Najuta kuifahamu stand ya Mwenge

Najuta kuifahamu stand ya Mwenge

Kuna jamaa yangu moja tulikuwa tumepanga nyumba moja pande za Tangi bovu. Yeye alikuwa ni mtu wa viwanjana sana. Siku moja mida mibovu kashuka pale mwenye. Wahuni wakamdandia, walimpiga roba moja matata sana wakampora kila kitu. Kurudi home akaamka kidogo afadhali. Ile kufika usiku wa saa saba siku iliyofuata aliamka akatumsha wapangaji wenzeke akawa anatueleza aoni vizuri, anaona giza tu, shingo imekataa kugeuka. Usiku huo huo tukamkimbiza masana hospital. Mwenge toka zamani ni noma.

Mkuu umenivunja mbavu, nimecheka hadi nipaliwa ka lite kangu Shukrani sana.
 
Jana katika mizunguko yangu, nimetoka banana Ukongo mida ya jioni kuelekea Bunju. Kufika Mwenge kukawa na usafiri wa shida sana. Mara gari ya Bunju hiyo.

Abaria tukaanza kufanya mahaba ya kuikumbatia gari toka lango la kungilia mpaka karibu na yanapo paki mabasi ya Tegeta, Bunju ndani ya kituo cha mwenge, sababu konda aligoma kufungua mlango tupande pale yanapo ingilia mabasi.

Baada ya mlango kufunguliwa likatokea purukushani la kufa mtu kuakikisha kila moja anawahi siti. Ile kufika ndani tu najikagua mifukoni Simu yangu holaa, nikaseach mpaka mifuko ya nyuma holaaa.

Najiangalia mfuko mwingine elfu hamsini hola. Nikachoka ghafla nikafa kiumee kimya kimya huku nikipata upweke wa kukosa kuperuzi JF. kwa bahati nzuri mfuko wa shati kulikuwa na ATM card na elfu mbili.

Ndugu zangu, Naaaaaaaajuuuuuuuuuutttttaaaa kuuuuuuuuiiiifahammuuuu Mweengeee Stand.
Kinachowafanya muibiwe ni kudhani kuwa haya mambo yapo stendi ya Mbagala tu
 
Wahusika tunaomba mtusaidie ili tatizo la usafiri kwa kweli sisi wapanda dala dala tunapata shida sana
 
nakumbuka enzi za UDA MILANGO MIWILI ,nilikuwa naweka viwembe kwenye mifuko ya suruali
 
Umenikumbusha siku moja
nimeenda taifa kucheki mechi ya Yanga na Mbaya C,ile nakaribia kigari
cha tiketi nikatoa pochi yangu nikachomoa Elfu kumi kumbe watoto wa mbwa wananichora tu. ile kukurukakara ya kugombea foleni hatimae nikafanikiwa kununua.
ile nimemaliza tu kujisachi sina pochi kitambulisho, kadi ya atm pesa kama elf themanini na vingingevyo vimeenda.

Nilichofanya ni kuchana tiketi na kupanda daladala na kugeuza kariakoo,uzuri simu ilipona ndio iliyonisaidia kupata nauli ya kurudi Mbeya.
 
hapo kwenye rangi nyekundu nimecheka sana khaa!!!!!
na wewe Capitalist M umeniacha hoiii nimechekaaa
mwisho CYBERTEQ nimecheka sana ulivomjibu Capitalist M loooh thanks

Jana katika mizunguko yangu, nimetoka banana Ukongo mida ya jioni kuelekea Bunju. Kufika Mwenge kukawa na usafiri wa shida sana. Mara gari ya Bunju hiyo.

Abaria tukaanza kufanya mahaba ya kuikumbatia gari toka lango la kungilia mpaka karibu na yanapo paki mabasi ya Tegeta, Bunju ndani ya kituo cha mwenge, sababu konda aligoma kufungua mlango tupande pale yanapo ingilia mabasi.

Baada ya mlango kufunguliwa likatokea purukushani la kufa mtu kuakikisha kila moja anawahi siti. Ile kufika ndani tu najikagua mifukoni Simu yangu holaa, nikaseach mpaka mifuko ya nyuma holaaa.

Najiangalia mfuko mwingine elfu hamsini hola. Nikachoka ghafla nikafa kiumee kimya kimya huku nikipata upweke wa kukosa kuperuzi JF. kwa bahati nzuri mfuko wa shati kulikuwa na ATM card na elfu mbili.

Ndugu zangu, Naaaaaaaajuuuuuuuuuutttttaaaa kuuuuuuuuiiiifahammuuuu Mweengeee Stand.
 
Last edited by a moderator:
mie waliniibia sim yangu pale stand ya nje nasubiria daladala za Posta

kumbe kanivizia napanda gari kanichomolea sim kwenye mkoba

halafu kumbe konda alikua keshaona kila kitu akaanza ka kunisanifu

hasira zangu ziliishia kwake siku hizi nakuwaga makin sana
 
Pole sana mkuu.
Kinachowafanya watanzania msipange foleni wakati wa kupanda daladala ni kitu gani?
Mbona sisi Nairobi tunapanga foleni kupanda matatu?
Mtaendelea kuibiwa sana hadi mtakapobadilika.
Badilikeni

hii ya kupanga foleni iko poa
lakin hadi watu wazoee yaani ile
ya kugombania imewakaa wengi
 
wanao chomolewa mifukoni wote ni wazembe!
 
Mwenge kulinifanya nione kila mtu mwizi,. Hadi akina dada wanapiga sachi siku hizi! Yaani ni shidaa!
 
Duh,

Umenikumbusha waay back in the days.Enzi za dotcom bubble tunawezesha taifa kuingia mtandaoni.

Napanda basi Mwenge kwenda kazini Posta asubuhi, basi mminyo mminyo hivyo hivyo, kujistukia sina wallet.

Nikajisemea mwenyewe "I have never been pickpocketed in my life, and I ain't starting now".

Basi nikapiga mkwala basi zima likawa lina mtafaruku. Huku kichwani napiga mahesabu ya kukumbuka movements zote za kuingia kwenye basi, nikakumbuka kama kulikuwa na kimkono kimepita hivi. Lakini wakati wa kugombea kupanda basi mminyo mminyo you can't tell, unaweza kufikiri ni movement tu ya kugombea basi, kumbe watu wapo kazini.

Basi katika mtafaruku wa kuamua iweje, gari liende polisi au vipi, nikaona kuna watu wanaanza kushuka.

Ikawa kama inazidisha mtafaruku, this is a crime scene, mnaruhusu vipi watu waondoke?

Mahesabu yangu ya kijasisi yakaniambia nicheze na hawa wanaotoka. Nikataka kubanana nao, nikasema hatoki mtu gari linaenda polisi hili. Enzi hizo Kiranga Kiranga kweli huyu wa leo katulia kidogo.

Basi kuna kitu kikaniambia niangalie chini ya gari.

Kuangalia chini ya DCM, hamadi, wallet limelala limefuba vilevile.

Nikaingia chini sikuamini macho yangu.

Inaonekana kuna mjuba kati ya wale waliokuwa wanatoka aliinyai halafu mkwala wa kwenda polisi ulivyotanda akaamua kuiminya chini hapo kuondoa ushahidi.

Nikachukua wallet yangu nikapanda basi jingine.

Toka siku hiyo wallet inakaa kwenye deep pockets, kama nina overcoat kamwe haikai kwenye overcoat.
 
Hamna wewe...si kwamba nawaogopa. Ni kwamba hao jamaa ni lazima uwe dakika tano mbele yao la sivyo ukijifanya gangwe eti huwaogopi unaweza kula hasara ya kijinga ambayo ingeweza kabisa kuepukika.

Kukurukakara za kudandia daladala unazijua lakini?

Hapo umenena! Usirushe ngumi na kuzua ugomvi huku mfukoni una milioni 3 zako. Utajuta!
 
MKUU sasa hivi hali ni shwari kabisa kiukweli mm bawapongeza sana serikali kwa KAZI nzuri walioifanya Leo hii.yakuwaondoa wale machinga woote wanaotandika bidhaa zao chini na kupanga kwenye meza.

mim mwenyewe sijawahi ibiwa ila kunakibaka alitaka kuniletea za kuleta akiniona wakuja purukushani mpaka nikakanyaga kiatu kilikuwa kimewekwa kinauza ugomvi ukahamia kwa huyo machinga .
 
Hivi mnaongelea mwenge kwenye wizi wa mifukoni! kwa taarifa yenu Arusha ni noma, nafikiri wanaenda hadi kozi.
 
asilimia kubwa wanaiita ndole....hiyo ni maarufu kwa mifuko ya nyuma...
 
Back
Top Bottom