"Nakupenda sana Jack Pemba, SIYO SIRI!"

"Nakupenda sana Jack Pemba, SIYO SIRI!"

WOS mi nimeipenda hiyo unacheza na baba watoto then Patcho Mwamba aka tajiri wsa FM Academia anaimba ``Nakupendaga sana mume wangu Jack Peeeeembaaaa`` hahaaaaa
 
Ndicho hasa kinanichekesha zaidi......watu wako bize...utaona hata wanaume (baadhi yao) wanaitikiwa kibwagizo hicho kwa furaha kabisa hahahahahah huku wengine wanakuwa wameuchuna utadhani wamelazimishwa kucheza ..ukizingatia anaeimbwa ni PDG mhhh.

wos sweetheart nakubaliana nawe kwamba ni kicheksho kikubwa kwa midume kuitikia kibwagizo hicho.
 
Mie nami huwa napenda nyimbo zao lkn yale majina yanayotajwa yanatuchefua wengi!
 
sometimes wanapewa offer za bia na vijizawadi vidogovidogo, Lakini wakati mwingine ni kama wanalipia tangazo mfano JB Mpiana au Koffi wakitaka kutoa nyimbo wana invite watu wanaotaka kurushwa hewani, wanalipwa and then wana rushwa. Joseph Kusagga alisha mlipa pesa JB Mpiana na akarushwa katika moja ya nyimbo zake.
 
Mkuu si unajua wabongo? Ana hiari atoe mamilioni kwenye harusi ili aonekane ila mtu huyo huyo mfuate kumuomba msaada kimya kimya kama ata kupa.


Ndugu yangu kutoa ni moyo na hiari ya mtoaji. Hao wanaofanya hivyo mara kadhaa kwao kuna matatizo au wenyewe wan frustrations za maisha ndio maana ukiwaomba hawakupi. Pili si lazima kusaidiwa na mtu usiyemjua eti kwa sababu tu anatoa hela kwa wanamuziki. Hiyo ndiyo furaha yake kama wewe ilivyo kuangalia bial kutoa chochote. Usilazimishe msaada utakutokea puani ndugu
 
Mimi huwa sisikilizi bolingo za bongo.
hivi bado wanawataja mabwana zao hao jamaa?
 
Ngoja na mimi nitakuja huko dar nitafute bendi nikiwapa kama milioni kadhaa waniimbe utasikia"wapi papa milioni tajiri mutoto,papaa milioni mutu ya watu"duu alf kesho yake nauli sina mmh!
 
Msaga Sumu alimuimba Lowassa. Inamaana Lowassa alitoa hela aimbwe?
 
Sijui imekaaje wanamuziki wengi sio tanzania tu hata wacongo kuuvaa u husika wa kike huwa sipati jibu utasikia"mume wangu ana matatizo yanayonifanya nikonde siku hadi siku kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba si jambo la kushangaza hilo kinachoniuma mwenzenu ni kulala sebuleni ooh mimi na watoto.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom