Nafikaje udsm(main campus)

Nafikaje udsm(main campus)

Wamechangia vizuri wachangiaji ila nadhani hawafahamu Tua ngoma ipo eneo gani. Tua ngoma ipo mara tu baada ya kupita kongowe hivyo kupitia feri ni kuzunguka sana. Kuna mabasi ya moja kwa moja kutoka Tuangoma hadi kariakoo nadhani hiyo ndio itakuwa njia nafuu na fupi, akifika Kariakoo sasa hapo atapanda Mwendo kasi na kufuata maelekezo kama yalivyotolewa hapo juu ya kushuka Ubungo Maji na Kupanda boda boda kushuka Utawala

Mkuu Kariakoo kwa mtu mgeni ipo complicated kidogo mpaka apande mwendokasi atakuwa kapata tabu sana bora ya kigamboni inamshusha kituoni kabisaaa
 
Khaaaa toangoma palefu nahisi iyo ipo kongwe mbagara sasa unapanda gar toka kongowe mpka mbagara then mbagara panda za mbgara makumbusho shuka makumbusho chukua za makumbusho mbenzi au gongoramboto shuka magufuli hostel

Sasa mkuu hebu angalia tu mwenyewe gari ngapi anapanda hapo? Halafu mwisho wa siku badala ashukie main campus anapoenda we unamuelekeza Hostel za magufuli mlimani city huko akafanye nini? Wakati ameshakwambia anaenda main campus! Yani afike hapo hostel aanze kuuliza tena main campus wapi aanze kusaka usafiri mwingine tena sasa si bora njia ya toa ngoma daladala moja na mwendokasi moja fasta hata kwenye foleni hatokaaa atafika fasta tena kwa urahisi
 
Ukweli ni kwmaba aliokueelekeza kkoo ni chaka magari ni ya shida sna. Na njia ya mbagaala ni ndefu ukitokea ubungo mpka ufike rangi tatu. Hizi option zote ngumu, njia fupi ni mwendokasi. Ukiweza ku manage kupnada gari. Mpaka kivukoni, basi kule usiwe na wasi wasi, wezi wa ferry wezi wa viroba. Hadi ukifika ferry mwizi mwenyewe anajua huyu mwenyeji. Sio rahisi sana labda uwe unauliza uliza kibwege. Chukua mwendokasi, kwa mida ukifika watu wa,kimara hakuna wa kwenda mjini, tena utapata hadi siti. Ktk mwendokasi. Mpaka kigamboni, kigamboni pale wewe sikiliza ukiskia kongowe kongowe kongowe. Panda, tua ngoma kituo kikubwa utamskia konda lazma ashushe. Kwa uhakika unakaa karibu na mlango anakua anakuona. Atakumbuka tu kukushusha. Then karibu mjini, unapata experience mbaya ya dar kutokana na huyo mwenyeji wako. Anakaaa makazi maapya. Tuangoma bado sana kuzoeleka.
 
Tumia google earth, uwe tunduma uijue jamii forum, usiijue google earth? Che!
 
Pa kufikia nmeshapapata kuna ndugu atanipokea ye anakaa toangoma.
Sasa ndo natak kujua kwamb nkishakuwa hapo toangoma labda napand magar ya wap mpk wapi ili nifike huko main campus
Huyo ndugu yako hapajui chuo kikuu ??
 
Kama una smartphone basi set route hadi UDSM kweny google map...yani itakupeleka hadi nkurumah hall [emoji3]

Au wanaume wa mkoani hamjui google map (kidding) [emoji3]
 
Kama una smartphone basi set route hadi UDSM kweny google map...yani itakupeleka hadi nkurumah hall [emoji3]

Au wanaume wa mkoani hamjui google map (kidding) [emoji3]

Jitahidi Kumpeleka Bagamoyo Huyo mwenzio 😀😀
 
Write your reply...
usije mjini kaa hukohuko kwenu
ukija huku utaibiwa mpaka nyeti zako
 
Ni vizuri mwenyeji wako akawepo kukusaidia au kama hana muda akutafutie mtu wa uhakika hata mtaani aje kukusaidia......Miluzi mingi humpoteza mbwa
 
Chuo kinafunguliwa lini? Usisafiri mapema sana utapata shida. Subiri chuo kifunguliwe ndo uje.
 
Back
Top Bottom