Naionya China, isijaribu

Naionya China, isijaribu

Yaani wabongo bana😂😂😂, unakaa nchi ya ulimwengu wa tatu, kwenye dampo la dunia, unajitia kuwashauri viongozi na serikali ya Russia na China yenye agents hatari wanayoijua hii dunia?
Umekula ugali wako na muhogo umeshiba unakuja kudhani una ijua kesho ya Russia kuliko FSB? Raisi tu wa Russia ni former KGB, serikali ya Ukraine ina agents wengi tu wana leak data...

Unaijua China kuliko MSS? Chinese wana puppets wengi tu serikali ya Taiwan, tunajua machache sana...

Russia wanajua walifanyalo, walishajiandaa, kila kitu kipo calculated...

Kama umeshiba ugali better ukae chini ufuatilie bifu ya Harmonize na Diamond na udaku wa insta, huwezi ijua China au Russia kama agents wao ambao hawalali, wana risk afya zao na maisha yao, wamesomea ukachero na wanaishi ukachero na wanakula kikachero hata mapenzi ni kikachero, wakipumua ni ukachero... Ogopa sana hio...

Kwamba Russia imeingia mtegoni😂😂😂, Huyo ni mbongo, hivi vile vichwa vyote vya wale wazee pale Moscow vyenye mvi, makachero wabobezi toka USSR hawakujua plans za US?😂😂

Inaskitisha sana kwa kweli..
Hatari hiyo mkuu😀
 
Mm nampinga sana Putin kuivamia Ukraine ila siamini kuwa Puttin ni mjinga mjinga. So far kuna mambo mengi ameshaprove kuwa he is smart kwa kiwango cha USA na washirika kutokukurupuka anapodeal naye.

Huenda mtego upo kwenye muda kama unavyosema na kuna member mmoja alishasema Puttin atapigana muda mrefu sana na ni makosa kufikiri atachukua nchi kwa haraka Nyamizi na ni kweli yametokea.

Ila nasema sio mjinga kwa sababu mpaka kufikia sasa ameonyesha kuwa ni smart enough to play along with USA and NATO games. Fuel prices zimekuwa unstable, Food imebidi wakubaliane meli ziachiwe, kuna vikwazo imebidi kuwe na exceptions baadhi ya nchi na hapo ni yeye mwenyewe. Imagine angekuwa na saport ya moja kwa moja ya nchi kama China, Iran, India n.k na wakaamua kusimama nae.

Pamoja na mm kutomtakia mema huyu Puttin huko Ukraine, (Nataka ashindwe awaachie watu nchi yao, kama kuna changamoto diplomacy itumike au njia mbadala za kudeal na mgogoro) lazima tu kukubali kuwa nchi anayoiongoza inahitajika na so far ameonyesha kuhitajika kwake duniani.
Mkuu haya unayosema kwa namna fulani nakubaliana na wewe. Lakin tukubali tu kwamba hasara kubwa anayoipata ni yeye sio Marekani, NATO nk. Kama marekani imeweza mutumia mabilioni ya dola kusaidia nchi mbali mbali aidha kwa faida au vinginevyo ni vipi atakuja kupata hasara leo kwa kuisaidia Ukraine? Kushindana na Marekani sasa hivi ni sawa na kujaribu kumuiga tembo kun.y..a mwishoni utachanika m..
 
Mkuu haya unayosema kwa namna fulani nakubaliana na wewe. Lakin tukubali tu kwamba hasara kubwa anayoipata ni yeye sio Marekani, NATO nk. Kama marekani imeweza mutumia mabilioni ya dola kusaidia nchi mbali mbali aidha kwa faida au vinginevyo ni vipi atakuja kupata hasara leo kwa kuisaidia Ukraine? Kushindana na Marekani sasa hivi ni sawa na kujaribu kumuiga tembo kun.y..a mwishoni utachanika m..
 
