Naliona anguko la Kibanda

Kibanda,
Mkuu wangu nikuulize.. wewe unasema ni mwandishi wa habari au sio? inakuwaje wewe huyo huyo unakuwa mtetezi wa Mnyika na Mrema dhidi ya Zitto wakati sidhani kama unaelewa hisia za hao watu.
Kama mwandishi mzuri kwa nini suikimbilie kwa Mnyika na Mrema ukawasikiliza wao wenyewe wanasema nini badala ya wewe mkuu wangu kuendeleza tungo zako ambao hazimsaidii mtu yeyote yule. Mkuu enough! unachosha sana yaani kama mimi ningekuwa Mbowe au mhariri wa Daima basi huna kazi!..
Reporter siku zote huandika maelezo ya watu na sio yake yeye kwa jinsi anavyojishirikisha ktk scandal kisha anakuwa mwandishi.. Haya ni matumizi mabaya sana ya madaraka sawa na Fisadi ambaye anatumia vibaya madaraka yake. Kama wewe ni mwandishi bakia kuwa mwandishi na kama unaandika kama Kibanda zungumza kama Kibanda mpinzani wa Zitto na ukubali kukosolewa pia.


Ameshatupiwa tusenti na vijisenti huyo!! Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni!!

Si unajua wakati wa mavuno kwa waandishi makanjanja uchwara unaingia na kwa wale editors wanaotumikia mafisadi badala ya waajiri wao na jamii inayoiandikia??? Naona campaign za mwaka 2010 zimeanza mapema sana!!!
 
Do you know Rostam Aziz effect in Tanzanian politics???? Do you know that at one time Zitto Kabwe wanted and supported the Government to buy the famous dilapidated Richmond Generators?? Huyu Kibanda amekuwa pia upande wa Raostam siku zote hasa wakati ule wa Mafisadi Papa Vs mafisadi Nyangumi!! I cant rule out kama wote hawako kwenye pay roll ya Fisadi Rostam. Rostam is something else in this country because he is a King maker. If he sponsored Riala Odinga duiring the 2007 election campaigns in Kenya, atashindwaje kumsaidia Zitto kwenye uchaguzi wa Chadema. Rostam effect is beyond imagination kwa kuwa Kibanda ni Kibaraka wake kama walivyo viongozi wengi wa nchi hii. jakaya Kikwete, Yusuph Makamba,Ibrahim Lipumba, Mbatia, Augostine Mrema and Christopher Mtikila can not deny this!!! wote hawa wako mfukoni kwa bwana mkubwa Rostam. Ukikosea ukamgusa Rostam, hawa wote pamoja na vibaraka wake watakushughulikia na lazima utamwomba radhi tu!!! Kibanda na Zitto kabwe wanaendeleza njaa tu ya watanzania!!!!!! Mimi naliona zaidi anguko la Watanzania kuliko hili la Kibanda na Zitto.
 
MzeePunch sina sababu hata moja ya kumshambulia Spika Sitta. Siku zote nimeepuka kushambulia watu. Kama mwandishi naandika makala za kukosoa ambazo kwa wengi tafsiri yake imekuwa ni kushambulia. Labda nielezwe tofauti ya 'criticism' (ukosoaji) and 'attacking' (kushambulia).

Nimeruhusu kuchapwa kwa makala za watu waliokuwa wakimkosoa Sitta nikiamini kwamba wanafanya hivyo kutimiza wajibu wao. Ni bahati mbaya sana kwamba kumbe sikujua kwamba Sitta alikuwa na anaendelea kuwa mtu anayepaswa kusifiwa kila siku na si kuguswa na mashabiki wake wakatokea kupinga makala zile.

Makala zile zilipoendelea, na habari mbili au tatu zikaandikwa na waandishi wa habari dhidi ya Sitta, basi spika huyo akaibuka bungeni na kulitaja Tanzania Daima kuwa moja ya magazeti yanayotuhumiwa kumchafua.

Baada ya tuhuma hizo dhidi ya Tanzania Daima nikaandika makala ya kumjibu spika nikikosoa utamaduni wa kudhani kwamba watu huwa hawawezi kuandika fikra zao pasipo kutumiwa. Ugonjwa huu wa kutilia shaka kila jambo badala ya kufikiri umekuwa ukininyima raha sana.

