NAJUTA SANA: Nilizaa nje ya ndoa, mke wangu haniamini tena. Natamani siku zirudi nyuma

Naona mnajaribu kumpa moyo mwenzenu kuwa ni kawaida. Yes ni kawaida, lakini SI KWAKE. Dhamiri yake iko hai ndo maana inamshtaki. Na dhamiri ikikushtaki si rahisi mambo yakaenda. Anajiona amelose pakubwa.

Sio siri, as a woman, naelewa huyu mwanamke alichopitia. Unampa mtu ushirikiano wote, unakuwa mwaminifu, unakuwa a wife package na unajitahidi as hard, lakini unapokea surprise yako, inauma.

Ila MUNGU hasinzii wala halali. Anajua unayopitia. Kama alisababisha nyinyi kuwa pamoja, anaweza kurestore that broken home. Mlitakiwa kuwa mahali fulani, na hao watoto wanatakiwa kufikia destiny zao, na shetani ameliona ndo maana anajitahidi kuwatoa kwenye reli.

Rudini msalabani. Hakuna linaloshindikana kwake. Nawaambia ukweli. Muombeni Mungu awafinyange upya, huo moyo uliojeruhiwa utengenezwe upya. God can fix and ammend broken stuff ambazo mwanadamu wala technology haiwezi. Trust in the work of Jesus at the cross. God can do what you can never imagine. Ask HIM to fix your home. Mnayo ndoa nzuri sana, its just a test of time, na mtalishinda hili. Pole sana kwenu wote. Usikosee tena sasa.
 
Sijaona kosa lolote hapo,,yaani nimkane mwanangu kisa mwanamke? Hupaswi kujutia lolote. Labda kama wewe unategemea kipato cha huyo mwanamke kimaisha. Be a man.
Tupo wengi tuna watoto nje,
Cc Equation x
Kuzaa nje si kosa, kosa ni kuendeleza yale mahusiano ya nje; akifikisha miaka 55+ ataona umuhimu wa kuwa na watoto, muhimu ni kuwapa msingi sahihi tu.
 
Naona mnajaribu kumpa moyo mwenzenu kuwa ni kawaida. Yes ni kawaida, lakini SI KWAKE. Dhamiri yake iko hai ndo maana inamshtaki. Na dhamiri ikikushtaki si rahisi mambo yakaenda. Anajiona amelose pakubwa.

Sio siri, as a woman, naelewa huyu mwanamke alichopitia. Unampa mtu ushirikiano wote, unakuwa mwaminifu, unakuwa a wife package na unajitahidi as hard, lakini unapokea surprise yako, inauma.

Ila MUNGU hasinzii wala halali. Anajua unayopitia. Kama alisababisha nyinyi kuwa pamoja, anaweza kurestore that broken home. Mlitakiwa kuwa mahali fulani, na hao watoto wanatakiwa kufikia destiny zao, na shetani ameliona ndo maana anajitahidi kuwatoa kwenye reli.

Rudini msalabani. Hakuna linaloshindikana kwake. Nawaambia ukweli. Muombeni Mungu awafinyange upya, huo moyo uliojeruhiwa utengenezwe upya. God can fix and ammend broken stuff ambazo mwanadamu wala technology haiwezi. Trust in the work of Jesus at the cross. God can do what you can never imagine. Ask HIM to fix your home. Mnayo ndoa nzuri sana, its just a test of time, na mtalishinda hili. Pole sana kwenu wote. Usikosee tena sasa.
Tunavoona mitazamo ya wanawake tunajifunza zidi sisi wanaume kwenye hili suala coz we get to see your perspective.
Swali la kizushi, hapo jamaa anasema wife ako na mbanga zake hana time na msela, sasa akianza maombi ya kukemea pepo si ndo atamtema kabisa??
 
Tunavoona mitazamo ya wanawake tunajifunza zidi sisi wanaume kwenye hili suala coz we get to see your perspective.
Swali la kizushi, hapo jamaa anasema wife ako na mbanga zake hana time na msela, sasa akianza maombi ya kukemea pepo si ndo atamtema kabisa??
Mambo ya rohoni yanaeleweka kwa jinsi ya rohoni. Huyu mwanamke ana majeraha ya moyoni, haya hayaponagi kwa jinsi ya kimwili, only GOD can do this. Unafikiri jamaa anatakiwa kukemea...never, anatakiwa aingie katika program ya toba ya muda mrefu. Ni mwendo wa toba tu.

Kuna mtu kashauri vizuri sana kule juu. Aintergrate both methods. Aanze kama kumtongoza upya mke wake. Aoneshe tena interest na mke wake. Asijifanye anaweza kupambana kwamba yeye ni mwanaume. Kama mke kabeba kisasi atakua anatwanga maji kwenye kinu. Aonyeshe efforts za kuijenga familia yake tena upya. Aapply efforts both kimwili na kiroho. Akifix hapa, michongo itanyooka.

Mwanamke akiwa na kinyongo afu umemkoroga wewe, na anafanya majukumu yake kama kawaida..wewe mwanaume ndo utapata tabu. Mnataka amani tafuteni amani na wake zenu. Hasa kama una mke mzuri Mungu amekupa, kaza fuvu na jione unaweza kufight mwenyewe...utajua hujui.

Kuna kipindi mshua alishampigaga bimkubwa wangu tukio kama hili, maza akagundua mdogo wangu wa nje akiwa na 12 years..basi bimkubwa akawa anaishi na sononeko, heheeeeee...mambo yalipinda nyumbani kwa miaka 10, mpaka mama alipoanza kuitafuta neema ya Kristo na kumsamehe mshua ndo mzee mambo yakawaga sawa sawia. Na kuanzia kipindi kile ndo mpaka leo wako vizuri sana Glory to God. Anayedharau ni sawa..kila mtu ana itikadi zake. Siwezi kumuaminisha mtu.
 
Mambo ya rohoni yanaeleweka kwa jinsi ya rohoni. Huyu mwanamke ana majeraha ya moyoni, haya hayaponagi kwa jinsi ya kimwili, only GOD can do this. Unafikiri jamaa anatakiwa kukemea...never, anatakiwa aingie katika program ya toba ya muda mrefu. Ni mwendo wa toba tu.

Kuna mtu kashauri vizuri sana kule juu. Aintergrate both methods. Aanze kama kumtongoza upya mke wake. Aoneshe tena interest na mke wake. Asijifanye anaweza kupambana kwamba yeye ni mwanaume. Kama mke kabeba kisasi atakua anatwanga maji kwenye kinu. Aonyeshe efforts za kuijenga familia yake tena upya. Aapply efforts both kimwili na kiroho. Akifix hapa, michongo itanyooka.

Mwanamke akiwa na kinyongo afu umemkoroga wewe, na anafanya majukumu yake kama kawaida..wewe mwanaume ndo utapata tabu. Mnataka amani tafuteni amani na wake zenu. Hasa kama una mke mzuri Mungu amekupa, kaza fuvu na jione unaweza kufight mwenyewe...utajua hujui.

Kuna kipindi mshua alishampigaga bimkubwa wangu tukio kama hili, maza akagundua mdogo wangu wa nje akiwa na 12 years..basi bimkubwa akawa anaishi na sononeko, heheeeeee...mambo yalipinda nyumbani kwa miaka 10, mpaka mama alipoanza kuitafuta neema ya Kristo na kumsamehe mshua ndo mzee mambo yakawaga sawa sawia. Na kuanzia kipindi kile ndo mpaka leo wako vizuri sana Glory to God. Anayedharau ni sawa..kila mtu ana itikadi zake. Siwezi kumuaminisha mtu.
I understand unachosema. But nisaidie kidogo kwenye hili suala la imani, umesema this giy ajae kwenye toba n.k, but hyo yoote ina faida gani kama huyu mwana.ke bado ako na uchingu na kusononeka.?
Wouldn't it be better kama huyo mams pia angeenda kupiga ma toba pia?
 
Kwa nini?
Mwanaume kumletea mtoto ni vizuri zaid kuliko angemletea maradhi.
Mwanamke si mtu wa kuuachilia moyo wake ni mtu wa kubeba vitu moyoni tatizo.

Kutokumshirikisha mume wake kama zamani tayali inaonyesha katengeneza matabaka kwa familia kitu ambacho ni cha kijinga.

Mtu kumkasirikia mume ambae tayali amekiri kosa na kuonyesha kujuta hiyo ni chuki na inamaanisha hajaubeba udhaifu wa mwenzie na kumrekebisha ila alichoamua ndicho kitachokuja kumtesa zaid mbele.

Somo alilopewa na kungwi na mama ake halikumuingia.
 
Habari,
Ngoja nianzia mbali kidogo mpate kuelewa mke wangu ni mtu wa aina gani. Na ilikuwaje mpaka nikazaa nje.

Mimi na mke wangu tulikutana kwenye kongamano la injiri kipindi namaliza chuo yeye alikuwa anasoma chuo kingine tofauti na chetu.

Ni mtu mpole sana niseme ukweli, na anavaa mavazi ya heshima sana, Nilitengeza nae urafiki mpaka kuingia kwenye mahusiano. Niseme ukweli kipindi bado sijamuoa alikuwa ni mtu wa kupenda maendelea sana tena maendeleo ya kushirikiana.

Nilikaa nae kwenye mahusiano kama miaka 6 hivi kisha baadae tukaamua kufunga ndoa takatifu. Nikili kuwa kipindi tupo kwenge uchumba au niseme urafiki nilikuwa sijawahi mgusa kabisa kwani alikuwa ni mtu mpole sana. Mimi nilikuwa na michepuko yangu.

Kipindi tumeanza ndoa yetu, mke wangu yeye wala hakuwa Mchoyo mshahara wake yeye na pesa zake zingine alikuwa anaweka mezani, kitu hiki kilipelekea mpaka mimi kumuamini mke wangu na mimi nikaanza kuweka pesa mezani na kujadili nini cha kufanya tupate maendeleo katika familia yetu itakayokuja.

Mke wangu yeye ni mtu wa kuchakarika sana, na alikuwa anapenda kufanya sana biashara za kushirikiana na mimi mume wake. Kusema ukweli tulikuwa tunainuka kiuchumi kabisa maana nilikuwa naona hali inabadilika katika ndoa yetu hasa kiuchumi,
Nilipanga mengi sana na mke wangu , nilijivunia kuwa nae sana, niliona nimepata, japo ndo kipindi kile ilikuwa still changa.

Sasa baada ya mwaka 1 na miezi 2 mke wangu alibeba ujauzito wangu, ujauzito ule tangu dalili zilipoanza ulikuwa unamsumbua sana mpaka kutafuta mfanyakazi kusaidia kazi. Baada ya miezi kama 4 hivi ya ujauzito, sisi wanaume si unajua bwana kikombe kilijaa maji maana ni miezi kadhaa sijakutana na wife sababu ni ujauzito wangu ule. Nilikuwa navumilia tuu.

Sasa karibu na office yetu kulikuwa na kampuni moja hivi inaagiza vitu china na kuuza, mara nyingi vitu vya home nilikuwa nanunua pale. Kulikuwa na mdada mmoja nilizoeana nae, yeye alikuwa anapokea wageni na kuwaonyesha bidhaa. Kipindi cha ujauzito mazoea yaliongezeka mpaka kubadilisha namba na yule dada. Niseme tu ukweli kuwa niliomba sexy kwake, mimi kwangu kisingizio ni hali ya mke wangu. Nilianza kukutana naye maeneo ya nyumba za wageni tulikuwa tunatumia kinga. Mchezo humu uiliendela mpaka mke wangu anajifungua.

Mimi nikaona mahusiano na mchepuko yameisha tayari kwa sababu mke wangu ashajifungua tayari, nilisitisha mahusiano na mchepuko.
Ila kumbe mke wangu alikuwa anamshono ulitokana na kujifungua . Home na alianza kukalia maji yaliyochanganywa na dettol. Lakini baada ya mwezi mmoja alikuwa still anaumia wakasema anakinyama kimeota kwa hio arudi hospital akashonwe tena, mimi daaa.
Siku namsindikiza hospital nilipanga tena kukutana na mchepuko wangu. Nilivyomuacha hospital mke wangu jioni nilikutana na mchepuko wangu yule kwenye bar moja hivi. Sasa kipindi tunaondoka tukajikuta kunanyanduana kwenye gari kusema ukweli sikutumia kinga kabisa.

Nilimpeleka mpaka sehemu yeye aliposema nimuache, si kujua maisha anayoishi wala kwao sikujui.
Mke wangu baada ya kushonwa tena na kurudi home, mimi niliendelea kukutana na mchepuko kwa mwezi mmoja.
Siku moja aliniambia siku zangu sizione , daaa maneno yale nilishituka sana .
Nikamwambia mimi ni mume wa mtu akasema sawa ila ninahisi ni mjauzito. Mimi daa kusema ukweli hamu naye ilikata kabisa, nikaacha kukuatana nae tena. Nilifikili anatania ila siku zinavyoenda tumbo linatoka nje.

Mke wangu alivyopona tuliendela na maisha huku mchepuko anaujauzito wangu.
Maisha na mke wangu yalikuwa mazuri sana na mafanikio, mchepuko nilikuwa namtumia pesa za kumsaidia tuu, baada ya kujifungua hata mtoto sikwenda kumuona nilikaa kama miezi 5 hivi sikwenda hata kwao.
Mke wangu alikuwa hajui kabisa, mimi na mke wangu tulipanga vingi sana kuhusu maisha yetu, na mafanikio yalikuwa yanatimia kabisa kwani nilikuwa nayaona haya mlangoni na mengine yanangia kabisa.

Siku moja nikasema ngoja nikamuone kwake huko.
Aisee yule dada kumbe anaishi maeneo ya uswazi kabisa , yani ni mtahani kwa waswahili kabisa, waswahili wenyewe wale, nyumba mbanano hata pikipiki haipiti, mimi daa ndo nimezaa na huyu, niliumia sana tena sana ndo mwanzo wa kuanza kujuta, binti anaishi na mama yake tuu, na mama yake ni mswahili kweli kweli, yani hata home wakimuona watanishangaa sana.

Niliondoka na kurudi home namawazo sana huku mke wangu hajui, nilikaa kimya kama 2 years huku maisha na mke wangu yanaendela tukiwa tunakuwa kabisa kimaisha, mke wangu alibeba ujauzito mwingine , sikuchepuka kabisa, alifanikiwa kujifungua.

Baada ya miaka 2 tangu mke wangu ajifungue mtoto wa 2, mtoto wa mchepuko alikuwa miaka 4.

Mimi niliona daa sio vyema mtoto wangu kabisa yule aishi kule kwenye mazingira yale ya mtaani tena uswazi.
Kuna siku moja nilikaa mpaka 3 night kwa niliezaa nae. Daa mazingira ni hovyo sana na kelele nyingine, watu wanapita dirishani wanatukana matusi, maisha ya uswazi mnaelewa jamani.

Mimi niliona ngoja nimshirikishe mother, nipokee ushauri mama aliniambia ni kweli kama mazingira sio mazuri mchukue tuu ila atapata kuzoeana na wenzie mapema. Ila alinisisitiza sana kutengeza kwanza vizuri na mke wangu kuepuka madhara baadae. Niliongea mpaka na viongozi wa dini, kusema ukweli walinikaripia sana kwa sababu ni uzinzi nilifanya. Wakaniambia tuu ni damu yako ongea na mke wako tuu.

Mimi niliamua kwenda kufunguka kwa mke wangu, Nilitanguliza msahama na majuto kwa wife. Niliongea nae sana kuhusu mtoto wa nje na kuacha mahusiano na mama mtoto na ishu ya kumchukua mtoto tukae nae. Mimi sikufukilia madhara yatakayo tokea baadae sikufikilia hilo.
Mke wangu yeye alijibu tuu SAWA HAKUNA SHIDA NI MTOTO WAKO NA ATAENDELA KUWA WAKO TUU.

Kusema ukweli sikufikilia labda mke wangu atapata maumivu kiasi gani mimi nilivyoona yeye kakuabali mimi nikaona sawa. Nimwambia mother akasema kama kakubali sawa mchukue tuu ila kuwa karibu na mtoto.

Baada ya kama wiki nilimchukua mtoto japo mama yake alikuwa mgumu ila nilimchukua, na kuishi nae home.

Ila uwezi amini , ukaribu na mke wangu ulikufa kabisa , si ukaribu wa ndoa. Namaanisha ushirikiano kama Wanandoa.
Kipato chake sikukiona tena , mambo yote tuliokuwa tunashirikiana hasa ya kimaendelo na kiuchumi zilishia kabisa, ndani ya kama mwaka mmoja hivi niliona kipata ndani kimepungua kabisa, nilijua shida ni ile ishu, nilijaribu kukaa na kuongea nae tena sana, yeye anasema kuwa yeye yupo sawa hana shida. Nilijaribu kupambana mimi mwenyewe na maisha ila wapi ni vijipesa vidogo tuu ndo vinaingia ndani na mshahara wa kazini tuu.
Mke wangu yeye yupo na mambo yake haniusishi kabisa mimi.

Sometime nikawa najipa tuu moyo kuwa mimi ndo me ninatakiwa kurisha familia yangu, naamua kusonga mbele ila mambo yanaenda kawaida na mambo yangu mengi wanaanguka, mishe hacienda kabisa.

Natafuta ushauri kwa watu wa ninaokutana nao kwenye bar na sehemu zingine , wengi wanasema tuu ulizingua mara nyingi watoto hao tunawaacha kwa mama zao huko huko, kwani ulivyofanya hivyo umemwonyesha mkeo ushahidi kuwa ulimsaliti tena ukamletea home kabisa ushahidi. Wengi wanasema tuu usaliti unauma sana huyo mkeo anaumia mpaka kesho. Wananiambia tuu potezea kaka.
Ila ni kitu ninakijutia sana sio kwamba ninamchukia mtoto hapana nachukia ule uzinzi nilifanya .
Nilimueleza mother aliniambia tuu kama mtoto anaishi nae fresh hakuna shida kubali matokeo tuu.

Sometime natamani kuona siku zinarudi nyuma ila haiwezekani, Najuta sana maana naona maisha yamedrop sana. Yale maendeleo hakuna kabisa kama awali.

Sasa nina umri wa miaka 42,
Maisha napambana tuu mimi mwenyewe kama Baba wa familia sioni ushirikiano kutoka kwa mke wangu, lakini nimejipa moyo kuwa mimi ndo mwanaume nitalisha familia yangu. Ila kinachoniuma ni mahusiano wa kushirikiana na mke wangu yamekufa kabisa. NAJUTA SANA.

Marafiki zangu wengi wapo na mafanikio sana na wake zao nawaona hata jinsi wanavyoishi.
Kuna rafiki yangu mmoja wa karibu sana mwezi wa 3 aliingiza Toyota land cruiser LC300 GX la kwake na mke wake GX.
Huyu ni mmoja tuu wapo wengine wapo fresh sana , najua wapo hivyo kutokana na mahusiano na wake zao hasa ya kiuchumi.

Mimi hapa ni na ka harrier changu kimetengenezwa miaka 14 iliyopita naona hata aibu kuwakaribisha hata home friends wangu.
Na Hata kukutana nao tuu.

NB; JAMANI WANAUME WENZANGU TUTULIE KWENYE NDOA ZETU HASA TUNAPOPATA MKE MWENYE MIBARAKA KWENYE NDOA ZETU. NI MUHIMU SANA UNAWEZA UKAONA STORY ILA MWENZENU YAMENIKUTA.

SOMETHING NAJIRAUMU KUWA NINGEJUA NINGEMUACHA KWA MAMA YAKE NIKABAKI MUUDUMIA.
SOMETHING NAONA NILIKUWA SAHIHI KUMCHUKUA.


Sorry mimi sio mwandishi mzuri, naomba radhi kwa makosa mtakayo baini.
Ulie zaa nae endelea nae kea mkeo pia atakuwa anapigwa nje kwani kisha kutoa thaman
Agakuthamini siku nawe umemfumania
Ulie zaa nae, nae ni mkeo mpe haki zake pia
Ona mazingira anayo Ishi muone e huruma
Usimdharau kutokana na maisha anayoishi ya uswahilin ndo kipato chake kinamtoshereza kuishi huko, ilimrad sio malaya na wala ajiuzi
Mkeo atajirudj baadae kabisa akiona uteseki
We jioneshe huruma huruma uone cha moto
 
I understand unachosema. But nisaidie kidogo kwenye hili suala la imani, umesema this giy ajae kwenye toba n.k, but hyo yoote ina faida gani kama huyu mwana.ke bado ako na uchingu na kusononeka.?
Wouldn't it be better kama huyo mams pia angeenda kupiga ma toba pia?
Ni kweli unachokisema mkuu. Lakini sasa mimi ninaemshauri hapa ni huyu kaka. The power of God atakayoipata ndio itakayopelekea na huyu mams afunguke na kusamehe. Yani Mungu huwa anataka hata mmoja katika wanandoa wasimame vizuri na yeye afu aingie hapo kati na kulisababisha.

