kinundu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2016
- 2,028
- 2,168
Kijana
Sikushauri kunywa pombe na zaidi tafuta starehe nyingine pombe kama huna hela nzuri utaishia kwenye madeni .
Pombe usipoweza kujidhibiti utakuwa na magonjwa ya zinaa kila uchwao .
Pombe ukiendekeza utafeli mipango ya maisha
Mwisho pombe ni uraibu mbaya kuacha sio rahisi .
Siongei nikiwa nyumbani naongea nikiwa bar nakunywa pombe kwa hela yangu ila sitamani uje huku .
Nilianza kunywa pombe nikiwa na miaka 14 , sasa mimi kwa maelezo yako ni baba yako , nilitamani kuacha nikiwa na miaka 29 sijafanikiwa mpaka sasa na uzee huu .
Pombe imenipunguzia heshima kwa jamii kubwa iliyodhani mimi ni mtu wa heshima kwa elimu yangu na kazi yangu .
Pombe imenipunguzia ufanisi kazini , pombe imepelekea sasa nina gonjwa lisilotibika japo lipo katika early stage hivyo naweza kupambana kupona nikiamua .
Pombe imenifanya vitu vingi kuamuliwa na ndugu na mke hata kama kitu naona naweza kuamua mwenyewe lakini bado naamuliwa kwa nguvu .
Ndugu sikushauri kunywa pombe , watakuja vijana sio muda watasema nakunywa matuputapu wambie sijaanza kunywa pombe Tanzania hivyo wakumbushe nje hakuna mataputapu .
Usinywe pombe .
Kwasasa Mbeya pazuri .
Mbeya pazuri upo upande upi au kaunta gani mana pamekua pakubwa sanaa hapa ndani kaunta tatu bado nje live band hahha