Majibu yangu ya kumshangaa Sitta ndiyo yakawapa makuwadi wa mwanasiasa huyo na wale wanaodai wanapambana na ufisadi mlango wa kusema eti ninamshambulia spika.


Nashukuru kwa ufafanuzi Kibanda. Wewe ni mpiganaji shupavu. Tafadhali sana usikubali kununuliwa na mafisadi. Baada ya shutuma za hapa na pale nilianza kuhofu kwamba tumeshakupoteza mpiganaji muhimu! Lakini mwangalie sana huyo kijana wako aitwaye Mulinda. Kuna tuhuma nyingi dhidi yake, zisije zikaliharibia sifa gazeti letu tulipendalo - Tanzania Daima.
 
Nashukuru kwa ufafanuzi Kibanda. Wewe ni mpiganaji shupavu. Tafadhali sana usikubali kununuliwa na mafisadi. Baada ya shutuma za hapa na pale nilianza kuhofu kwamba tumeshakupoteza mpiganaji muhimu! Lakini mwangalie sana huyo kijana wako aitwaye Mulinda. Kuna tuhuma nyingi dhidi yake, zisije zikaliharibia sifa gazeti letu tulipendalo - Tanzania Daima.
Kibanda ni Mwandishi makini sana siyo mtu wa kununuliwa kama walivyo wengine. Wote misimamo yako tunaiona kabisa
 
Kibanda ni Mwandishi makini sana siyo mtu wa kununuliwa kama walivyo wengine. Wote misimamo yako tunaiona kabisa

Thanks Josh,

Lakini je ni sahihi kuweka their dirty laundry za CHADEMA humu jamvini kwa namna aliyoweka??
 
Jamani,

Hivi Hayati Nyerere aliposhinikiza Jina la John litolewe ama la anarudi Butiama, si ilipita? Na je Dr. Mohamed Gharib Bilal alipoambiwa ajitoe kunusuru chama si ilipita? Why Chadema? Kwani ndio wa Kwanza?

Kumbukeni maneno ya Raila Odinga siku walipotiliana mkaataba wa kugawana madaraka na Rais Mwai Kibaki, "It comes a time when Kenya is the most important thing than Raila or Kibaki".

Kuna wakati maslahi ya Chama au Taifa au Jumuiya fulani ni muhimu kuliko mimi na wewe. Sasa hii ya Kumsakama Kibanda eti kamumaliza Zito Kabwe ni Kushindwa kuone mbali na kujikita katika Siasa uchwara za Rose Garden, Tamali Bar na Lumumba.

Binafsi nilisoma makala ya Kibanda kuhusu Zito, ilijaa hoja za msingi sana wala haikuwa ya kumtukana au kumdhalilisha. Tukubali kuambiwa ukweli na inapotokea, tusidhani eti fulani kalipwa au la. Kwani nyie mnaotoa maoni yenu humu mumelipwa na mtu? Si kweli.
 
Jamani,

Hivi Hayati Nyerere aliposhinikiza Jina la John litolewe ama la anarudi Butiama, si ilipita? Na je Dr. Mohamed Gharib Bilal alipoambiwa ajitoe kunusuru chama si ilipita? Why Chadema? Kwani ndio wa Kwanza?

Kumbukeni maneno ya Raila Odinga siku walipotiliana mkaataba wa kugawana madaraka na Rais Mwai Kibaki, "It comes a time when Kenya is the most important thing than Raila or Kibaki".

Kuna wakati maslahi ya Chama au Taifa au Jumuiya fulani ni muhimu kuliko mimi na wewe. Sasa hii ya Kumsakama Kibanda eti kamumaliza Zito Kabwe ni Kushindwa kuone mbali na kujikita katika Siasa uchwara za Rose Garden, Tamali Bar na Lumumba.

Binafsi nilisoma makala ya Kibanda kuhusu Zito, ilijaa hoja za msingi sana wala haikuwa ya kumtukana au kumdhalilisha. Tukubali kuambiwa ukweli na inapotokea, tusidhani eti fulani kalipwa au la. Kwani nyie mnaotoa maoni yenu humu mumelipwa na mtu? Si kweli.