Sasa kwa story hii, hii nyumba ina ukiwa, ina utupu, upendo wa kwanza umeondoka, usifikiri kutatokea maendeleo humu. Ninao wajomba, baba wadogo, punde walivyofanya mambo ya mfanano huu, na uchumi wa familia ukacollapse. Ninadhani mpaka leo mama na shangazi zangu wana maumivu kwa sabbu uchumi hauko ok katika familia zao. Mke halali wa kiagano, aliyejitahidi kutembea katika ukamilifu, akiumia afu akalazimika kutulia katika ndoa ili kumuheshimu Mungu, uwe na uhakika kisago cha uchumi ni inevitable.

Huyu mleta mada anatumika katika adhabu ya uzinzi. Na hii hali inamletea sonona. Inamuumiza. Ndo maana kaandika. Angekua anaweza kuhimili asingejisumbua kutype. Hakuna jambo swadakta kama kumpata mwandani wa uhakika..first class wife. Anamtaka mke wa ujana wake back, ili maisha yawe mazuri ndani ya nyumba. Mwanamke ndo mwenye maumivu. So kama alivyofanya efforts kutafutana na mcheps, afanye sasa efforts kuutafuta USO WA MUNGU. Naomba nimuache na mstari wa Isaiah 59:1-21.
 
Ni kweli unachokisema mkuu. Lakini sasa mimi ninaemshauri hapa ni huyu kaka. The power of God atakayoipata ndio itakayopelekea na huyu mams afunguke na kusamehe. Yani Mungu huwa anataka hata mmoja katika wanandoa wasimame vizuri na yeye afu aingie hapo kati na kulisababisha.

Sasa kwa story hii, hii nyumba ina ukiwa, ina utupu, upendo wa kwanza umeondoka, usifikiri kutatokea maendeleo humu. Ninao wajomba, baba wadogo, punde walivyofanya mambo ya mfanano huu, na uchumi wa familia ukacollapse. Ninadhani mpaka leo mama na shangazi zangu wana maumivu kwa sabbu uchumi hauko ok katika familia zao. Mke halali wa kiagano, aliyejitahidi kutembea katika ukamilifu, akiumia afu akalazimika kutulia katika ndoa ili kumuheshimu Mungu, uwe na uhakika kisago cha uchumi ni inevitable.

Huyu mleta mada anatumika katika adhabu ya uzinzi. Na hii hali inamletea sonona. Inamuumiza. Ndo maana kaandika. Angekua anaweza kuhimili asingejisumbua kutype. Hakuna jambo swadakta kama kumpata mwandani wa uhakika..first class wife. Anamtaka mke wa ujana wake back, ili maisha yawe mazuri ndani ya nyumba. Mwanamke ndo mwenye maumivu. So kama alivyofanya efforts kutafutana na mcheps, afanye sasa efforts kuutafuta USO WA MUNGU. Naomba nimuache na mstari wa Isaiah 59:1-21.
Umemshauri vizuri kweli. Mleta mada naomba usome hapa kwa hatua ili upate suluhisho la mambo yako. Nami nimepata kitu hapa.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Kilichonishangaza una miaka 42 halafu bado huna akili.
Acha kumuita mwenzio hana akili,
Wewe unavyojiona unazo akili,
Kwenye uzi mmoja nakumbuka ulisema ulivyotoka ughaibuni ulizini na wake za watu ambao ni ex zako eti walikuwa na shida na pesa.

Biblia imesema wazi kuishi nao kwa akili sasa wewe umeshindwa kutumia akili.
Biblia yenyewe imesema azinie na mwanamke hana akili,
Yani wewe unafanya unamuona mwenzio hana akili kumbe wewe mwenyewe upo kundi lile lile.

Hahaha binadamu bhana,
Na PHD yako still hata wewe unazini na mwanamke.
 
Matatizo ni mawili tu hapo.

1. Kumtegemea mke katika kipato
2. Kuwa vuguvugu na kukosa akili ya mahusiano. (Walokole huwa na hili tatizo)

Suluhisho ni moja tu.
1. Kuwa mwanaume mwenye uwezo wa kujisimamia kifedha na kimsimamo.

Kila la heri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom