Nilifanya mapenzi kinyume na maumbule 2016, mwaka huu imemfanya mchumba wangu kuniacha kabla ya ndoa!

george aloyce

JF-Expert Member
Aug 22, 2017
1,177
1,823
Kaka, kuna kitu umeniandikia leo kimenigusa sana, hiyo ishu ya kuwa karibu na marafiki kwamba rafiki yako ndiyo kila kitu, mimi imenikuta na naumia mpaka sasa sijui kwanini siku zote sikushtuka wakati nakusoma na ulishaandika tangu mwaka 2017 nakusoma.

Iko hivi, mimi ni yule mtu ambaye siwezi kufanya kitu bila kumuambia rafiki yangu, nina rafiki yangu mmoja ambaye alikua dada yangu, ananisaidia kwa kila kitu na kweli ni mtu nilikuwa namuamini sana. Katika mahusiano alikuwa ni mshauri wangu mkuu hivyo nikimpata mwanamume ni mpaka amkubali ndiyo naendelea naye kwenye mahusiano, hata kulala na mwanamume alikuwa anipangia yeye.

Lakini yeye alikuwa haniambii mambo yake yanayohusu mahusiano yake ukiyajua ni kwa juujuu, anaweza kuanza mahusiano mpaka anaachana na mtu lakini hakuniambia. Ila mimi kama nikimpata mwanamume nisipomuamia basi inakuwa shida ataongea mpaka basi. Ukiwa na mahusiano atatafuta kila kitu cha kubaya cha mwanamume mpaka utamuacha, yaani unaweza kukuta mwanamume mko vizuri basi ataanza kukwambia nilimkuta mlimani city na mwanamke, hata si uongo hujui ni nani lakini atakutumia mpaka picha yuko an amwanamke!

Ukitaka labda kumuacha atahakikisha anakwambia na maneno ya kumuumbua ambayo yatamchoma mwanamume. Mwaka juzi 2022 nilikutana na huyo kaka yuko TRA nilipomwambia tu kwamba yuko TRA niliona kama hana raha, akaanza kunambia wakaka wa TRA ni malaya sana kuwa makini, mara mdogo wangu huyo si mwanamume sijui hiki sijui kile yaani kila siku anakuja kunichomekea kwa mabaya.

Lakini hakupata kitu chake hata kimoja na kila alipokuwa ananishauri mimi niliona kama vile si sawa, nikaendelea naye mpaka mwaka jana miezi 9 mwanamume akaja kujitambulisha ikabaki kunivalisha pete na mahari. Lakini ndiyo urafiki ukawa kama umeshaisha nikaona kama bibiye anakuwa hanitafuti yaani ilikuwa kama tumegombana.

Hapo mimi nikaanza kumtafuta, nikahangaika kumjulia hali lakini yeye hajali. Mwezi 11 nikaona kama karudi kuwa karibu na mimi, ila nikaona mwanamume kama amekata kamba, akawa hapokei simu zangu mara "nitakutafuta" mpaka nikahisi kuna kitu. Kumbuka hapo kaja kwetu na mipango ni kuja kutoa mahari mwezi 12 ili mwaka huu tufunge ndoa.

Nikawa nazani ni kitu gani kuna siku namtafuta mwanamume na kumkomalia aniamie uwkeli ninaambiwa kuwa "mimi sisi wezi kuendelea tu na wewe tafuta mtu mwingine". Namuuliza shida nini kwani kila nikimuuliza nimekosea wapi sijui basi nikalazimishai mpaka akaniambia, "mimi najua watu kama nyie hamuwezi kuacha siweiz kukuoa halafu uanliwa na watu wengine".

Namuuliza watu gani, akanijibu "wewe si ulishawahi kufanya mapenzi kinyume na maumbile?" Namuambia hapana, akanisikilizisha voice note zangu nikiongea na rafiki yangu.

Kuna kipindi niko chuo kuna baba nilikuwa natembea naye, sasa mambo ya kuomba pesa akawa ameniomba mapenzi kinyume na maumbile, mimi sijawahi kufanya nikaongea na shoga yangu akaniambia mbona kila mtu nafanya kawaida fanya ule hela. Nikafanya, sikufurahia lakini unajua hela nikafanya kidogo nikaja kuchoka wakati baba alikuwa anataka kila siku nikaona taniharibu mimi bado mdogo nikaacha kabisa, sasa kila kitu nilikuwa namsimulia shoga yangu.

Niliisha sahau kwani ni mwaka 2016 hivyosikua hata nakumbukana huo mchezo nishaacha, ila kuna siku rafiki yangu alinipigia simu hapo ndiyo alitoka kuninunia baada ya mimi kuchumbiwa akawa ananiambia nimekutana na yule X wako. Namuuliza yupo ndiyo ananikumbushia mambo ya huyo mtu.

Katika kuongea ananiuliza "hivi huja miss tu?" Nikajibu "mimi ulikuwa utoto siwezi kufanya vitu kama hivyo", akaniuliza "kama mume wako atataka utafanyaje?" Nilichokosea nilimuambia "mimi ni bora kuchepuka nifanye huko kwingine lakini si na mume wangu atanidharau." Sikujua alikuwa ananirekodi na baada ya hapo kamtafuta mwanamume wangu kamtumia voice note, yaani hata hakujali kama nitajua kua ni yeye kaniharibia!

Mwanamume akaniambia "kwaheri, siwezi kukuamini tena wakati umeshasema hutafanya na mimi utafanya na mchepuko, unafikiri nikueleweje?" Kaka, sikua na namna, sijui hata kujitetetea ni kulialia tu, rafiki yangu namuuliza ananiambia "kaka wawatu mstaarabu hivyo ulitaka aoe malaya?" Nimekubali kuachika na nimejifunza, ila marafiki hapana, nimeacha kuongea kila kitu kwa rafiki yako, nilivyokuwa namuamini sina hamu tena.
 
Hakuna siri ya watu wawili kamwe Dunian la mke na mume tu. Pili hii ni dunia ya wivu chunga kila isemacho kwa watu wako wakaribu. Tatu hem fikiria mwezako hana mume au anaye ila nimuuza chipsi jevatarizika wewe ukaolewe na professor?. Chunga sana siri zako kwawatu mwenye tabia njema niwewe peke yako na wakumuamini niwewe peke yako. Achana na huyo rafiki yako endeleza maisha yako mengine go on
 
downloadfile.jpg
Asante kwa kushiriki umejitahidi
 
Back
Top Bottom