Haya, toa tafsiri ya hiyo sentensi ya kiarabu maana wewe ume "ilimit" akili yako na unataka wengine nao wawe kama wewe!!
Unashikilia vitu ambavyo huna elimu navyo!!.
سحر الفضة على ذهب
Neno "sihr" hapo limetumika, toa tafsiri hapo, na uniambie Waarabu wanapotamka maneno hayo huwa wanamaanisha nini???


Unashikilia tu sihr ni uchawi na kwamba ni kitu kibaya, ndiyo lakini hiyo ni kulingana na matumizi yake, ukiitumia kwa njia mbaya kama wale wachawi wa Musa (as) kupinga haki hapo ndipo inakuwa ni kitu kibaya, wewe usiidhulumu nafsi na akili yako kwenye "negativity" tu, angalia pia na "positivity".
Chukuwa mfano wa kisu, katika "negativity", kisu kinaweza kutumika katika mauaji lakini katika "positivity" kisu tunakitumia katika kazi nyingi za manufaa, huelewi hapo??, au unataka utuaminishe kuwa kisu ni kibaya tu kwa sababu kimetumika kwenye mauaji!!!,
Mimi ninataka uiangalie "sihr" katika njia hiyo kama ya matumizi ya kisu, sihr ni zana kama kilivyo kisu na siyo kitendo kama vile zinaa au wizi.
"Sihr" ni SCIENCE ya kuficha uhalisia wa kitu na inafafanuliwa kisayansi, katika zama zile za nabii Musa (as) ilikuwa ni vigumu kuelezea "the phenomenon scientifically." Ndiyo ninasema kutokana na ule msingi wa Sihr (yaani kufunika uhalisia wa kitu) watu tunaweza kupata FAIDA kwayo.
Leo kuna ndege za kivita (fighter-jet), kuyokana na elimu ya sayansi zinayo sifa ya kutoonwa na radar (steathy), lakini magari na vifaa vingine vya kijeshi vinaonekana bila kizuizi, sasa, mfano, kama elimu ya sihr ikitumika huoni kama itasaidia??, na hapa kuna mifano kadhaa ni nafasi ya wanasayansi kutafiti.
Na hapa katika tafiti ndipo utaona tofauti kati ya sisi Waafrika/waarabu na Wazungu, mfano Wazungu wanasema Inzi anaeneza maradhi lakini Mtume (saw) alisema Inzi anapodondokea katika kinywaji chako umdidimize halafu ndipo umtoe na kumtupa kwani bawa lake moja limebeba maradhi na bawa jingine limebeba dawa---hapo Mtukufu mtume anatutaka tusiangalie "negativity" tu bali tuangalie pia "positivity" kuhusu Inzi,na leo wanasayansi/Wazungu wanaifanyia utafiti hiyo kauli ya mtume (saw) juu ya faida ya Inzi (positivity), Sisi waislamu/wanasayansi tumekaa tu kazi kupiga DOMO, tumewaachia wasiowaislamu wakifanya tafiti juu ya kauli za mtume wetu (saw).na huenda wakatunukiwa zawadi ya Nobel.
Qur'an ni kitabu, pamoja na nasaha na maonyo, kimejaa elimu ya sayansi, zingine ziko wazi na zingine zipo katika "fundamental level".
HITIMISHO:-
" It is through a use, one can determine pros and cons of a thing "