Kibanda
Platinum Member
- Aug 27, 2009
- 87
- 45
Mkuu Kibanda, maandiko yako mengi makali makali nimekuwa siyapendi na yamekuwa yakinifanya niumie sana. Maandiko ya baadhi ya wengine pia yameniumiza zaidi kwa kuwa yamezidi kutia moto kwenye petroli, lakini maneno hayo hapo juu yamenipa faraja kubwa na yanahitaji KUFANYIWA KAZI na sote humu JF. Bahati mbaya kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu (mawasiliano duni) nakosa nguvu ya kujadili kwa uzito unaostahili.
Ndugu yangu Halisi moto ni upi na petroli ni ipi? Hivi Nimesoma sana na kukaa kimya muda mrefu wakati watu wakiweka thread zenye majina yetu. Kimsingi nimesikia ushauri wako ulionipa kwa maandishi na kwa mdomo. Kila ninapoamua kuchangia nafanya hivyo nikitumia maneno laini. Hata hivyo upo wakati wa jiwe kuitwa jiwe badala ya kumung'unya maneno.
Niko tayari kupokea tuhuma za kweli na kimsingi niko tayari kuomba radhi hata katika mambo yangu ambayo pengine yanawakera Watanzania wenzangu wanaoipenda nchi yao kwa dhati.
Tuache wenye hoja za kweli wazitoe hata kama kwa kufanya hivyo tutaumizwa. Siwezi nikawa mtu wa kufanya uchambuzi katika gazeti halafu nikawa mwoga wa bakora. Maji nimeyavulia nguo sina budi kuyaoga.
Hata hivyo siko tayari kuona watu wanajaribu kuosha wenzao kwa maji taka halafu Halisi ukategemea mimi nikae kimya kwani hata Mzee Sitta ambaye aliwaasa wanasiasa kuwa na ngozi ngumu, yalipomfika yeye mwenyewe aliweka kando kijikanuni chake hicho na kuamua kupambana. Huo ndiyo ukweli. Nimeshindwa kuisoma private msg yako kwangu. Haikufunguka.