Najuta kuifahamu stand ya Mwenge

Najuta kuifahamu stand ya Mwenge

Msandawe Halisi

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
647
Reaction score
351
Jana katika mizunguko yangu, nimetoka banana Ukongo mida ya jioni kuelekea Bunju. Kufika Mwenge kukawa na usafiri wa shida sana. Mara gari ya Bunju hiyo.

Abaria tukaanza kufanya mahaba ya kuikumbatia gari toka lango la kungilia mpaka karibu na yanapo paki mabasi ya Tegeta, Bunju ndani ya kituo cha mwenge, sababu konda aligoma kufungua mlango tupande pale yanapo ingilia mabasi.

Baada ya mlango kufunguliwa likatokea purukushani la kufa mtu kuakikisha kila moja anawahi siti. Ile kufika ndani tu najikagua mifukoni Simu yangu holaa, nikaseach mpaka mifuko ya nyuma holaaa.

Najiangalia mfuko mwingine elfu hamsini hola. Nikachoka ghafla nikafa kiumee kimya kimya huku nikipata upweke wa kukosa kuperuzi JF. kwa bahati nzuri mfuko wa shati kulikuwa na ATM card na elfu mbili.

Ndugu zangu, Naaaaaaaajuuuuuuuuuutttttaaaa kuuuuuuuuiiiifahammuuuu Mweengeee Stand.
 
Dah!!! Kaka nakuelewa sana ukisema hivyo.. Mimi walinibebea passport yangu kaka gari za mwenge hizo hizo waliniona natoka kwenye atm pale posta wakawa wananifuatilia ile naingia kwenye basi naangalia passport hakuna . Nlichoka.. Sema wakaitupa pale kwa muuza vocha akanipigia kesho yake . Sasa hivi nimekoma
 
pole mkuu...ndio majaribu yetu hayo!
 
Hapana Chezeya Mwenge weye! Pale kuna professional wezi in east Africa and central Africa.
 
Jana katika mizunguko yangu, nimetoka banana Ukongo mida ya jioni kuelekea Bunju. Kufika Mwenge kukawa na usafiri wa shida sana. Mara gari ya Bunju hiyo. Abaria tukaanza kufanya mahaba ya kuikumbatia gari toka lango la kungilia mpaka karibu na yanapo paki mabasi ya Tegeta, Bunju ndani ya kituo cha mwenge, sababu konda aligoma kufungua mlango tupande pale yanapo ingilia mabasi. Baada ya mlango kufunguliwa likatokea purukushani la kufa mtu kuakikisha kila moja anawahi siti. Ile kufika ndani tu najikagua mifukoni Simu yangu holaa, nikaseach mpaka mifuko ya nyuma holaaa. Najiangalia mfuko mwingine elfu hamsini hola. Nikachoka ghafla nikafa kiumee kimya kimya huku nikapata upweke wa kukosa kuperusi JF. kwa bahati nzuri mfuko wa shati kulikuwa na ATM card na elfu mbili.

Ndugu zangu, Naaaaaaaajuuuuuuuuuutttttaaaa kuuuuuuuuiiiifahammuuuu Mweengeee Stand.

Du Mkuu hapo mwenge mimi pamesababisha niwe nanunua simu za 40 elfu kushuka chini ni majanga!
 
Kipindi nasoma, kuna siku nimetoka menge naenda Ubungo, mfukoni nina elfu tatu bajeti ya nauli kula na maji. Ile karibu nafika Mlimani city mifuko miupeeee.
Uzuri wake konda alikuwa hajaanza kukusanya nauli, ikabidi nimwombe kazi ya kuita abiria hadi Ubungo ili nisilipe nauli.
Uzuri wake konda alikuwa mwelewa kwa sababu aliona ninavyojisachi baada ya kuchezewa chezo na watoto wa mujini.
So nikachapa mzigo hadi Ubungo na nikaachiwa na sh. 1000 na konda kama mshahara halali.
 
Hujawahi kuibiwa dogo...........watakuibia siku hadi utawapongeza na halafu ukajichoma yako bisbis kujilaumu!

Ah wapi! Mi mtoto wa town wewe. Mwana Abajaro wa zamani. Nimezipiga sana na Kiboko Msheli.

Mbinu zote wanazozitumia nazijua. Sipandi daladala na chochote cha thamani zaidi ya pipi kijiti.
 
Nchi hii :-
Ndiyo maana MVUA zetu majangaaa!!
Ndiyo maana Ukame wetu Balaa !!!!!
Ndiyo maana BUNGE letu vurugu kufa !!
Ndiyo maana MAISHA yetu ni misiba tu !!
Ndiyo maana MFUMKO wa BEI hawshuki !!!
Ndiyo maana TIBA zetu maomukizi sugu !!
Ndiyo maana SHULE zetu Ma-Division " !!!
endelea.........
 
Ah wapi! Mi mtoto wa town wewe. Mwana Abajaro wa zamani. Nimezipiga sana na Kiboko Msheli.

Mbinu zote wanazozitumia nazijua. Sipandi daladala na chochote cha thamani zaidi ya pipi kijiti.
Hahah mwana wa abajato acha woga. Mimi toka mwana 2012 huwa nikipanda daladala nina i phone 4 nai pa na sijawahi kuibiwa . Sijisifii manake najua wanaweza kuniotea kama walivyoweza kunipiga passport ila hii ya kupanda dala dala na pp kijiti manake unawaogopa na mbinu zao huzijui
 
Kipindi nasoma, kuna siku nimetoka menge naenda Ubungo, mfukoni nina elfu tatu bajeti ya nauli kula na maji. Ile karibu nafika Mlimani city mifuko miupeeee.
Uzuri wake konda alikuwa hajaanza kukusanya nauli, ikabidi nimwombe kazi ya kuita abiria hadi Ubungo ili nisilipe nauli.
Uzuri wake konda alikuwa mwelewa kwa sababu aliona ninavyojisachi baada ya kuchezewa chezo na watoto wa mujini.
So nikachapa mzigo hadi Ubungo na nikaachiwa na sh. 1000 na konda kama mshahara halali.

wakuu naona wewe na Nyani Ngabu mmeamua kunivunja mbavu leo, kwa hiyo mwanaume ikabidi umnong'oneze konda abiria wenzako wakashangaa umekuwa mpiga debe!!!..hapo pata picha ungekuwa na kadem halafu na kenyewe kamefulia kwenye pochi kamejaza handkerchief ni vioo tu!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom