Nahisi nilimegewa

Nahisi nilimegewa

The terminology could reveal so much about you, your personality and your thought process, therefore it is a crucial part of the question.

Very funny how people like you think you can know someone's personality and their thought process based on what they write here. It's very funny.

You don't know me like that homie, or do you?

I sure don't know you more than I know every inch of my glorious naked body!

Jealousy is really for the insecure.

Jealousy is human.

Kwangu mimi kuna kuwa na mtu au kutokuwa naye, kama nammind nakuwa naye, akichemsha naanza, kwa system hii utaona hakuna muda wa kuwa jealous hapo.

Kwani nani hakuanza? Hujui hata kudandia treni. Rudi tokea mwanzo usome vizuri. Unaongea kama vile bado niko kwenye huo uhusiano.

Ninayekuwa naye ninakuwa na confidence naye, nikiwa sina confidence naye siwi naye, no room for jealousy.

So?

Sasa wewe ambaye uko na mtu ambaye humuamini ndiye mwenye room for jealousy,

Narudia tena, rudi mwanzo usome uelewe nilichoandika. Sio unakurupuka tu majibu bila hata ya kuelewa. Nani ambaye niko naye?

kumtaka unamtaka lakini hapo hapo humuamini, kwa nini usiwe na jealousy, kila anapopiga kona unamuandama, bado kidogo umkodie private detective amfuatilie nyendo.

Hivi ni viroja sasa. Eti nilibaki kidogo nimtafutie kiduhushi? Umejuaje? Nilikwambia hivyo au unadhania tu?

Kama mtu humuamini kiasi hiki ya nini kuwa naye? Haya si mapenzi ni mateso

Uelewa wako saa ingine unatia shaka. Narudia tena, siko naye kwa sababu sikuwa na imani naye. Nilimwacha hata kabla hajaondoka. Sasa kipi kisichoeleweka hapo bana? Mbona uko mgumu sana kuelewa? What the hell?
 
Msichoshe Brazil;

Hakuna ambacho angeweza kukifanya! Hata leo hii ingenitokea mimi Mama Jr anaamua kufanya aliyofanya huyo Mdada; namruhusu kwa roho nyeupe kabisa! Ya nini kupata shida bana! Kwa sababu mpaka ameamua hivyo ujue tayari tafakuri zimepita na ameshapima na kuona kuwa huo ndio uamuzi wa maana kwake binafsi; Kumzuia ama kufanya mbinu abaki itakuwa kumuweka na kuwa naye kinyume cha dhamira yake!

She got what she wanted! Kibuti!
 
Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msichana mmoja mrembo sana. Hakuwa mrembo tu bali pia alikuwa na akili zilizoendana na urembo wake. Nilimpenda sana kwani niliona hatimaye nimempata anayeendana na mimi.

Wakati tunakutana nilimkuta akiwa tayari ana mtoto mmoja. Mtoto huyo alikuwa na umri wa miezi tisa. Baba wa mtoto huyo aliachana na huyo msichana wakati akiwa bado mjamzito wa miezi mitano na hata alipozaliwa jamaa hakuwepo na hakuja kumwona mwanae hadi alipofikisha umri wa miaka miwili.

Ndani ya miaka miwili ya uhusiano wetu jamaa akaanza kumshinikiza demu wangu ampeleke mtoto Toronto ili akamwone baba yake. Demu wangu akawa kwenye mazingira magumu kwa sababu tokea amzae huyo mwanae, baba yake alikuwa hajamwona na alikuwa anataka sana mwanae amjue baba yake. Wakati huo huo uhusiano wetu ulikuwa umekolea na mimi fikara za kumvalisha pete zikawa zimeanza kutawala kichwani mwangu.

Kwa takribani mwezi mzima akawa anafikiria ni jinsi gani ataweza kwenda kumpeleka mtoto Toronto bila kuharibu uhusiano wetu. Kumpandisha mtoto ndege na kuwakabidhi watu wa ndege halikuwa wazo zuri kwa sababu mtoto alikuwa bado mdogo sana. Mwishoni kukawa hakuna jinsi zaidi ya yeye mama mtu kumpeleka mtoto kwenda kumwona baba yake.

Siku ya siku ikafika. Mama na mtoto wakapanda ndege kwenda Toronto kumwona baba wa mtoto. Nikaachwa nyuma peke yangu. Toronto walifikia kwa huyo jamaa. Na jamaa alikuwa akiishi kwenye condo ya vyumba viwili. Ufikiaji wao hapo haukunipendeza licha ya demu wangu kuniahidi kuwa atakuwa analala sebuleni huku jamaa akilala chumbani kwake na chumba kile kingine cha pili atalala mtoto.

Walikaa huko kwa wiki mbili. Kila siku akiwa huko alijitahidi kunipigia simu angalau mara moja kuongea na mimi. Ilikuwa wakati mgumu sana kwangu mimi kwani sikumwamini hata kiduchu eti kuwa atakuwa analala sebuleni. Nikamwambia amwambie hivyo mtoto wa chekechea na si mimi kwani ingawa nilizaliwa usiku, sikuzaliwa jana usiku!!

Baada ya kurudi nilimwuliza kama alimegwa na yeye alikataa katakata. Mimi kwa upande wangu sikumwamini hata kidogo na nikamwacha.

Wadau, hivi kweli mnadhani alikuwa ananiambia kweli? Mtu kafikia kwa jamaa halafu kakaa wiki mbili, hivi kweli hawakumegana? Komredi Fidel hebu nipe mawaidha yako...unalionaje hili? Nilimegewa? Mimi nadhani nilimegewa ingawa sina ushahidi wa bunduki inayofuka moshi.

Pole mkuu ila wewe ulishasema huamini uaminifu katika mapenzi hata siku1
 
hapo pagumu kaka, hata ukiambiwa kuwa umemegewa tunda lako, ww bado unampenda huyo binti cha msingi ni kuupuuzia mawazo yote, na kuanza ukurasa mpya wa maisha, ila usimruhusu tena kumpeleka mtoto, kama anamtaka amfuate yeye nyie mlipo.
 
mzee bila kumung'unya maneno ALIMEGWA, mimi nilizaa na mwanamke lakini hatukuoana kila nikikutana kama nikitaka KUMMEGA ANANIKUBALIA hajawahi kuninyima, hiyo ni kweli kwa watu wote waliozaa pamoja wakijisikia kukumbushia huwa hawanyimani
 
mzee bila kumung'unya maneno ALIMEGWA, mimi nilizaa na mwanamke lakini hatukuoana kila nikikutana kama nikitaka KUMMEGA ANANIKUBALIA hajawahi kuninyima, hiyo ni kweli kwa watu wote waliozaa pamoja wakijisikia kukumbushia huwa hawanyimani

Eeeh banaaa ehhh duh haya bana hii inawapa mawazo mapya walooa wanawake wenye watoto:A S-alert1:
 
Well you can't tell, kwanini ilikuwa rahisi yeye kumpeleka mtoto kwa babake? Si angekuja tu kumtafuta mtoto after all years of being missing in action.

Alooo, I am starting to believe umemegewa. Kama unamlove just forget and start all over again na mikakati mipya.
 
Kwanza Kwangu mimi Mwanamke tayari keshazaa na mtu dah yaani ntapata sana phsycological torture ya kufikiria jinsi jamaa alivyokuwa anammega mpaka akapata mimba dah tyaache hayo. Kingine Mkuu NN kwa nini ulimruhusu aende peke yake, mzee na wewe ungekwwenda km ingewezekana na mkamwacha mtoto huko atleast for hizo weeks. sasa demu kenda kakaaa na mtu muda wote huo lzm walikumbushana tuuu. Mkuu pole sana heri uibiwe kila kituu lkn si MPENZI WAKO kamanda inaumaaaaaaaaa sana.
 
Babu jinga mali zako zinaliwa, mali zako zinaliwa.

Unauliza jibu?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
ni bora ulimuacha maana siyo vizuri kwako kuwa na mtu amabaye unamhisia. it doesn't matter kama alimegwa au hapana.... ile kuhisi kwako lazima ikunyime faraja..and it is natural. Jitahidi utafute mwanamke asiye na mtoto. Nimeshuhudia ndoa nyingi xa wanawake waliozaa tayari zimeharibika either kwasbabu ya mume alimzalisha au mtoto mwenye aliyomzaa mke kabla ya ndoa. kwahiyo hata kama si yule bwana wake wa zamani kuna asilimia kubwa kuja kugombana kwa sababu ya huyo mtoto wake. Kumbuka na mtoto akiwa mkubwa anakuwa upande wa mama yake siyo wewe. unaweza kukimbia hata nyumba. Mi naona umauzi wako ulikuwa wa busara SANA.
 
Back
Top Bottom