Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

kedekede

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
5,298
7,646
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.

Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Lakini na wewe! Asa mtu kaugua kwa mapenzi ya Mungu kachukuliwa mtanzania anahusikaje apo
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Unataka kuharibu uzi huu sasa!!
 
Wamakonde wana kauli zao wanasema "we live once".
Ukiwa karibu na mtu anayekuamini, jaribu kutompuuza, jikaze hata kama unahisi huna msukumo, madhara yake ni kuja kupambana na nafsi yako kama hivi.

Watu wengi tunasumbuliwa na ubinafsi tu, na kama ukijaribu kujihusisha kutatua matatizo ya wengine, amini nakwambja utakuwa mtu mwenge furaha sana, tena itakuwa maradufu endapo utaona kuna watu wanafurahi kwa sababu yako.

Ili nafsi yako ipone, anza kuishi kama jamaa yako, hakikisha hakuna mtu anakuwa na huzuni mbele yako, muulize, mpe ushauri, muekekeze. Utasaidia wengi na kujiona ulivyo muhimu.

Mimi huwa napenda sana kupiga story na watoto wa kike,huwa nawaeleza mambo mengi tu kuhusu mahusiano, nguvu ya mwanamke na hata uwezo walio nao katika dunia hii.
 
"Guilty Consciousness"
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM , its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Mbona tayari dalili zimeanza.

Ndio maana niliwaambia wapuuzi fulani, inawezakuwa jamaa huyu alikukwaza kwa namna moja au nyingine, kitendo cha yeye kufa na bado unamtukana unajitafutia ugonjwa mbaya sana wa majuto.

Kifo ni form nyingine ya maisha ya kiumbe, hatujui labda kinapewa uwezo zaidi ya huu tulio nao,au kinakuja kwa namna tofauti hapa hapa duniani tena.
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Umetia gundu uzi wa mwenzio ona sasa unaaza kudoda.
 
Unajiuwa ili iweje!
Mkuu acha tu. Nakumbuka miaka ya 90 huko maeneo ya mburahati barafu. Kuna mtu alijinyonga, tukaenda kuona, tulivyorudi mmoja wa mdada tulioenda nae alikuwa Nesi akatoa kauli kuwa "mimi siwezi kujinyonga yani".

Baada miezi kadhaa yule Dada alijiua kwa kujikata koromeo! Inasemekana alikorofishana na shemeji yake.

Kauli yako imenikumbusha huu mkasa.
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Aisee Katika Yatima wanaoteseka wewe ni Kiongozi wao,kila mahali unamtaja huyo Hayati.
 
"Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa (Mtakuja kujionea wenyewe )
yaani tujione wenye hatia kwa kifo cha muuwaji ndio unatupandisha hasira tukimuwaza ben lisu na azor
 
Back
Top Bottom