Nalivua pendo...

Nalivua pendo...

...😀 hapo kwenye wekundu Mj'1, wewe si wa kwanza kulitamka hilo wala si wa mwisho. Nishawasikia wanawake wengi wakiyatamka hayo kipindi cha misukosuko, na wengine wachache hata baada ya kuachana na wenzi wao...

Tatizo kila mwanaume (wa kisasa) utayekutana naye ana sifa hizo hizo za 'yai bichi'. Maovu ya mtu ni mwonekano wa tabia za nje, ambapo wewe ukiwa ni dereva wa mawazo yako una hiari ukwepe au uparamie.

Fikiria wewe ni dereva na mbele kuna shimo, ...Ukilikwepa hutaliumiza gari lako, ukiliparamia unajiumiza mwenyewe ilhali shimo linabakia pale pale. Mwache na 'kilema chake', huwezi kumtibu.

Chukulia mazuri yake (uliyompendea) yafunike hicho kilema.

Siyo nia yangu kumfanya aonekane mbaya (of which sitaki kuamini ni mbaya) but hata yale niliyompendea hapo mwanzo yamefunikwa. Nilikuwa nampenda alivyoweza kunichekesha kunifurahisha kwa matani yake ila sasa siyapati kwani hata kukusemesha ni tabu.

- Nilimpenda kwa kile nilichodhania ni caring yake- kumbe alikuwa ananibembeleza tu niingie kumi nanane- alishaacha kitambo na badala yake yote nikawa nafanya mimi- kubembeleza mimi, vijizawadi mimi n.k.

Sijui ngoja nivumilie pengine atabadilika !!
 
Aksante Mbu maneno yako mazito ila duh ngoja nijaribu maana sina tena nguvu wala uvumilivu.

Nitawezaje kuondoa dhana hiyo wakati unaona kabisa dharau na chuki usoni kwa mwenza? au na haya ni dhana? Mwenzangu huyu haoni vibaya kukwambia 'you know everything that is happening is because of YOU' au unajua wewe ni mfitini ? to me kwa kweli sidhani kama nawezamshutumu mpenzi wangu so direct naona hii- Blaming everything kwake?? tena macho makavu hata kama ninauhakika there is no truth about it?

Ntajaribu Mbu. Nitafuata ushauri wako!

...😀 ngoja nikupe siri, hata ningekuwa mimi katika nafasi yako sasa ningekuwa sina nguvu. I empathize with you Mj1. lakini kiukweli, hayo yote unayoyaona sasa, hata kama utakuwa na mume mpaka kuzikana ipo siku atakuonyesha makucha yake hivyo hivyo!

Hiyo sura ya ndita, majibu makali ya mkato, blames na aggressions zote ni matokeo na mkusanyiko wa hisia za binaadamu ambaye kashindwa kabisa kufikisha ujumbe wako kwako kwa njia nyingine.

Back off!...

Give him a chance to calm down...

japo ni ngumu, usimuonyeshe "ume panic!", usimuonyeshe umenyong'onyea saaana, ... mpe nafasi.... mwanaume anahitaji nafasi kurudisha 'adrenaline' levels zake kwenye hali ya kawaida... mpe nafasi nyingine...

Nakuhakikishia, akisha calm down, hata kama atajifanyisha hataki kuongea (kwa aibu zake), mtaweza kuongea kwa kituo 'palipita shetani gani'...

Mpe muda mwanaume, atapokuwa kwenye hali ya kawaida (as if hakuna lililotokea) ndipo hapo itapokuwa zamu yako kumweleza kero na maamuzi yote yaliyo ndani ya moyo wako!...utaona kama hatakupigia magoti kukuomba msamaha.

Ikiwezekana chukua likizo fupi uende mbali na hapo ulipo ili kumpa muda wa kutulia! Mpe muda wa kutulia ndipo ufikishe kwake uamuzi wako.
 
...😀 ngoja nikupe siri, hata ningekuwa mimi katika nafasi yako sasa ningekuwa sina nguvu. I empathize with you Mj1. lakini kiukweli, hayo yote unayoyaona sasa, hata kama utakuwa na mume mpaka kuzikana ipo siku atakuonyesha makucha yake hivyo hivyo!

Hiyo sura ya ndita, majibu makali ya mkato, blames na aggressions zote ni matokeo na mkusanyiko wa hisia za binaadamu ambaye kashindwa kabisa kufikisha ujumbe wako kwako kwa njia nyingine.

Back off!...

Give him a chance to calm down...

japo ni ngumu, usimuonyeshe "ume panic!", usimuonyeshe umenyong'onyea saaana, ... mpe nafasi.... mwanaume anahitaji nafasi kurudisha 'adrenaline' levels zake kwenye hali ya kawaida... mpe nafasi nyingine...

Nakuhakikishia, akisha calm down, hata kama atajifanyisha hataki kuongea (kwa aibu zake), mtaweza kuongea kwa kituo 'palipita shetani gani'...

Mpe muda mwanaume, atapokuwa kwenye hali ya kawaida (as if hakuna lililotokea) ndipo hapo itapokuwa zamu yako kumweleza kero na maamuzi yote yaliyo ndani ya moyo wako!...utaona kama hatakupigia magoti kukuomba msamaha.

Ikiwezekana chukua likizo fupi uende mbali na hapo ulipo ili kumpa muda wa kutulia! Mpe muda wa kutulia ndipo ufikishe kwake uamuzi wako.

....................Mbu this is a resource kwa kweli. Yaani maneno yako yamenifanya nijione kama ni mtu mwenye kukata tamaa upesi but ukweli ni kuwa he is anotehr person kwa kweli (sijui inawezekana namjudge vibaya but nikilinganisha na hayo niliyoyavumilia huko nyuma dah. aksante nitajitahidi kuyafuata ulinishauri

Naomba niprint!......... teh teh
 
Siyo nia yangu kumfanya aonekane mbaya (of which sitaki kuamini ni mbaya) but hata yale niliyompendea hapo mwanzo yamefunikwa. Nilikuwa nampenda alivyoweza kunichekesha kunifurahisha kwa matani yake ila sasa siyapati kwani hata kukusemesha ni tabu.

- Nilimpenda kwa kile nilichodhania ni caring yake- kumbe alikuwa ananibembeleza tu niingie kumi nanane- alishaacha kitambo na badala yake yote nikawa nafanya mimi- kubembeleza mimi, vijizawadi mimi n.k.

Sijui ngoja nivumilie pengine atabadilika !!

No no no!

sio suala la kusubiri, ni suala la kumkumbusha WAJIBU WAKE! ni haki yako yeye kukufurahisha, kukujali na yote hayo. Mkumbushe kwamba hayo ndiyo yaliyowaweka pamoja mpaka leo,.... Mwambie ni wajibu wenu kujenga kwa pamoja, si wewe pekee, wala si yeye pekee...

Kumbuka huyu shemeji yangu unayemsema hapa naye akiulizwa upande wake kuna kero zake kuhusu wewe zitazokuwa zinamsumbua. Ndio maana kuna mahala umesema, yeye husema " you know everything that is happening is because of YOU' au unajua wewe ni mfitini ?"... kwanini anayasema hayo? Unajua kwanini anayasema hayo? kama huyajui, umechukua hatua gani kuyajua na kuyatafutia ufumbuzi? ...Ndio maana nakwambia maisha ya pamoja yanahitaji effective communication,...

mmoja asikilize wakati mwingine akiongea, akishamaliza nawe uongee naye asikilize,...hivyo hivyo mpaka mtapoweza kuelewana kila mmoja anamaana gani katika ujumbe wake. Hakuna mkamilifu, ...ni jukumu lenu kuletesha ukamilifu katika maisha yenu.

Katika msuko suko huu pia ni vyema ukamtanguliza Mw'Mungu,.... soma vitabu vyake, simamisha ibada, YEYE atakupatia nuru... usikubali kurubuniwa na Shetani katika wakati huu wenye upweke na udhaifu wa roho.
 
Kulala sasa inakuwaje mzungu wa nne nini?

...ha ha ha,...acha uchokozi bana 😀 ...halafu hiyo location yako unasema uvunguni duuuh! hakuna mbu huko?
 
[/COLOR]


sasa huyo x kama alikuona wa maana sana kwanini hakukununua jumla? mambo ya kwenda mbele na kurudi nyuma c mazuri, huwaga nawashauri ma rnds zangu kama umeamua kufanya kitu ufanye bila kujutia baadae, ndio kama hapo MJO aamua kuchukua maamuzi mengine afanye bila kugeuka nyuma na awe ameridhika kutoka rohoni sio afanye huku rohoni anaumia hiyo itam cost, sipo haya mambo ya kusema "kujikumbushia" hayatakiwi kupewa nafac.

Nimekuelewa dada. Thank you
 
kumbe kuna wanume wapuuzi saana dunia hii? nina uhakika mwajamiione ni shori mkali ila jamaa anachezea bahati....najua una maumivu hebu vumilia kidogo sali sana muombe muumba wako aliondoe hili shetwaini.......

NB:muangalia sana fidel80 anaonekana anataka kuchukua substution....kaa nae mbali.....
 
kumbe kuna wanume wapuuzi saana dunia hii? nina uhakika mwajamiione ni shori mkali ila jamaa anachezea bahati....najua una maumivu hebu vumilia kidogo sali sana muombe muumba wako aliondoe hili shetwaini.......

NB:muangalia sana fidel80 anaonekana anataka kuchukua substution....kaa nae mbali.....

Mpwa usimtupie lawama huyu jamaa, maana ujasikiliza kwa upande wake,umesikiliza upande mmoja tu.Unajua wanawake nao saa nyingine wanakuwa na mambo ya ajabu ajabu sana ambayo mwanaume huwezi kuyavumilia.

Pia na muona Mwanajamii ni mlalamishi sana,kila tatizo linalotokea ndani ya ndoa yake,badala ya kulisort out na mumewe ana anakuja hapa na kudai analivua pendo da*n******** mwanamke unapaswa kuwa mvumilivu.
 
Last edited:
Pia na muona Mwanajamii ni mlalamishi sana,kila tatizo linalotokea ndani ya ndoa yake,badala ya kulisort out na mumewe ana anakuja hapa na kudai analivua pendo da*n******** mwanamke unapaswa kuwa mvumilivu.
labda.....maana naona thread zake zinalalamika tuu.....
ingekuwa vema kama akini PM nimuulize baadhi ya maswali kabla ya kumshauri...sidhani kama mwanaume kweli afikie kusema maneno kama hayo bila mwanajamiione ku play part kuleta mfakano.....
 
Mwanaume akisema hadhani kama kuna future kati yenu, he mean it!! Kasema hivyo au ka-imply hivyo? Inawezekana ume overeact kutokana na situation ilivyokuja. Lakini kama kasema, najua hilo liko moyoni. Kuna wengine husema hivyo tu ili kulazimisha kitu fulani.

From yoote niliyosoma, MJ1 ni typical woman. Wanawake wengi wako hivyo na hudhani kuwa they are doing too much to keep the relationship. Hawaangalii the fact kuwa mwanaume anawekeza zaidi materially na morally.

Kuwa fair kwako mwenyewe na kuwa fair kwake. Hivi wewe huna makosa? Haiwezekani mtoto wa kiume azuke tu na kusema hana future na wewe. You must be sucking him dry! Kutokana na jinsi ulivyoeleza hapa anaonekana ni mtu mstaarabu ambaye hawezi kukufanyia uovu bila sababu.

Simtetei, lakini kabla ya kurusha mkuki ni lazima ujue unauelekeza wapi. Mapenzi is never smooth. Lakini vile vile too late is bad. Watu huwa wanapata uchizi kutokana na kung'ang'ania penzi lililokwisha.

Narudia kule mwanzoni, tafuta muda uliotulia uconfirm kama he meant what he said. If he mean it, take your time na usianze kubembeleza. He may be tired as well as you are.
 
kabla sijaoa nilikuwa nafikiri naijua ndoa sana baada ya kuoa mpwa na ile miezi ya honey moon kupita,mpwa nikagundua sijui kitu na nikahisi ninahitaji kurudi darasani.

Hili neno!
Hakuna bingwa wa mahusiano ( yawe ya ndoa au mapenzi)asikudanganye mtu!

Mahusiano huenda yakibadilika kila kukicha kwa maana hayagandi - kuna factors nyingi ambazo huchangia kuwabadilisha wanandoa na kufanya mahusiano kukomaa au kulegalega.Sidhani kuzianisha hixo sababu hapa zitamsaidia MJ1 kwa sasa.

Wanaodumu kwenye ndoa miaka mingi ni ama wale walioamua kukomaa humohumo ndani, au walioamua kuji adjust na ku fit kwenye hali mpya zinazojitokeza au waliojitafutia upenyo wa kuwa na maisha mbadala kufidia mapungufu ( kujikita kwenye kazi/biashara/dini au imani zao na kupuuza mwenza, kuwa na mpenzi wa pembani, kujikita katika kushikamana na watoto, wakwe n,k).Kila mkakati una gharama zake hivyo siwezi kusema ni mkakati upi ni bora.

Mj1 pole sana kwa yaliyokukuta na Mungu atakusaidia utapata ufumbuzi.
 
kumbe kuna wanume wapuuzi saana dunia hii? nina uhakika mwajamiione ni shori mkali ila jamaa anachezea bahati....najua una maumivu hebu vumilia kidogo sali sana muombe muumba wako aliondoe hili shetwaini.......

NB:muangalia sana fidel80 anaonekana anataka kuchukua substution....kaa nae mbali.....
Yo Yo aksante kwa ushauri

siwezisema ni mpuuzi ila ninaamini kuwa anajua anachokifanya. Hata kama ningekuwa mbaya kiasi gani sidhani kama anayo haki ya kuchezea moyo wangu ambao nilimpa kwa hiari nikiamini kuwa atautunza. Amesahau kuwa moyo u nyama ukioza umeoza!

Fidel namwelewa!
 
Mpwa usimtupie lawama huyu jamaa, maana ujasikiliza kwa upande wake,umesikiliza upande mmoja tu.Unajua wanawake nao saa nyingine wanakuwa na mambo ya ajabu ajabu sana ambayo mwanaume huwezi kuyavumilia.

JosM nakubaliana nawe kabisa na ndio maana kama umenisoma vizuri nimesema kabisa kuwa inawezekana nami ninayo makosa yangu but nitayajuaje kama haniambii? Besides bado mimi ninaamini maneno hayo aliyoyasema ni mazito sana kuyasema kwenye relationship no matter what isipokuwa tu pale kwenye makosa ambayo ni obvious yamekuwa yakijirudia na mkosaji kukanywa pasipo kujirudi of which sikumbuki mimi kumfanyia kosa la namna hiyo.

Inawezekana ninapomkalia kimya anaponirudia asubuhi (bila kuonyesha hasira wala kumwuliza) ndio kosa. Ninatamani ningeweza kumleta hapa naye azungumze upande wake na nina uhakika kama akiamua kuwa mkweli mbele ya MUNGU wake he has nothing absolutely nothing against me!


Pia na muona Mwanajamii ni mlalamishi sana,kila tatizo linalotokea ndani ya ndoa yake,badala ya kulisort out na mumewe ana anakuja hapa na kudai analivua pendo da*n******** mwanamke unapaswa kuwa mvumilivu.

Ninashukuru ndugu yangu na ninaheshimu ushauri wako. Pengine ni kweli niko hivyo ila ukweli ninaujua mimi mwenyewe. Sijui mwenzangu ingekuwa wewe tatizo linatokea unapoamua kulizungumza na mwenzako kisha mwenzio anakaa kimya tu bila kukujibu lolote utalichukuliaje besides the moment utakaposema uzungumze naye yeye anaona kama unamshutumu na hivyo kuzua ugomvi mwingine? Unafanyaje JosM.

To me inakuwa rahisi kuja na kulalamika hapa kwa sababu nakuwa huru kuyasema yaliyomo ndani mwangu na vivuli ninyi but honestly hakuna hata ndugu, rafiki anayejua nina matatizo! (Ningekuwa mlalamishi nafikiri hata hawa wangekuwa weshanichoka!!
 
Mwanaume akisema hadhani kama kuna future kati yenu, he mean it!! Kasema hivyo au ka-imply hivyo? Inawezekana ume overeact kutokana na situation ilivyokuja. Lakini kama kasema, najua hilo liko moyoni. Kuna wengine husema hivyo tu ili kulazimisha kitu fulani.

KipimaPembe aksante kwa angalizo but naelewa tofauti ya kuimply na kusema. Those were the words which came out of his mouth tena I asked him mara mbili akanijibu Boldly yes nimesema hiyo!

From yoote niliyosoma, MJ1 ni typical woman. Wanawake wengi wako hivyo na hudhani kuwa they are doing too much to keep the relationship. Hawaangalii the fact kuwa mwanaume anawekeza zaidi materially na morally.

Kuwa fair kwako mwenyewe na kuwa fair kwake. Hivi wewe huna makosa? Haiwezekani mtoto wa kiume azuke tu na kusema hana future na wewe. You must be sucking him dry! Kutokana na jinsi ulivyoeleza hapa anaonekana ni mtu mstaarabu ambaye hawezi kukufanyia uovu bila sababu.

Simtetei, lakini kabla ya kurusha mkuki ni lazima ujue unauelekeza wapi. Mapenzi is never smooth. Lakini vile vile too late is bad. Watu huwa wanapata uchizi kutokana na kung'ang'ania penzi lililokwisha.

Narudia kule mwanzoni, tafuta muda uliotulia uconfirm kama he meant what he said. If he mean it, take your time na usianze kubembeleza. He may be tired as well as you are.

Being fair nakubali na ndio maana nimesema inawezekana am the one with makosa (ambayo siyatambui) but is that a way ya kumwambia mpenzi wako ili kumrekebisha? If it is then yes am mlalamishi na msumbufu.

Ninaamini hivyo pia kuwa huyu ni mstaarabu ambaye hawezinifanyia uovu but maumivu niyapatayo kila mara yananifanya niamini vingine! Kama penzi limekwisha inakuwaje anashindwa kusema zaidi ya kuumizana mioyo?

Samahanini ndugu zangu najua mnawezafikiria mengi but kwa kweli ni MUNGU mwenyewe ndiye anayejua kinachoendelea.
 
NB:muangalia sana fidel80 anaonekana anataka kuchukua substution....kaa nae mbali.....

Mkuu umesahau ukisusa wenzio twala.
Ganda la mua la jana......chungu kaona kivuno.
 
KipimaPembe aksante kwa angalizo but naelewa tofauti ya kuimply na kusema. Those were the words which came out of his mouth tena I asked him mara mbili akanijibu Boldly yes nimesema hiyo!


Being fair nakubali na ndio maana nimesema inawezekana am the one with makosa (ambayo siyatambui) but is that a way ya kumwambia mpenzi wako ili kumrekebisha? If it is then yes am mlalamishi na msumbufu.

Ninaamini hivyo pia kuwa huyu ni mstaarabu ambaye hawezinifanyia uovu but maumivu niyapatayo kila mara yananifanya niamini vingine! Kama penzi limekwisha inakuwaje anashindwa kusema zaidi ya kuumizana mioyo?

Samahanini ndugu zangu najua mnawezafikiria mengi but kwa kweli ni MUNGU mwenyewe ndiye anayejua kinachoendelea.


pole sana mami, lakini naona kama umeshakata tamaa kabisa,yaani unatakiwa uwe strong mami, haya mbona majaribu tu na mie sioni kama unalalama naona we ni mwanamke mwenye roho ndogo(unaumia sana kwa lolote likienda tofauti) unatakiwa kuparangana,mie wangu alivyoanza hiyo tabia iliniumiza mara ya kwanza baaadae nikakaza roho, amerudi/hajarudi cjali/culizi lolote, na alijirekebisha mwenyewe, sasa mami nadhani wewe kuwa na roho ngumu ndio kumekushinda, wakati mwingine inabidi aisee mana utandelea kuumia na kuumia.
 
well mummy pole sana na imani utakuwa unawakilisha wanawake wengi tu kuliko unavyofikiria mimi mwneyewe niko kwenye ndoa mummy but will tel u one thing.
KILA WANANDOA WANA MATATIZO YAO YA AINA YA KIPEKEE AU YANOYAFANANA NA NDOA ZINGINE lakini jinsi ya kuyatatua hakuna kanuni kila mmoja ana njia zake ila matokeo tu ndio yanayofanana aidha kuachana au kusonga mbele.
Pili may b am not a good adviser, bcoz for me my happiness kwanza kabla ya kitu chochote not even a child.kwa maneno mengine ni kwamba siwezi teseka kwa mume wangu nikavumilia kashfa na manyanyaso kisa eti tuna watoto tukiachana watateseka, but at the same time watu wanasahau pia watoto kuwa kwenye nyumba ambayo haina furaha ni wanateseka pia kwasababu wazazi saa zote wanakuwa kwenye moods mbaya.
mummy life is too short na miaka hairudi nyuma darlin inakwenda mbele na ndivyo unavyozidi kuzeeka , yanini yeye ale raha na huyo kishanshuda anayempa raha wewe ndo uteseke? bibi angalia hamsini zako na ukiwa unatafakari hilo weka furaha yako mbele kwanza kuliko chochote.
najua mtaniiita 'selfish' niiiteni tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom