Kaka, huyu ndugu yetu nafikiri anatatizo kubwa, na tatizo lenyewe ni kushindwa kutambua haki yake ya kuwa mkuu wa nyumba na ndoa yake mwenyewe kama vitabu vya dini vinavyotanabaisha!
Lakini kwa sasa, maadamu amegundua kuwa hakufanya uamuzi sahihi kuishi ukweni, nafikiri anahitaji sasa kufanya maamuzi ya kiume. Anapaswa kuchukua vilivyo vyake, naamanisha mali zake, mke wake na mtoto wake na kuondoka na kuhamia nyumbani kwake, huko alikojenga. Hakuna sheria ya ndoa inayomlazimisha muoaji kubaki ukweni, huu ni umburura!
Asijidanganye kumuacha mkewe kama bado wanapendana hata kama wazazi hawataki. Mke ni mali yake maana kamtolea mali na pia wanandoa inayotambulika hivyo hakuna mtu aliye juu yao wa kuwapangia mambo yao ya ndani ya familia yao. Anapaswa kusimama kama mtoto wa kiume.
Eiyer, come this way, ujionee ulimwengu ulivyo na mambo!