Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

Pole kedekede kwa yaliyokukuta.

Taarifa ziko za aina tatu:

1. Kwa ajili ya kuzingatia (for noting):
Hii ni kwamba mtu anakuarifu kitu, ili ujue tu, kipo hicho kitu. Huna nafasi ya kufanya chochote kile kuhusu hicho kitu kukizuia au kukifanya kiendelee.

2. Kwa ajili ya Kupendekeza (for endorsement):
Hii ni pale mtu anapokuarifu kitu, ili ukichekeche na kuwa na nafasi ya kukipendekeza kiende kwa yeye ambaye anao uwezo wa kukizuia au kukifanya kiendelee. Kwenye hili unakuwa kwanza umezingatia (you have noted), halafu ukikubali kupendekeza jambo linaendelea mbele ya safari. Usipopendekeza, unaweza kumrudishia mwenyewe kwamba sipendekezi mpaka ufanye yafuatayo utakayotaka wewe ili upendekeze. Au unaweza kuendeleza mchakato kwa kutoa maoni yako kwamba hupendekezi, lakini taarifa isonge mbele. Mtoa maamuzi atajua kwamba hukupendekeza, lakini umeruhusu mchakato uendelee. Yeye ataweza kutoa uamuzi kurudisha suala kwako lirekebishwe mpaka ukubali kupendekeza, au ataendelea na mchakato huku akizingatia kwamba hukupendekeza.

3. Kwa ajili ya Kuridhia (For Approval):
Hii ni pale unapoletewa taarifa kwamba kitu fulani hakiwezi kufanyika, mpaka wewe utoe uamuzi kwamba kifanyike au kisifanyike.


Kwa hiyo, ile taarifa uliyopewa inaangukia fungu lipi?
Namba moja!
 

Uzi rejewa kwenye linki hapo juu unaweza kuwa wa manufaa.
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.

Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
Pole sana. Jaribu kusahau kwani sioni kosa lako liko wapi. Nakuhakikishia huna kosa. Kuna story ya mpiga picha wa Africa Kusini ambayo nadhani baadhi wameshaisikia inaitwa ''The vulture and the little Girl''. Huyu mpiga picha alikuwa anapiga picha Sudan kuhusu njaa miaka ya 90. Siku moja akakutana na mtoto aliyedhoofika sana hata kutembea hawezi, anajitahidi kutambaa kwenda kwenye kambi ya kutoa msaada huku ndege mla mizoga akimnyemelea kwa nyuma, ikitokea akifia njiani amle. Ile picha ilileta simanzi sana na mpiga picha alipouzwa hatua alizochukuwa alidai alimfukuza yule ndege mla mizoga. Hili lilifanya watu wengine wamlaumu kwa sababu walisema ilitakiwa pia atoe msaada kwa yule mtoto. Jambo hili lilimuuma sana yule mpiga picha na akaamua kujiua mwaka mmoja baadae.
1622472265052.png
 
Pole sana. Jaribu kusahau kwani sioni kosa lako liko wapi. Nakuhakikishia huna kosa. Kuna story ya mpiga picha wa Africa Kusini ambayo nadhani baadhi wameshaisikia inaitwa ''The vulture and the little Girl''. Huyu mpiga picha alikuwa anapiga picha Sudan kuhusu njaa miaka ya 90. Siku moja akakutana na mtoto aliyedhoofika sana hata kutembea hawezi, anajitahidi kutambaa kwenda kwenye kambi ya kutoa msaada huku ndege mla mizoga akimnyemelea kwa nyuma, ikitokea akifia njiani amle. Ile picha ilileta simanzi sana na mpiga picha alipouzwa hatua alizochukuwa alidai alimfukuza yule ndege mla mizoga. Hili lilifanya watu wengine wamlaumu kwa sababu walisema ilitakiwa pia atoe msaada kwa yule mtoto. Jambo hili lilimuuma sana yule mpiga picha na akaamua kujiua mwaka mmoja baadae.
View attachment 1803741
Anaitwa Kevin Carter mkuu!Alijiua 1994 nadhani!
 
siku ya Idd nilimpigia simu rafiki yangu nikitaka kujua kwanini hakunialika/kunikaribisha kwenye IDD wala hakunitumia ujumbe hata zile za kufowadiana tu ( Yeye alikua mwislam) na tulikua na mazoea haya ya kukaribishana au hata kujuliana hali tu kila mara, basi nikapiga, haikupokelewa, nikazidi kupatwa mashaka maana haikua kawaida yake, nikajua akiona missed call yangu atanipigia, ila hadi asubuhi ya siku iliyofuata hakupiga, nikazidi kukosa amani. Nakumbuka ilikua mida ya saa tatu asubuhi nilikua nimetoka home nikapiga tena simu ila nikaanza kukosa tu amani bila sababu ya msingi, mara simu ikapokelewa na sauti ya kike, sikustuka maana ni kawaida simu yake siku nyingine kupokelwa na mke wake. Nilivyosikia sauti ya kike nikaanza kumtania "Shemeji imekuaje mmekula iddi peke yenu bila kunikaribisha?:" nikaona kama vile yule mtu hanifahamu, ikabidi nitulie nimuulize, wewe si ni mama fulani? Akajibu akasema "Mimi ni Shemeji yake, jana nilikua kwako Baba fulani ni mgonjwa, hivyo wakati naondoka nikasahau nikabeba simu yao nikaacha yangu, wapigie kwenye namba ya airtel"

Nikaipiga namba ya mshkaji akapokea mke wake akaniambia jamaa yako ni mgonjwa, nikamwambia mpe simu niongee nae, akasema hawezi hata kuongea, aagh kidogo sikuamini maana tangu nimefahamiana na jamaa zaidi ya 15 years ago sijawahi kusikia anaumwa kiasi hiki, shida nini akaniambia. nikawashauri wampeleke hospital........ila hawakuweza.

Jioni ya siku ile nikapiga simu tena, nikaambiwa jmaaa bado hali yake sio nzuri, nikaongea na ndugu zake na bado nikasisitiza wampeleke hospital, Kaka yake akanijibu kuwa ni vyema niende kwanza nikamuone then mambo ya hospital yatafuata, Siku ya Mechi ya Kazier Chiefs na Simba SA bikajisemea moyoni wacha hii mechi ikiisha niende kwake hata kama ni usiku nikamchukue nimpeleke hospital.

Mechi iliish akwa Simba kufungwa, nikasema wacha tu nikalale muda huu nitaenda asubuhi nikamchukue nimpeleke hospital maana ndugu zake walikua wanasema amerogwa hivyo sikutaka sana kuingilia mambo ya ndugu japo mkewe alinielewa.

Asubuhi saa kumi na moja moja kuna namba ngeni ilinipigia mara mbili ila sikusikia simu, saa 12 asubuhi nikaamka nisikilize DW nikaona missed calls, nikawa najiiliza huyu anayepiga simu mida hii nani? Kupiga ile namba nikapokelewa na KILIO cha Mwanamke, dah nilikufa ganzi aiseeee....

Pengine ningeacha kwenda mpirani jana yake ningeweza kumuokoa Jamaa......Hii scenerio bado mbichi kabisa, nimeshiriki kila kitu kwenye msiba wake but naona nina hatia kubwa sana. Pumzika kwa amani Kaka.
Ulithamini mpira kuliko rafiki yako!?
 
Naelewa mkuu lakini "ninge" haiwezi kutoka akilini mwangu!
Kwa hiyo ndugu kedekede ulipewa taarifa kwa ajili ya kuzingatia tu. Ujue tu kwamba jamaa ana mpango wa kujiua. Ila wewe hukuwa na kauli yoyote ya kuidhinisha au kuzuia kujiua. Kwa hiyo kwa sasa wewe umebeba mzigo mzito usiokuhusu, kwa vile hukuwa sehemu ya maamuzi.
 
Asante mkuu kwa maneno yako ya faraja na ya kunizidisha nisonge.Nimejifunza mengi kutokana na kuondoka kwake,nimejifunza nichukue hatua kwa mtu mwingine akinishirikisha jambo kama hili tena.Kusahau ndio imeshindikana mkuu.Namuona hadi leo,nahisi kuna wajib sikuuitimiza katika kumshauri kwangu.
Siku ya tukio nilienda kwenye harusi ya mfanyakazi mwenzangu alikuwa anaoa.Rafiki yangu huyo aliwapigia simu baadhi ya rafiki zake wengine kuwaaga,simu yangu niliisahau nyumbani siku hiyo sikwenda nayo kwenye harusini.Niliporudi alfajiri nilikuta missed calls nyingi sana,lakini kwa vile ni alfajiri ilikuwa nikasema nilale nitapiga kesho yake asubui.12 asubui nikagongewa mlango ya taarifa ya msiba.
Nililia sana,kwenye msiba wake nilmkumbatia mama yake nikalia sana na kumuomba nsamaha.Majibu ya mama yake aliniambia sina cha kuombea msanaha nilikuwa mtu mzuri sana kwa rafiki yangu.Laiti ningepokea ile simu nikaongea naye,laiti angeongea na mimi,labda yasingetokea hayo yote!
Dah I feel ur pain,pole sana
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.

Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
Kubali ulikosea na nisamehe nafsi yako, hii ndio njia ya kutoka hapo ulipo, usipojisamehe itakuandama maisha yako yote
 
Naelewa mkuu lakini "ninge" haiwezi kutoka akilini mwangu!
Kübler-Ross alitoa modeli ya hatua tano za kuomboleza. Kwa modeli hiyo, inawezekana "ninge" zinaashiria hatua ya tatu ya modeli hiyo.

Modeli ya Kübler-Ross inataja hatua tano:

1. Kukanusha (Denial)
2. Hasira (Anger)
3. Kubembeleza (Bargaining)
4. Sononi (Depression)
5. Kukubali (Acceptance)

3. Kubembeleza (Bargaining)
Hapa mtu hutamani hali irudie kama ilivyokuwa hapo kabla.

"Kama ningeongea naye kuhusu kujiua asingejiua."
"Kwa kuwa sikuongea naye kuhusu kujiua mimi ndie niliyesababisha ajiue."
"Ningeweza kurudisha muda nyuma, ningeongea naye kuhusu kujiua."
"Mtu yoyote mwingine akitaja kujiua, nitatenda tofauti na siku ile rafiki aliponiambia."

Ukiona vema, kawaone washauri wa unasihi kwa msaada wa kitaalam.
 
Kübler-Ross alitoa modeli ya hatua tano za kuomboleza. Kwa modeli hiyo, inawezekana "ninge" zinaashiria hatua ya tatu ya modeli hiyo.

Modeli ya Kübler-Ross inataja hatua tano:

1. Kukanusha (Denial)
2. Hasira (Anger)
3. Kubembeleza (Bargaining)
4. Sononi (Depression)
5. Kukubali (Acceptance)

3. Kubembeleza (Bargaining)
Hapa mtu hutamani hali irudie kama ilivyokuwa hapo kabla.

"Kama ningeongea naye kuhusu kujiua asingejiua."
"Kwa kuwa sikuongea naye kuhusu kujiua mimi ndie niliyesababisha ajiue."
"Ningeweza kurudisha muda nyuma, ningeongea naye kuhusu kujiua."
"Mtu yoyote mwingine akitaja kujiua, nitatenda tofauti na siku ile rafiki aliponiambia."

Ukiona vema, kawaone washauri wa unasihi kwa msaada wa kitaalam.
Asante mkuu kwa kunielewesha na kunifariji
 
Back
Top Bottom