Russia asipokuwa makini atajikuta kafilisika na hii vita, vita sio mchezo na ndio mwanzo wa umaskini, sababu kubwa ya kuanguka Russia federations ilikuwa ni matumizi makubwa ya kijeshi wakasahau uchumi, China asiingie vitani huo ni mtego, lakini nilivyoona Pelosi akiingia Taiwan na zile war jets na China hakufanya chochote wakati makombora na meli za kivita za China zinaangalia tuu basi naamini China hataingia vitani maana anajua hasara ya hii kitu
Mkuu China hana ujasiri wa kufanya chochote kwa Marekani, bora muirani ni mwanaume. Akisema hataki marekani avuke mstari huu na kweli marekani akivuka lazima majibu atayapata tena kwa wakati ule ule waliopanga. Hawa jamaa wasingewekewa figisu za kutengeneza masilaha na kumiliki uchumi mkubwa kama China, nina imani wangeisumbua sana marekani.
 
Hamjambo wakuu.

Ndugu wana Jamii Forum baada ya kufuatilia kile kinachoendelea kutokea kule katika mpaka wa kisiwa cha Taiwan, kuhusu mzozo wa China na Taiwan.

Kama ningekuwa na uwezo wa kuwasiliana na uongozi wa China, basi ushauri wangu mkubwa kwao ingekuwa ni kuwaambia wasithubutu kukivamia kisiwa kile.

Ule ni mtego uliotegwa na hawa wababe wa dunia wakiongozwa na baba lao USA.

Ikumbukwe kwamba hata vita ya Ukraine na Russia ilianza hivi hivi, huku Russia ikiwa na uhakika wa kuisambaratisha Ukraine kwa muda wa siku 3 tu au ikichelewa sana ni week. Sasa kinachoendelea leo kila mtu anakiona.

Russia imekuwa ikitumia kila aina ya njia za kijeshi, rasilimali, na jeshi lake la akiba kuimaliza vita hiyo lkn inashindikana.

Leo hii Russia ishatumia kiasi kikubwa cha silaha zake, ishapoteza kiasi kikubwa cha wanajeshi wake, ishayumbisha uchumi wake na kushuka thamani kwa hela yake (na hili ndio USA na nchi zingine za NATO walilitaka) bila kufanikiwa kuiangusha Serikali ya Ukraine wala kuuteka mji mkuu.

Kile kinachoendelea sasa hivi kimetokana na uzembe wa Putin na serikali yake, sasa wanaona yamekuwa magumu kwao, zile siku 3 ikawa week, ile week ikawa mwezi, mwezi sasa imekuwa miezi.

Na kila wanavyoendelea na vita na ndio jinsi wanavyoendelea kupata hasara kwa kupoteza askari, silaha mbalimbali za kijeshi na kudhoofisha uchumi wao.

Na wamarekani wakishirikiana na ndugu zao wa West wataendelea kuijambisha Russia kwa kujifanya wanaitumia Ukraine silaha (japo nyingi ni za kichovu) ili kuichochea Russia izidi kuendeleza mashambulizi na kudhoofisha nguvu zake kwa miaka kadhaa ijayo.

Ni nani kati ya wana NATO asiejua madhara ya kuingia vitani mzimamzima. Leo hii marekani haiwezi kuthubutu kuingia vitani hata na Mexico, japo kijeshi inaweza kutumia hata jeshi lake lililo katika jimbo la California tu kuisambaratisha Mexico, lakn wanaangalia hasara ambayo inaweza kuipata katika vita hiyo.

Marekani inaweza kutuma silaha au vijana wake kadhaa wa jeshi kwenda kusaidia sehem fulan kwa ajili ya masilahi ya marekani ila haiwezi kuingia vitani moja kwa moja kama ilivyofanya Russia.

Ni mara ngapi Iran imekuwa ikiangamiza ndege zisizo na rubani za Marekani, kuzilipua meli za Marekani na pengine kuteka hata meli za washirika hao wa Marekani, lakn kamwe Marekani haikufikiria na haifikirii kuingia vitani, maana inaelewa kuwa vita kuianza ni vyepesi sana lakin kuimaliza ni vigumu.

Sasa inashangaza kuona China pamoja na kuwa na wasomi wengi pamoja na intelejensi kubwa duniani, lakin inataka kuingia mtegoni kama alivyoingia ndugu yake Russia. USA na swaiba zake wana uwezo wa kutoa msaada kwa Taiwan au Ukraine kwa miaka kumi ili mradi lengo lao litimie.
Marekani na swaiba zake sio wajinga, wanajua vizuri kile wanachokifanya.

Na majibu kuhusu uchumi wa Russia na nguvu zake za kijeshi tutayapata baadae baada ya vita kuisha. Kwa sasa bado inachochewa chochewa ili iweze kutumia hata zile silaha ambazo ingetakiwa kutumia pale inapopambana na nchi kubwa kama USA, China, India nk.
Mwisho wa siku ghala la silaha litabaki tupu.

So naionya China kama inataka kuendelea kuwa nchi ya pili kwa uchumi na ya tatu kwa nguvu za kijeshi, basi iachane na wazo la kuivamia Taiwan maana itapoteza nafasi zake zote mbili, kuanzia kwenye uchumi hadi jeshi. Vikwazo itakavyowekewa na wakubwa hao wa dunia vitakuwa sio vya dunia hii, na hapo ndipo atakapoanza kuona madhara ya kuingia vitani kichwa kichwa bila kutumia akili.
Iache iporomoke kiuchumi ili isiwe na hela za kuwajaza wachina africa. wamekuwa kero kila mahali africa hawa wachina. halafu lazima walipe hasara ya kuleta siasa za kupeleka vijana vijijini, kukamata wazururaji na kujenga vyuo vya propaganda.
 
Mkuu haya unayosema kwa namna fulani nakubaliana na wewe. Lakin tukubali tu kwamba hasara kubwa anayoipata ni yeye sio Marekani, NATO nk. Kama marekani imeweza mutumia mabilioni ya dola kusaidia nchi mbali mbali aidha kwa faida au vinginevyo ni vipi atakuja kupata hasara leo kwa kuisaidia Ukraine? Kushindana na Marekani sasa hivi ni sawa na kujaribu kumuiga tembo kun.y..a mwishoni utachanika m..
Mkuu akilihuru Marekani ni nchi kubwa yenye nguvu duniani na hii ni moja ya uthibitisho mwingine kuwa Urusi si wakubeza sana sababu USA anavyodeal nae ni tofauti kidogo na anavyodeal na nchi nyingine. Hata ishu ya China vs Taiwan angalia USA alichofanya halafu ulinganishe na suala la Ukraine vs Russia kabla Ukraine haijavamiwa.
 
Marekan bado ataendelea kuwa super power kwa sababu ana nguvu kubwa mno za kijeshi, uchumi mkubwa na imara zaidi, ana uwezo wa kutengeneza maadui karibu na mipaka ya adui yake ili awatumie hao maadui ku deal na ww kijeshi na kisaikolojia kama tunavyoona alivyomtengeneza adui wa Russia (Ukraine) na adui wa China (Taiwan) nk.
Naaaam!
 
China ameshalisoma SoMo vizuri sana kupitia kile kinachoendelea nchini Ukraine,
Kwa hiyo usitegemee kumuona china akijiingiza kwenye mgogoro wakati huu,

Anachofanya china Kwa Sasa ni kufutafuta tu aibu Ili ulimwengu uendelee kumuona kama super pawer
Mkuu umenifanya nicheke kwa sauti maeneo yasiostahili mtu kucheka hovyo hovyo.
 
Yaani wabongo bana, unakaa nchi ya ulimwengu wa tatu, kwenye dampo la dunia, unajitia kuwashauri viongozi na serikali ya Russia na China yenye agents hatari wanayoijua hii dunia?
Umekula ugali wako na muhogo umeshiba unakuja kudhani una ijua kesho ya Russia kuliko FSB? Raisi tu wa Russia ni former KGB, serikali ya Ukraine ina agents wengi tu wana leak data...

Unaijua China kuliko MSS? Chinese wana puppets wengi tu serikali ya Taiwan, tunajua machache sana...

Russia wanajua walifanyalo, walishajiandaa, kila kitu kipo calculated...

Kama umeshiba ugali better ukae chini ufuatilie bifu ya Harmonize na Diamond na udaku wa insta, huwezi ijua China au Russia kama agents wao ambao hawalali, wana risk afya zao na maisha yao, wamesomea ukachero na wanaishi ukachero na wanakula kikachero hata mapenzi ni kikachero, wakipumua ni ukachero... Ogopa sana hio...

Kwamba Russia imeingia mtegoni, Huyo ni mbongo, hivi vile vichwa vyote vya wale wazee pale Moscow vyenye mvi, makachero wabobezi toka USSR hawakujua plans za US?

Inaskitisha sana kwa kweli..
Sasa hao watu wengi ikawaje wakashindwa jua Pelosi anaenda Taiwan hadi waliposikia kwenye vyombo vya habari, ndo wakaanza mobilization ya vifaa?
 
Nimuda sahihikabisa Kwa uchina kuchukuwa hatua kaletena kala mrusi haja acha operation yake,na pia ni muda sahihi zaidi ya ushiriki wa mchina na mrusi dhidi ya beberu wa ulaya na America na ni muda sahihi wakuwadhoofisha zaidi,kama mrusi ameweza kuwatikisa pamoja na umoja wao mungano wa mrusi na mchina na harakati zao ni tulizo Kwa mabeberu hutaki muulize kiherehere BoJo,Macron,Dragh mjanja TU ni victor Orban kwani amewakataa mabeberu mchana kweupere🏃
Mkuu laiti ungeyajua maumivu anayopitia mrusi kutokana na vita vyake kule Ukraine wala usingekuja kupongeza vita hivyo. Mpaka sasa mrusi ashapoteza maelfu ya wanajeshi wake wakiwemo majeneral wakubwa, mrusi ashapoteza silaha nyingi katika vita na bado matumaini ya kushinda vita hiyo hayapo. Hapo hatujazungumzia madhara yatokanayo na vikwazo vya west countries. Kwahiyo ni lazima mrusi atakuwa ashamsimulia mchina kwamba asijaribu kakwe kuivamia taiwan, maana hasara atakayopata ni kubwa kuliko faida.
 
Acha kutudanganya,huyo ni mnaa maana anawatumia mazuzu yeye kuwa salama🤔
Sasa kuwatumia mazuzu ni moja ya njia ya ushindi vitani. Ndo maana hata katika mpira ukijifunga goli mwenyewe inasabiwa umefungwa tu.
 
Kweli mkuu, vita vya Ukraine vimei cost na kuipa hasara kubwa Russia. Hapo bado hatujazungumzia vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa wa watemi hawa wa dunia ya kwanza. Miaka 3 ijayo Russia itakuwa nyuma hata ya Saudia Arabia kijeshi na kiuchumi.
Vita urusi imepata faida hasa kuyachukua maeneo muhimu kama kinu kikubwa kabisa cha nuclear hapo ulaya na sehemu zenyewe migodi mingi na viwanda vingi hapo urusi imechukua karibu asilimia 95 la eneo lote la kulima ngano hapo Ukraine

Upande WA vikwazo kila mtu ni shahidi vikwazo vimewapiga wao kuliko hata urusi na kupelekea regime change

Ukweli mchungu hii vita West wameishiwa mbinu hata himars zimeshindwa kufua dafu kwa urusi ha ha ha ha ha ha ha ha ha Putin aliletwa kuwashughulia hawa wapuuzi WA West
 
Mkuu laiti ungeyajua maumivu anayopitia mrusi kutokana na vita vyake kule Ukraine wala usingekuja kupongeza vita hivyo. Mpaka sasa mrusi ashapoteza maelfu ya wanajeshi wake wakiwemo majeneral wakubwa, mrusi ashapoteza silaha nyingi katika vita na bado matumaini ya kushinda vita hiyo hayapo. Hapo hatujazungumzia madhara yatokanayo na vikwazo vya west countries. Kwahiyo ni lazima mrusi atakuwa ashamsimulia mchina kwamba asijaribu kakwe kuivamia taiwan, maana hasara atakayopata ni kubwa kuliko faida.
Vikwazo Kwa warusi SII jambo geni na ndio maana wapo tayari kupambana na mabeberu na kutafuta ushawishi duniani Kwa gharama yeyote,mwanajeshi kufa vitani ni sehemu ya kazi kama ilivyo kazi zingine na porojo za beberu wala hazimtishi kwani adui hukuombea njaa siku zote🤔
 
Back
Top Bottom