"Nakupenda sana Jack Pemba, SIYO SIRI!"

Lakini WOS cha kukumbusha Jack Pemba hivi sasa amefulia totaly mpaka anaona aibu kutoka alikuwa anamzalau mdogo wake sasa yupo TBT pale aibu kafulia.

Badala ya kuinvest kwenye vitu vya maana kainvest kwenye sifa za kijinga matokeo yake ndiyo hayo sasa.
 
Mkuu si unajua wabongo? Ana hiari atoe mamilioni kwenye harusi ili aonekane ila mtu huyo huyo mfuate kumuomba msaada kimya kimya kama ata kupa.

hehehe mzee usinikumbushe machungu ya kule kwenye sadia JF kisha saidia wana Mbagala mifano ipo hapa hapa wazi JF waTZ wagumu sana kuchangia kimya kimya lakini ile ya kuonekana wazi mbele za umati tunapenda sana masifa, maujiko n.k
 
Hebu tuone/tuwaorodheshe wale wote wanaoimbwa tuangalia wamefanya nini cha mno kwenye jamii na kama kuimbwa kwao na kutukuzwa kunastahili:
1.Jack Pemba
2. Ndama Mtoto wa Ng'ombe
3. Papaa Msofe
4.Chief Kiumbe
5......
 
Hebu tuone/tuwaorodheshe wale wote wanaoimbwa tuangalia wamefanya nini cha mno kwenye jamii na kama kuimbwa kwao na kutukuzwa kunastahili:
1.Jack Pemba
2. Ndama Mtoto wa Ng'ombe
3. Papaa Msofe
4.Chief Kiumbe
5......

Huyu ameshafulia WOS mtoe kabisa.
 
hehehe mzee usinikumbushe machungu ya kule kwenye sadia JF kisha saidia wana Mbagala mifano ipo hapa hapa wazi JF waTZ wagumu sana kuchangia kimya kimya lakini ile ya kuonekana wazi mbele za umati tunapenda sana masifa, maujiko n.k

Mkuu wewe sema tu una changisha kwa ajili ya harusi na wachangiaji wakuu watakaa high table utaona michango itakavyo miminika. Watu watakua tayari hata kutoa ID zao za kweli. Au waambie hela zikisha changwa tunaenda kutoa Mbagala na camera crew.
 
..hivi hat akama ndio kutoa hela uimbwe... najua hizi bendi zinamilikiwa na watu wenye kuheshimika katika jamii - Akudo kwa mfano nasikia kuna Waziri mmoja anaimiliki...
InawezA kuwa ni heshima bandia, si unajua jinsi viongozi hawa wanavyosifika kwa ufisadi?
 
Wadau, hivi huyu Jack Pemba nilisikia kuna kibibi kilikuwa kinam-backup huko
UK then akishuka huku ndo mbwembwe kibao.

Au alikuwa na other dubious means za kuingiza pesa?
 
Hebu tuone/tuwaorodheshe wale wote wanaoimbwa tuangalia wamefanya nini cha mno kwenye jamii na kama kuimbwa kwao na kutukuzwa kunastahili:
1.Jack Pemba
2. Ndama Mtoto wa Ng'ombe
3. Papaa Msofe
4.Chief Kiumbe
5......

Dada WoS hayo majina tu kazi. Mtu yoyote mwenye akili hajiiti hivyo.
 
Last edited:
hehehe mzee usinikumbushe machungu ya kule kwenye sadia JF kisha saidia wana Mbagala mifano ipo hapa hapa wazi JF waTZ wagumu sana kuchangia kimya kimya lakini ile ya kuonekana wazi mbele za umati tunapenda sana masifa, maujiko n.k

uko sawa kabisa Fidel80,badala tuchangie vitu vya maana na majanga yanayowakuta wanajamii wenzetu,eti mtu mzima kabisa na akili zako unaenda toa pesa ili uimbwe,jamani hivi akili zetu lini zitaamka?
 
Mkuu wewe sema tu una changisha kwa ajili ya harusi na wachangiaji wakuu watakaa high table utaona michango itakavyo miminika. Watu watakua tayari hata kutoa ID zao za kweli. Au waambie hela zikisha changwa tunaenda kutoa Mbagala na camera crew.

hahahaha we acha tu kuna mzee mmoja binti yake alikuwa anaolewa maeneo ya baruti pale sasa kikao cha send off cha kwanza watu walijaa bar nzima mi nilikuwa nasuuza koo pale dah nilishangaa mala ya kwanza nilijua kuna sherehe nikaambiwa kikao cha send off hicho nilishika tama sasa watu walipo anza kutoa ahadi na pesa taslimu kima cha chini kilikuwa laki moja 100,000/= nilishangaa sana mkuu watu tunapenda sana kujionyesha sana.
 
HAYA tuache hayo ya Kumpenda Mume wa wenyewe Jack Pemba
Kuna maPDG huimbwa mwanzo hadi mwisho... tena wenye wasifu wa kutiliwa mashaka --- kina Papa Msofe, Ndama Mtoto wa Ng'ombe,n.k hivi wanaimbwa ili iweje? Kuwapa umaarufu kwa jipi jema wanalofanyia jamii ya watanzania?MAKUBWA HAYA!

WoS utamaduni huu haukuwahi kuwapo katika miziki yetu(ya dansi) kabla ya wakongo kuingia katika muziki hapa nchini ndio maana inawapa shida sana watu wengine. Lakini ukweli ni kwamba tabia hii ya kutaja majina ni aina fulani ya matangazo na inawasaidia sana wanaotajwa kwenye biashara wanazozifanya. Kwa mfano hao wote uliowataja ukiacha Jack Pemba ni wafanya biashara na kwa namna moja au nyingine mafanikio yao yametokana na kuimbwa. Kwa mfano biashara za mamaa Dotnata umeweza kumsaidia kupata kazi nyingi kwa urahisi kwenye biashara yake catering na decoration. Kifupi faida wanazo zipata ni kubwa sana ukilinganisha na gharama wanazotumia. jaribu kuwaza hiyo air time anayopata mtu kama ndama angekuwa amelipia tangazo redioni ingekuwaje? Kwa watu wengine pia inawajengea umaarufu wanaoutumia kwenye siasa, mfano said ntimizi aliweza kuwashinda wagombea wengine wa uenyekiti wa vijana mkoa wa dar kwa kuwa wapiga kura walikuwa wanalijua jina lake kabla. Nafikiri utaratibu huu si mbaya ukilinganisha faida na hasara zake pia unasaidia kuwalipa wasanii wetu ukizingatia muziki hapa nchini haulipi na hata hizo radio station huwa zinafaidika kutokana na huo muziki bila kurudisha fadhira kwa wana muziki lakini bila kujua wapiga matangazo ya biashara humo humo.KUHUSU kuifanyia kitu jamii hilo ni suala binafsi kwani hata sisi ambao hatutajwi tunaifanyia nini jamii? kwani Pretty na mwanajamii one wanatofauti gani mamaa Dotnanta?
 
hahahaha we acha tu kuna mzee mmoja binti yake alikuwa anaolewa maeneo ya baruti pale sasa kikao cha send off cha kwanza watu walijaa bar nzima mi nilikuwa nasuuza koo pale dah nilishangaa mala ya kwanza nilijua kuna sherehe nikaambiwa kikao cha send off hicho nilishika tama sasa watu walipo anza kutoa ahadi na pesa taslimu kima cha chini kilikuwa laki moja 100,000/= nilishangaa sana mkuu watu tunapenda sana kujionyesha sana.

Mimi nina baba mkubwa aliuza pikipiki atoe mchango wa harusi haha.
 
Dada Wo hayo majina tu kazi. Mtu yoyote mwenye akili hakjiiti hivyo.

Ni kweli kabisa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kujiita eti Ndama Mtoto wa ng'ombe,hivi hawa watu wanafamilia?Mi naona kama vile wanazidhalilisha familia zao kwa kujiita majina ya ajabu ajabu.
 
Mimi nina baba mkubwa aliuza pikipiki atoe mchango wa harusi haha.

hahahaha duh kisa akanywe na ale hii balaa na huyo akienda apewe bia 2 si unajua harusi za wenzetu wa kule Bukoba ukiongeleshwa ukashindwa kujibu wanakutambua sio mwenzetu utakuta bia zinamiminika meza ya 2 kwako dry tu na umetoa mchango laki mbili niambie hapo hahahahaha watu iwa wanarusha ngumi hahaha.
 
Ni kweli kabisa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kujiita eti Ndama Mtoto wa ng'ombe,hivi hawa watu wanafamilia?Mi naona kama vile wanazidhalilisha familia zao kwa kujiita majina ya ajabu ajabu.

Majina kama ya kichawi vile. Mimi nadhani hawa wanakua na matatizo fulani maana hawaeleweki. Mara ya kwanza nasikia haya majina nilidhani utani kumbe wenzetu wapo serious kabisa.
 
WoS utamaduni huu haukuwahi kuwapo katika miziki yetu(ya dansi) kabla ya wakongo kuingia katika muziki hapa nchini ndio maana inawapa shida sana watu wengine. Lakini ukweli ni kwamba tabia hii ya kutaja majina ni aina fulani ya matangazo na inawasaidia sana wanaotajwa kwenye biashara wanazozifanya. Kwa mfano hao wote uliowataja ukiacha Jack Pemba ni wafanya biashara na kwa namna moja au nyingine mafanikio yao yametokana na kuimbwa. Kwa mfano biashara za mamaa Dotnata umeweza kumsaidia kupata kazi nyingi kwa urahisi kwenye biashara yake catering na decoration. Kifupi faida wanazo zipata ni kubwa sana ukilinganisha na gharama wanazotumia. jaribu kuwaza hiyo air time anayopata mtu kama ndama angekuwa amelipia tangazo redioni ingekuwaje? Kwa watu wengine pia inawajengea umaarufu wanaoutumia kwenye siasa, mfano said ntimizi aliweza kuwashinda wagombea wengine wa uenyekiti wa vijana mkoa wa dar kwa kuwa wapiga kura walikuwa wanalijua jina lake kabla. Nafikiri utaratibu huu si mbaya ukilinganisha faida na hasara zake pia unasaidia kuwalipa wasanii wetu ukizingatia muziki hapa nchini haulipi na hata hizo radio station huwa zinafaidika kutokana na huo muziki bila kurudisha fadhira kwa wana muziki lakini bila kujua wapiga matangazo ya biashara humo humo.KUHUSU kuifanyia kitu jamii hilo ni suala binafsi kwani hata sisi ambao hatutajwi tunaifanyia nini jamii? kwani Pretty na mwanajamii one wanatofauti gani mamaa Dotnanta?
Asante Burn kwa kuonyesha upande chanya wa kuimbwa.Sasa inakuwaje wengi wa wanoimbwa siyo wale wenye biashara zinazoeleweka?
Na ninajua kuwa wanazo pesa za kutosha kujitangaza.Kwa wanasiasa kama Ntimizi, hicho ni kitu kingine kwa sababu miaka ya nyuma miziki ya Tanzania ilijaa kuimba wanasiasa - Nyerere, Karume, Aboud Jumbe, Kawawa, mama Maria Nyerere,mara Dr Kleruu n.k. hadi lilkuwa ina bore!
 
hahahaha duh kisa akanywe na ale hii balaa na huyo akienda apewe bia 2 si unajua harusi za wenzetu wa kule Bukoba ukiongeleshwa ukashindwa kujibu wanakutambua sio mwenzetu utakuta bia zinamiminika meza ya 2 kwako dry tu na umetoa mchango laki mbili niambie hapo hahahahaha watu iwa wanarusha ngumi hahaha.

Ishu una fikiria ilikuaje? Jamaa siku ya kutoa ahadi za mchango kakaa na watu wenye nazo. Kusikia ahadi za wenzake akaona aibu ikabidi atoe ahadi kubwa. Siku zina karibia hana kitu ikabidi auze pikipiki. Sasa mtu mwenye akili unauza mali yako kisa mchango?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom