Nahisi mkuu wa shule ananichukulia mke wangu

Nahisi mkuu wa shule ananichukulia mke wangu

we cku akikupa safari ondoka ila uende ukazuge mahala usiondoke kiujumla, fanya research kiutalaam huku ukiwa na vijana wasoma ramani hasa maeneo ya home na mienendo ya mkeo!
 
Habarini wana jamvi,

narudi kwenu kuomba ushauri,mimi ni mwalimu wa shule x iliyopo katika mkoa x.Ni hivi karibuni nimekuwa na mahusiano mazuri sana na mkuu wa shule yangu,kitu ambacho kilikuwa ni nadra kuwahi kutokea,kwani amekuwa akinipa safari za mara kwa mara kutoka nje ya kituo na malupulupu mengine kibao wakati staff members wenzangu wakisota na kulalama.

Kinachontisha zaidi ni huyu mkuu kuanzisha tabia ya kuwa ananitembelea nyumbani na mara nyingine akijua fika kabisa kwamba mimi sipo nyumbani.

Sasa hii nahisi ni hali ya hatari na mimi ni mnyalu kutafuta kamba wala sioni kazi.

Naombeni ushauri wenu jaman, nifanyeje?
Kama shule ya serekali omba uwamisho,mbona shule nyingi tu.Na kama ni shule binafsi,tafuta shule nyingine uombe kazi,shule binafsi pia nyingi,na zinatafuta waalimu.
 
Wewe umesaidiwa kutunziwa familia wkt haupo halafu unalalamika, km vipi kataa hizo offer ili ukae na mkeo muangaliane
 
N wewe anza kutia Maguu kwa Mkuu wa shule pindi anapokuja Kwako
 
Ukijitundika ndo umempa nafasi ya kumwoa kabisa,kwani anaimaliza yote?? we faidi tu marupurupu ya bure ilhali wenzio wanalalamika.Tehe-Tehe-Tehe-Tehe.
 
Nshamchunguza sana,saivi mjamzito ila cna hakika kama ni mm
 
Habarini wana jamvi,

narudi kwenu kuomba ushauri,mimi ni mwalimu wa shule x iliyopo katika mkoa x.Ni hivi karibuni nimekuwa na mahusiano mazuri sana na mkuu wa shule yangu,kitu ambacho kilikuwa ni nadra kuwahi kutokea,kwani amekuwa akinipa safari za mara kwa mara kutoka nje ya kituo na malupulupu mengine kibao wakati staff members wenzangu wakisota na kulalama.

Kinachontisha zaidi ni huyu mkuu kuanzisha tabia ya kuwa ananitembelea nyumbani na mara nyingine akijua fika kabisa kwamba mimi sipo nyumbani.

Sasa hii nahisi ni hali ya hatari na mimi ni mnyalu kutafuta kamba wala sioni kazi.

Naombeni ushauri wenu jaman, nifanyeje?
wewe nahisi ndo hzo hela zinakuchanganya na hayo marupurupu kwan ukikataa na hizo ofa mshahara wako utakatwa? ucpende dezo sana kuwa na mipango yako tu..
 
Back
Top Bottom