Nakupenda sana Shetani

Unasema Mungu hakudhamiria kuishi pamoja na wanadamu but devil has made that. Je, Mungu hana msimamo?
Mungu anabadilika?
Mungu hajui la kesho?
 
Ulivyo andika kana kwamba una mjua vizuri huyo shetani
 
😎Hata mimi nikuwa na mashaka makubwa sana kuhusu uwepo wa huyu kiumbe anayeitwa shetani, kwa sababu kwa maelezo ya vitabu vyote vya dini ni kuwa huyu kiumbe alikua ni Malaika mkuu aliyekuwa ameumbwa na mungu kwa ajili ya malengo yake mwenyewe mpaka siku alipomuasi muumba wake ambaye ni Mungu kwa mujibu wa hizo hadithi za kwenye vitabu;

Naomba wajuzi wa haya mambo waje hapa kilingeni kujibu hoja, bila kuleta Jazba.

Maswali.😱

1 -Ni kwanini Mungu anaendelea kumvumilia huyo kiumbe anayeitwa shetani katika harakati za kuwaangamiza viumbe wengine walioumbwa na Mungu wanaoitwa binadamu?

2 -Mungu Muumba wa binadamu na Shetani atapata faida gani kuwachoma binadamu ambao kwa maelezo ya vitabu hivyo upeo wake wa kuelewa mambo ni mdogo kuliko wa shetani aliyekua Malaika wake Mkuu?

3 -Inamaana Mungu wakati anamuumba shetani hakujua kama angeweza kumuasi?

4 -Nilini shetani alibadilika na kuwa na mapembe na mkia kama taswira ya shetani inavyoonyeshwa na wanazuoni wa dini?

5-huko kwenye hivyo vitabu kuna hadithi ya Adamu na Hawa ama Eva, na kwa mujibu wa hadithi za humo ni kuwa baada ya kula tunda walipewa adhabu na moja ya viumbe vilivyopewa adhabu ni nyoka, Ni kwanini mungu ampe nyoka adhabu wakati aliingiliwa na shetani badala ya kumpa adhabu shetani?

6 -Je Mungu anakiogopa kiumbe chake alichokiumba (Shetani) hadi anashindwa kukichukulia hatua stahiki na badala yake amempa uhuru wa kuingilia viumbe dhaifu kama nyoka na binadamu.😎
 
7- kwanini mungu amekuwa akimlaumu sana shetani kuliko shetani kumlaumu mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wororo yayeeee...akagudha uroro
 
Dunia inahitaji muongozo mpya kwenye maswala ya kiimani no wonder sasa hivi kuna corona ambayo inatishia uwepo wa taasisi za kiimani, Ambazo mpaka sasa zaidi ya hadithi za shetani na kwamba kila changamoto inasababishwa na kiumbe hiki ambaco Mungu alikipenda zaidi hapo kale kiasi cha kukipa ufalme 😎 zinaonekana kushindwa kutoa suluhu kwa changamoto mpya zinazoikabili dunia (Mfano corona, ajali, concer, mafuriko, vimbunga, mabadiliko ya tabia ya nchi nk. yanayoikabili dunia kwa sasa.
 
JE, UMESHAFUTA HII KAULI YAKO? FANYA HIMA!
 
Laana tullahi. Allah, akupe ufahamu na kutubia hili kabla hujafa ktk ukafiri huo.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na Shetani naye anakupenda? Mnapendana wote?
 
Mungu hakutaka watu wakaishi Kwake ila kwa akili zako ulitengeza kifo ili watu warudi wakaishi alikokuwa baba yao sijui nikupe zawadi gani katika hili. DAAA

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani kabla Babu yetu Adam na Bibi Eva kuletwa duniani, waliishi wapi mwanzo ? si kule Padise (peponi)?
Na ni nani aliyewafitini mpaka wakatolewa huko? Si yeye Nyoka (shetani-ibilisi)
hapa duniani si tupo kwa muda maalum kisha tutarudi kule tulikokuwa?
Lakini si yeye shetani anayetaka tusirudi kule bali tuishie Jehannam?
mbona sikuelewi?
 
kwa sababu kwa maelezo ya vitabu vyote vya dini ni kuwa huyu kiumbe alikua ni Malaika mkuu aliyekuwa ameumbwa na mungu kwa ajili ya malengo yake mwenyewe mpaka siku alipomuasi muumba wake ambaye ni Mungu kwa mujibu wa hizo hadithi za kwenye vitabu;
Wewe muongo hujasoma hivyo vitabu vyote, labda ulipitia tuu Biblia,
Qur-an hujaipitia popote pale wala hujauliza kwa wadau wa kitabu hicho,kuwa kinasemaje juu ya uasili wa Shetani.

Hebusoma Hii Quran sura ya 18:aya ya 50.
''Na pale
tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! basi Walimsjudia wote , isipo kuwa Ibilisi, kwa kuwa Yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi.Basi Je! hivi Mnamfanya yeye IBILISI na kizazi chake kuwa marafiki badala yangu mimi Mungu?, hali wao (hao mabilisi) ni adui zenu? Hili Ni chaguo ovu mno na mbadala mbaya sana waliofanya kwa wenye kudhulumu. ''
NB:
Nimeongeza ufafanuzi ndani ya aya hii.

Kwa hiyo shetani hakuwa Malaika,bali ni katika Majini.
 
Huyo shetani ulishawahi kumwona?

Sent using Jamii Forums mobile app
Si kila asiyeonekana hayupo,

Bali kuna namba zake.

Unapokwenda kwa FUNDI kumloga mwanume wako asikupige buti,huwa unatumia nguvu gani kule kama si huyo jamaa?
Limbwata, Misukule, ili kuongeza tija za biashara, hamuzioni hizo kwa kuwaua Mama zenu au Baba zenu au watoto ili mupate Mali?

Wewe si Mtu wa Iringa? Mkinga? huyajuwi haya?
 
Wengine wanaiita ganja wengine msuba wengine bomu lakini naona umekuja na jina jipya "shetani" 😁 😁 😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…