Ungesoma maoni ya watu usingekuwa ungekuja ukiwa more balanced!! unachanganya vitu viwili, cha kwanza ni ile article ya gazetini, na ya pili ni majibu anayoyatoa yeye humu jamvini;

to be honest afadhali angeishia kwenye article kwani kazi yake iliishia pale, tatizo ni alipokuja humu na kuanza laundry and kuexpose kitchen stuff zao forgetting his profession na ethics za grievances kwa watu ndani ya chama hasa mmoja akiwa kwenye propaganda [mwandishi] na mwingine akiwa kiongozi wa juu kiutendaji [naibu katibu]

Sina hakika kuna siasa zalumumba au rose garden....
 
Last edited:
Mkulima,

Be careful.

Kuna interest free loan ambazo hutolewa na waajiriwa kama wafanyakazi wa ngazi fulani kama kivutio kazini. Mwananchi imetoa mikopo ya kati ya milioni kumi mpaka 20 kwa wahariri ili wawe na usafiri na hawalipi riba.

CRDB wamefanya hivyo. Benki kuu pale nani anao uwezo wa kununu X FIVE BMW kama sio mikopo? Ni utaratibu wa Corporates Nyingi Duniani. Inatokea hivyo hasa pale ambapo riba za Mabenki zinaonekana kuwaumiza wakopaji. Mfano Barclays asiliamia 25, ukikopa milioni kumi ukanunua ghanri siku unamaliza kulipa deni ni milioni 17.5(They calculate compound interest).

Sasa kukopa kwa muajiri wako sio dhambi.
 
Kosa la Kibanda lilikuwa 'to pressurize Zitto to stand down" lakini anasulubiwa kwa kununua magari matatu... Je unajuaje amechukua mkopo benki?

I have known the fellow for years, even worked with him and his hands are cleaner than most of the other journalists out there.

Crucify him for his mistakes but not his developments especially when you cant prove that he is corrupt
 
Last edited:
Do you know Rostam Aziz effect in Tanzanian politics???? Do you know that at one time Zitto Kabwe wanted and supported the Government to buy the famous dilapidated Richmond Generators?? Huyu Kibanda amekuwa pia upande wa Raostam siku zote hasa wakati ule wa Mafisadi Papa Vs mafisadi Nyangumi!! I cant rule out kama wote hawako kwenye pay roll ya Fisadi Rostam. Rostam is something else in this country because he is a King maker. If he sponsored Riala Odinga duiring the 2007 election campaigns in Kenya, atashindwaje kumsaidia Zitto kwenye uchaguzi wa Chadema. Rostam effect is beyond imagination kwa kuwa Kibanda ni Kibaraka wake kama walivyo viongozi wengi wa nchi hii. jakaya Kikwete, Yusuph Makamba,Ibrahim Lipumba, Mbatia, Augostine Mrema and Christopher Mtikila can not deny this!!! wote hawa wako mfukoni kwa bwana mkubwa Rostam. Ukikosea ukamgusa Rostam, hawa wote pamoja na vibaraka wake watakushughulikia na lazima utamwomba radhi tu!!! Kibanda na Zitto kabwe wanaendeleza njaa tu ya watanzania!!!!!! Mimi naliona zaidi anguko la Watanzania kuliko hili la Kibanda na Zitto.

uliyoyasema mkuu ni mazito. can you prove it?
 
Simply said a pandemic pot of despicable despotism, nauseating nepotism and incospicuous incompetency coupled with idiocratic incoherency.

Mkuu unanimaliza na u language wako. Dictionary wapi........???
 
Ndugu,

Rostam hakuwahi kumsaidia Raila Amolo Odinga kwa sababu kama ni fedha huyu Jaluo ana pesa ya kutosha na elimu ya maswala ya kisiasa na kijeshi zaidi ya Aziz. Leo hii ni partner na matajiri wa Afrika kama Cyril Ramaphosa.

By the way, RA kwa kenya hajafikia hata level ya Joe Michuki ambaye anamiliki benki ya Housing and Finance ambayo ni kubwa zaidi ya CRDB.

Raila kwa hapa Tanzania ana uhusiano na familia ya akina Odemba na Magufuli Pombe aka Masamaki, lakini sio RA. Haitatokea hata siku moja mpiganaji wa level kama ya Odinga awe partner wa RA.

Fanya utafiti usikurupuke tu kwa vile internet iko free. Utajiri binafsi wa Raila ni wa kutosha kwani licha ya kurithi mali toka kwa babake pia anayo makampuni ya kibiaeshara ndani na nje ya Kenya. Huyu sio kibaka
 
ZuluBoy,

Sijakuambia kukopa free interest loan ni dhambi. Nilichosema ni kwamba ukipewa mkopo na rafiki yako au mwajiri na usiwe na interest mahali mbalimbali duniani inatakiwa ulipie kodi kwenye ile amount unayo save.

Watu wengi wanafanya kimya kimya na yanaishia hivyo hivyo. Ni sawa na wanaopangisha nyumba ambao hawalipi kodi miaka na miaka.

Lakini ukitangaza rasmi kama alivyofanya Kibanda, hapo unawakaribisha TRA nyumbani.

Labda kama sheria zetu za kodi ni butu sana. Kumbuka kuna viongozi wengi tu duniani wamepoteza kazi kwa kushindwa ku declare interest free loan na hivyo kushindwa kulipa kodi.

Mkulima,

Be careful.

Kuna interest free loan ambazo hutolewa na waajiriwa kama wafanyakazi wa ngazi fulani kama kivutio kazini. Mwananchi imetoa mikopo ya kati ya milioni kumi mpaka 20 kwa wahariri ili wawe na usafiri na hawalipi riba.

CRDB wamefanya hivyo. Benki kuu pale nani anao uwezo wa kununu X FIVE BMW kama sio mikopo? Ni utaratibu wa Corporates Nyingi Duniani. Inatokea hivyo hasa pale ambapo riba za Mabenki zinaonekana kuwaumiza wakopaji. Mfano Barclays asiliamia 25, ukikopa milioni kumi ukanunua ghanri siku unamaliza kulipa deni ni milioni 17.5(They calculate compound interest).

Sasa kukopa kwa muajiri wako sio dhambi.
 
Kibanda,
Mkuu wangu nikuulize.. wewe unasema ni mwandishi wa habari au sio? inakuwaje wewe huyo huyo unakuwa mtetezi wa Mnyika na Mrema dhidi ya Zitto wakati sidhani kama unaelewa hisia za hao watu.
Kama mwandishi mzuri kwa nini suikimbilie kwa Mnyika na Mrema ukawasikiliza wao wenyewe wanasema nini badala ya wewe mkuu wangu kuendeleza tungo zako ambao hazimsaidii mtu yeyote yule. Mkuu enough! unachosha sana yaani kama mimi ningekuwa Mbowe au mhariri wa Daima basi huna kazi!..
Reporter siku zote huandika maelezo ya watu na sio yake yeye kwa jinsi anavyojishirikisha ktk scandal kisha anakuwa mwandishi.. Haya ni matumizi mabaya sana ya madaraka sawa na Fisadi ambaye anatumia vibaya madaraka yake. Kama wewe ni mwandishi bakia kuwa mwandishi na kama unaandika kama Kibanda zungumza kama Kibanda mpinzani wa Zitto na ukubali kukosolewa pia.

Ndugu yangu Mkandara wewe mwenyewe unakiri kuwa mimi ni mwandishi wa habari halafu unaniuliza ninajuaje juaje hisia za Mnyika na Mrema?. Hiyo ni moja ya kazi za mwandishi wa habari. Ninazijua hisia zao kwa sababu nimefanya nao mazungumzo ya ana kwa ana kuhusu suala hili zima akiwamo na Zitto mwenyewe.

Mbowe si dikteta na mbinafsi kama wewe na ndiyo maana katika gazeti lake la Tanzania Daima habari na taarifa nyingi tu zinazoandikwa zinahusu maamuzi mbalimbali ya kiserikali. Si hayo tumeandika kwa kina taarifa kuhusu masuala yanayohusu vyama vingine vya siasa kama CCM, CUF, TLP na NCCR Mageuzi.

Ni kwa sababu tu kwamba hivi sasa ajenda kuu katika vyombo vyote vya habari nchini hivi sasa ni Uchaguzi wa Chadema na sisi kama wana habari tunao wajibu wa kueleza kile tunachokiona na kukifahamu.

Hata hivyo tunatambua kwamba maandishi yetu yanawakera na wakati mwingine kugusa hisia za wasomaji. Inapotokea hali kama hiyo kwa mwanahabari ni jambo la kulifurahia kwani ndivyo inavyopaswa iwe.

Mimi si reporter nilishavuka huko mwaka 1999. Ni mhariri, ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa. Ninao wajibu (nasisitiza wajibu) na haki ya kuchangia masuala yote yanayoweza kuathiri mustakabali wa taifa letu.

Wanahabari tunapoijadili Chadema hapa hatufanyi hivyo kwa sababu ama ni wanachama wa Chadema au maadui wa chama hicho. Tunafanya hivyo tukitambua kuwa chama chochote cha siasa chenye ushawishi mkubwa kama vilivyo vyama vya CCM, Chadema na CUF hivi sasa vinapaswa kuwatumikia wananchi ipasavyo.

Kwa sababu hiyo basi, tunapomjadili Mbowe hapa au Zitto, Mnyika, John Mrema na wengine, tunawaangalia kama viongozi wa kitaifa wenye wajibu wa kuwatumikia si wanachama wao tu la hasha bali pia wananchi. Ndiyo maana hata hoja za ufisadi wa EPA, Buzwagi, Meremeta, Deep Green, Richmond, na mwingine wote ambao umekuwa ukipingwa na akina Mbowe, Slaa, Zitto, Mnyika na Mrema unagusa masuala ya nchi na si ya mtu mmoja mmoja.

Kwa sababu hiyo basi, tunapomhoji na kumbana Zitto au mwingine yeyote tunafanya hivyo lengo likiwa ni kuhakikisha Chadema na kambi ya upinzani inabakia madhubuti. Tunatambua kwa kufanya hivyo tunawakera sana mamluki na CCM yao, ambako vijana wengi (si wote) wanaangalia zaidi madaraka na matumbo yao kuliko mustakabali mwema wa nchi yao.

Ni wazi kwamba, kwa kufanya hivyo tunaweza tukawa tukifanya makosa. Ni kwa kutambua hilo, tuko tayari kukosolewa wakati wowote na huo ndiyo msingi wa kukubali kwetu kwa hiari kujiunga katika JF na kabla ya hapo tulikuwa wafuatilia wa mara kwa mara wa maandiko yake.
 
Nashukuru kwa ufafanuzi Kibanda. Wewe ni mpiganaji shupavu. Tafadhali sana usikubali kununuliwa na mafisadi. Baada ya shutuma za hapa na pale nilianza kuhofu kwamba tumeshakupoteza mpiganaji muhimu! Lakini mwangalie sana huyo kijana wako aitwaye Mulinda. Kuna tuhuma nyingi dhidi yake, zisije zikaliharibia sifa gazeti letu tulipendalo - Tanzania Daima.


Kaka nimekupata, nimekuelewa. Tutajisahihisha
 
Ni wazi kwamba, kwa kufanya hivyo tunaweza tukawa tukifanya makosa. Ni kwa kutambua hilo, tuko tayari kukosolewa wakati wowote na huo ndiyo msingi wa kukubali kwetu kwa hiari kujiunga katika JF na kabla ya hapo tulikuwa wafuatilia wa mara kwa mara wa maandiko yake.

Thanks Kibanda... you have done what real men do!!!. its now good to pick up pieces and move on...
 
Unajua Kibanda hapa naona unafaidisha wabaya wako wengi kwa kumwaga mboga bora unyamaze wengi wamezoea kudanganywa na kudanganya unapo ongea ukweli unawanufaisha kukujua in and out.

Ninakubaliana na ninatofautiana na msimamo wako. Kimsingi ninachokiandika wala si mambo ya siri kwani mimi siko ndani ya vyama vya siasa, ni mambo ya kawaida tu ambayo baadhi ya watu kwa sababu ya kutoyajua sawasawa wanalishwa uoza na mawakala wa vyama vya siasa kwa sababu zao binafsi.

Usihofu jambo lolote ndugu yangu. Nimekuwa nikisoma maoni mbalimbali ya watu katika jamvi hili na nikabaini kwamba wako mabingwa wa propaganda ambao wamekuwa wakitumia mbinu ya kusema uongo mara nyingi na kuufanya uongo huo hatimaye uaminike na kuonekana ni ukweli.

Huyu Zitto ambaye niliupinga uamuzi wake wa kugombea uenyekiti (kwa sasa) amekuwa akizushiwa kila aina ya uongo, wakati mwingine imefikia hatua anachafuliwa kwa sababu tu ya kuwa na msimamo ambao hauwapendezi wengi.

Imefika mahali sasa hivi watu wanawazushia wenzao kwamba wamehongwa fedha au vitu na wanataja hata kiasi ambacho mhusika amepewa na wanafanya hivyo wakitumia majina tofauti bandia, kwa sababu tu ya malengo yao. Tabia hii haiwezi kukabiliwa kwa kukaa kimya na kuuacha uongo uote na kukomaa ndani ya vichwa vya Watanzania.

Naamini wakati wa kuanza kubainisha pumba na mchele umefika. Hili jamvi linaitwa 'The Home of Great Thinkers' ambalo hivi sasa baadhi ya wahuni wamefikia hatua ya kutaka kulifanya kuwa 'The Home of Great Liars'. Hili jambo si la kuliunga mkono hata kidogo na kuacha likaendelea kutalipeleka taifa kusikofaa.

Ingawa sijapata kuwa mwanaharakati wa siasa zaidi ya kuwa mwana habari na mchambuzi wa masuala ya kisiasa naamini ipo haja ya kulipigania taifa letu. Ninajua wakati tukichukua hatua za namna hiyo, tutakuwa tukifanya makosa madogo na makubwa, walakini kila tutakapobaini makosa ya namna hiyo tutakuwa na wajibu wa kuomba radhi na kusonga mbele. Huko ndiko TUENDAKO.
 

Naamini wakati wa kuanza kubainisha pumba na mchele umefika. Hili jamvi linaitwa 'The Home of Great Thinkers' ambalo hivi sasa baadhi ya wahuni wamefikia hatua ya kutaka kulifanya kuwa 'The Home of Great Liars'. Hili jambo si la kuliunga mkono hata kidogo na kuacha likaendelea kutalipeleka taifa kusikofaa.

Ingawa sijapata kuwa mwanaharakati wa siasa zaidi ya kuwa mwana habari na mchambuzi wa masuala ya kisiasa naamini ipo haja ya kulipigania taifa letu. Ninajua wakati tukichukua hatua za namna hiyo, tutakuwa tukifanya makosa madogo na makubwa, walakini kila tutakapobaini makosa ya namna hiyo tutakuwa na wajibu wa kuomba radhi na kusonga mbele. Huko ndiko TUENDAKO.

Mkuu Kibanda, maandiko yako mengi makali makali nimekuwa siyapendi na yamekuwa yakinifanya niumie sana. Maandiko ya baadhi ya wengine pia yameniumiza zaidi kwa kuwa yamezidi kutia moto kwenye petroli, lakini maneno hayo hapo juu yamenipa faraja kubwa na yanahitaji KUFANYIWA KAZI na sote humu JF. Bahati mbaya kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu (mawasiliano duni) nakosa nguvu ya kujadili kwa uzito unaostahili.
 
Ndugu yangu Mkandara

Mbowe si dikteta na mbinafsi kama wewe na ndiyo maana katika gazeti lake la Tanzania Daima habari na taarifa nyingi tu zinazoandikwa zinahusu maamuzi mbalimbali ya kiserikali.

Sikujua bro Mkandara kwamba wewe ni dikteta na mbinafsi.

Nakuheshimu Mkandara kwa mawazo mazuri hapa jamvini na sijui ya mtu kukuita dikteta na mbinafsi inatoka wapi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom