sikuzimia wala sikuskia maumivu ila nilikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana sana.

Ile gari ilivyonigonga na ilizima pale pale yenyewe tu na kwangu huku sikuona tena ya mbele, nikawa najipapasa nikihofu yasije yakawa mambo ya uti wa mgongo kushtuka na kushindwa kuamka forever, nikajaribu kutikisha miguu naona mguu mmoja haurespond na kama bega linaniuma hivi, sikujua tena nini kimetokea ila mguu ulivunjika, bega kustuka na huu mguu uliovunjika ni tuseme ulikuwa umepasuka na ndo chanzo cha zile damu, na hii baadae nilikuja kujua ni kwamba nilikanyaga break kwa nguvu na kunyoosha mguu kwa kukaza labda kwa kustuka au hofu so gari ilivyopigwa kwa nguvu na kubonyea so presha yake na effect ndo ikaniletea hayo madhara.

Kilichofuata kuanzia hapo ikawa sina sauti tena, naona naamriwa tu vitu na wananchi waliokuwa wamejazana pale, kila mmoja akisema hivi na mwingine akisema vile na wangine wakirekodi kwa simu tukio lile na mie mwenyewe nikiwa bado nna mstuko mkubwa sana nawaza hivi ni mimi au naota? Nikiaskia sauti mkagueni vizuri labda ameumia kichwa?

Nikaskia shauri likiendeshwa juu yangu, wananchi wakasema tumpeleke polisi tukachukue PF3, wakaja kunitoa huku naona watu wameshika vichwa wakina mama wanalia na mie sasa nikaanza kuogopa uende nimeumia sana kuliko ambavyo najiwazia wakati huo, so najaribu kusimama mwenyewe siwezi, wananibeba na wanasema twende polisi, damu kila mahala na huo ni mguu tu, japo nna maumivu ya bega na mkono lakini najishangaa nasema kwa namna damu hizi zinavyotoka huko polisi ntafika nikiwa mzima kweli? Na kwa maeneo hayo kituo cha polisi kipo wapi sasa? Na je kutokea hapo mpaka kufika Hospitali itakuaje? Naona kabisa wananchi hawana elimu juu ya kuzuia damu kutoka na i feel like labda nijisaidie ila siwezi kufanya lolote, moyo unaenda speed sana na bado niko shocked tu.

Polisi hapakuwa mbali na hawakuwa na hiyana, ni kakituo ka dogo hakukuwa na jam ni walinihudumia ndani ya dakika 5 tu nikaipata pf3 tukaondoka na wananchi ambao walikuwa wamenibeba kwenye kirikuu.

So tukaelekea hospitali na hapa ntaomba nisitaje majina ya hospitali wananchi wasije wakaamua kwenda kuzichoma moto, so nikapelekwa hospital ya wilaya, mpaka nafika hospitali hapo nadhani labda nilikuwa nimebakiza damu lita mbili tu nadhani, so jamaa hakuna wanachokifanya, manesi wananitizama tu, nikawa mkali, wakasema wewe mgonjwa unamfokea nani? Daah bongo, akaja muuguzi mmoja akanichoma sindano ya tetenasi na nyingine sijui ni nini, nikamwambia wewe bwana embu fanya kitu kuzuia damu basi, wakaanza kunizuia damu na wakafanikiwa lakini nadhani mpaka muda huo labda nilikua nna lita moja tu mwilini, nikaanza kuskia kabisa moyo unasukuma kitu kisicho kuwepo.

Lakini pale pale najiuliza ina maana nchi hii mtu anaweza kufariki kisa mguu, mkono na bega? how could that be possible? Ila nikajisemea "mimi sitokufa mahala hapa na wakati wangu bado haujafika, ewe Mungu wa haki usinichukue nikiwa katika umri huu nna deni na wewe", sasa Mungu ni muaminifu sana, baada ya kusema maneno hayo nikawa najipa moyo mkuu na imani na japo naskia sina damu na ata kuongea tu tabu, moyo una push kitu kisicho kuwepo, kazi yangu ikawa ni kurudia tu hayo maneno hapo juu, natamani labda nilale niamke nikiwa fresh ila hakuna kitu siwezi ata kusinzia au kuzimia.

Ile hospital ya wilaya wakasema hatuwezi kumtibu, mpelekeni hospital ile ya taifa, na mpaka muda huo hapo kwenye hio hospitali wamenichoma sindano mbili tu, drip ya maji na wakanipa rufaa kwenda kwenye ile hospitali nyingine baba lao.

Mpaka muda huo, wadau wangu washafika so ikabidi tutafute private ambulance sababu hio hospital wanasema ambulance ipo moja na imempeleka mgonjwa mmoja hospital ya taifa so tuisubirie na hapo tumesubiria saa na nusu haiji ndo kufanya maamuzi ya private ambulance.

Kufika kwenye ile hospital baba lao la taifa aisee kumbe bora kule wilayani ambako hawana kitu, wale wako too slow, yaani unawaona kabisa hakuna kitu kinachoweza kuwastua, wamezoea matatizo na kila mtu anapita tu ana shangaa shangaa hivi anaondoka, vijana wadogo ndo wajinga zaidi pale yaani wako sector ya emergence ila wanachezea tu simu ambazo ata ukiziangalia simu zenyewe ni tecno na samsung A series, hakuna humanity, samahani kwa kuyasema haya ila ndo nimeyaona tena emergence kabisa sasa fikiria kule kwengine ndo kupoje?

So wadau wangu wakaanza kutilia mkazo na mikwala mingi ndo na wale kuanza kunihudumia, na kila dakika hapo emergence wanaletwa watu ambao wanalia kila mtu kama anachinjwa hivi.

Sina damu na moyo unapambana sana kwa zaidi ya masaa matano sasa toka tukio litokee, naskia njaa naskia kiu na kama siwezi kupumua vizuri iv yaan nna fosi, ajab sizimii wala sisinzii, so hawa nao wakaniwekea drip za maji, nawaambia wazee nahitaji damu nitoleeni haya ma maji yenu hakuna kitu yanacho nisaidia hapa, wananiambia ngoja tukuchukue vipimo kwanza na tuone, basi wadau wangu waka fosi ki mjini mjini mambo yakaanza kukimbizwa na nini, mpaka naingia chumba cha upasuaji ni masaa 11 yamepita toka nipate ajali na damu kuniisha mwilini.

Basi baadae nikaingia wodini tena na nini, kuanza kupona sasa na nini ila expirience ambayo sio ya kuombea.

Namshukuru Mungu wangu alie mkuu sana, sikufa siku ile na sitarajii kufaa miaka hii hii na amenipa uhai na ataendelea kunipa uhai na tukio hili limeniweka karibu sana na yeye.

Kule wodini na tiba zingine unashangaa wataalam wanakwambia "aah kitu ichi hakiwi covered na bima ya nhif, aah hapa inabidi ulipe kiasi flani, aah kamuone flani" yaan unashangaa jambo dogo lina mlolongo mrefu ambao ni very unnecessary.

Wodini mule wadau wakaanza kunipa habari za namna watu wanavyoteseka na wengine ambao hua wanafia emergence, so scarry wazee. Bongo hauna kitu unaondoka unajiona wakuu, so hata kutafta room private nalo mpaka mchongo eti daah aisee.

Naomba kuishia hapo, nilitoka hospital sikumaliza hata siku saba, nilifosi nikaondoka kibishi tu na kuendelea na tiba tokea nyumbani kwangu na Mungu mwingi wa rehema na neema basi nimepona ndio niko narudi rudi na mimi kwenye majukumu yangu mengine, wale walionosababishia hayo matatizo ndo nataka kuanza kuwashughulikia sasa na sitokuwa na msamaha ktk hili. Lakini sitosahau miezi miwili iliyopita wazee nilikuwa kama niko Ukraine mstari wa mbele pale kumpinga bwana Putin asiendelee na majeshi yake kuichukua Kyiv.

Sijajua wewe umewahi kuyapata yapi au umewahi kuyaona yapi ya kuhusu ajali hizi za barabarani na experience za ma hospital yetu ambayo unaweza uka dead unajiona! Basi itakua vyema ukishare nasi basi tukapata la kujifunza.

Wasalaam.
Pole sana..bongo kifo nje nje..usipo fia kwenye tukio unaweza fia hospitali kwa kuchelewa kupata huduma.

#MaendeleoHayanaChama
 
Pale Muhimbili emergence ni ushubwada sana pale wale watoto sijui ni intern wale.
Na kweli wengi ni Samsung na infinix. Zile za zamani.
Kwangu Mimi, nilikula Mzinga mwaka 2017, nikalala Bochi Mwaka na miezi nane? Aisee nilipitia Mengi ila nilipona kwa uwezo wa Mungu. Sikutoka kitandani mwaka na miezi miwili, miezi sita ilikua yakujitoa muhanga.
Nimewahi kutaka kutoroka kitandani, nakutwa nimedondoka chini siwezi rudi kitamdani, nimefanya physical workouts nilinunua vyuma vya gym nikawa napiga kitandani. Mpaka siku niliwezi kuinuka,
Na nilifanikiwa kupiga show in the same 6 months zakujiweka sawa kashori kangu kamoja. Aisee. Hizi ajari, acha tu.
Doooh mkuu pole sana, story yako nusu inachekesha 😂😂😂 nusu ina ujumbe mzito sana, ilikuaje hio siku ya mzinga na uliumia uti wa mgongo au kichwa maana mwaka na miezi nane sio mchezo mzee.
 
Pole sana..bongo kifo nje nje..usipo fia kwenye tukio unaweza fia hospitali kwa kuchelewa kupata huduma.

#MaendeleoHayanaChama
Very true, ndo mtu mmoja hapo juu akasema "sasa iv bongo tulipaswa kua milion 90 sema hospitali zetu tu ndo zimetuyeyusha".
 
Poleni sana. Shemeji yako alipata kitu imaitwa "Retrodgrade amnesia". Ni complication ambayo ni common baada ya ajali inayohusisha kichwa.
Hope sasa hivi anaendelea poa.
Sorry mkuu, hali hio hua inadumu kwa kipindi cha muda gani?
 
Hii ya kusema kung'ang'ania brake ndio imekuvunja mguu ni kweli. Jamaa yangu mmoja nae hivyo hivyo ule mguu ulioshikilia brake baada ya kishindo ukasukumwa juu ukapachuka kwenye hip hapo sema mambo ya hela yakasaidia akaenda India wakamuweka sawa
Tatizo ile hali hutokea kama tendo automatic kwani tukio ni la ghafla....kila kwenye ajali akili hukimbilia kwenye beki.
 
Pole son.

Na vipi kuhusu gari na vitu vyako ulikuwa navyo kwenye gari.

Hosp wapo wenye roho mmbaya acha tu
 
Aiseh mkuu pole sana.....me nakumbuka kabla ya mwaka mpya....nlikua ndani kwangu nmelala gafla nkasikia kishindo kikubwa nje me naish karibu na barabara.....basi roho inanambia toka nje nkajisogeza mdogo mdogo kufika sehem ya tukio nkaona watu kama watatu mmja ni mwanamke analia kwa uchungu sana.......kumuangalia usoni bwana we nkamjua ni Dem wa mshikaji.......nkaanza kuomba msaada tumsaidie huyo dada....hakuna anaenisikiliza.....ikabid nitafute namba ya mshikaji.... mshikaji akasema ametuma mtu aje.....hapo nishahangaika mno Sina hata mtu wa kunisaidia.....badae akaja traffic ndo kumpeleka huyo dada hospital......kumbe alipasuka figo yule dada akawa amefariki........ nakumbuka hyo siku nlikua na mia 800 ndani ...... nkasema Mungu naomba unipatie maisha mazuri niweze kuwasaidia watu kipindi Cha shida

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
Pole sana mkuu 800 kama 800 dah maisha haya yani
 
Pole Mkuu.Ila story yako haijasaidia chochote. Hukutakiwa kuficha jina la hiyo hospitali uliyoanzia. Laiti kama ungeitaja hapa hakika ungekuwa umesaidia wengi sana. Naamimi wahusika wangejiona hapa wangeshikwa na mshipa wa aibu wangejirekebisha, aidha mamlaka za juu zingewakemea. Ungekuwa umeokoa uhai wa watu wengiHukutakiwa kuficha. Unaogopa nini?
 
Back
Top Bottom