bro_A
JF-Expert Member
- Nov 5, 2015
- 1,371
- 1,063
Tatizo ni kuwa huangalii status yaani hali ya hao wanaume wanaokufata na ukawakubalia....yaani unakubali tu ila ungekuwa unawachunguza maisha yao kazi, biashara yao walau kujiridhisha kuwa nao wana shughuli zao za kueleweka. Wanaume nao siku hizi wanaangalia mahala anapoweza kupata pumziko na kulelewa hivyo uwe unaangalia sana kabla hujaingia ktk mahusiano. Pia umesema una huruma sana haina shida kuwa na huruma kama ndivyo Mwenyezi kakuumba hivyo usibadilike ukaanza kuigiza roho ngumu hapana ila kile unachotoa kusaidia kiwe cha ziada isiguse mtaji au akiba yako. Pia nimeelimika sana kutoka kwako yaani unakuwa na mil 5 bank ila bado unapanda daladala na kula kwa mama ntilie nimependa maisha yako nami nitaiba hiyo mbinu ili kunisaidia ktk maendeleo yangu ya kifedha..
Kifupi dada fikiria aina ya mwanaume unayemtaka sifa unazozitaka ili hao wanaokutongoza basi uweze kuwapitisha ktk chujio dhidi ya vigezo vya mwanaume unayemtaka kama kuna mwenye sifa basi mkubalie. Naona umekuwa ukiwakubalia vijana au wanaume wasio na mipango wa muelekeo wa.maisha ndo maana wanaishia kula hela zako tu.na huenda wengi wamekutongoza kwa dhumuni la kula hela zako na si vinginevyo.
Kifupi dada fikiria aina ya mwanaume unayemtaka sifa unazozitaka ili hao wanaokutongoza basi uweze kuwapitisha ktk chujio dhidi ya vigezo vya mwanaume unayemtaka kama kuna mwenye sifa basi mkubalie. Naona umekuwa ukiwakubalia vijana au wanaume wasio na mipango wa muelekeo wa.maisha ndo maana wanaishia kula hela zako tu.na huenda wengi wamekutongoza kwa dhumuni la kula hela zako na si vinginevyo.