Zunguka duniani kote!
Biashara ya ukahaba ipo tangu enzi za mitume!
Hata Yesu mwenyewe katika pitapita zake mtaani Aliwahi kukutana na kisa Cha kahaba! , Ni pale kahaba alipo busu miguu ya Yesu na kumfuta kwa nywele zake,...Ni pale alipowaambia wale sungusungu
...."Ambae hajawahi kutenda dhambi awe wa kwanza kumipiga jiwe mwanamke huyu....
Hivyo kahaba walikuwapo na wataendelea kuwapo!
TATIZO
Tatizo halipo kwenye ukahaba wao, Bali lipo kwenye Eneo ambalo wanafanyia ukahaba wao ambako Ni machoni pa watu (jamii!)
Hivyo makahaba endapo kama Wizara ya Afya ingeweza kuwapa semina elekezi na kuwapatia leseni ya namna ya kutafta faragha au watengewe maeneo maalum (mfano; ghorofa ya juu ya majengo malefu, Soko maalum ambapo hakuna mwingiliano wa makazi ya watu (mfano Majengo ya machinga complex kule gorofani wapangishwe). hii itasaidia Sana kutokomeza madhara!!
Biashara ya ukahaba inasaidia wengi Sana tukianza kutajana humu hapatatosha!
Yamkini hata anaemkamata kahaba nae anaweza pewa rushwa ya papa! akatulia.
Ukahaba ni fursa Kama fursa zingine ALMRADI hawaibi Cha mtu!
NINI KIFANYIKE
Makahaba Ni waungwana Sana wataftiwe sehemu maalum walipe Kodi, Ingewezekana Manispaa za majiji kote nchini Yale Majengo yasiyotumika mnaweza kuyafanya kuwa eneo maalum Kwa kuweka viwango mbalimbali vya makahaba wenye leseni level, kwanza pale langoni watu wataingia kwa kuponi, pili mtapata Kodi ya leseni za makahaba mliowasajili!
Hivyo ndivyo wanavyofanya huko Duniani!
Ukiona Jambo linawateja tambua Kuna shida!