Nachingwea: Mabomu ya machozi yarindima mchana wa leo...

Nachingwea: Mabomu ya machozi yarindima mchana wa leo...

Planner

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
348
Reaction score
149
Wadau Mchana wa leo (saa 6 mpaka 8 mchana) kumetokea vurugu mchana huu hapa Nachingwea hali iliyofanya polisi kujihami kwa kuanza kurusha mabomu ya machozi.

CHANZO CHA TUKIO:
Vijana waendesha pikipiki almaarufu bodaboda wengi wao yasemekana wakitokea Masasi wamefika kituo cha polisi hapa Nachingwea wakidai kumtafuta mtuhumiwa aliyempora pikipiki mwenzao,baada ya muda hali ikachafuka na polisi wa hapa wakajihami kwa mabomu.

Muda si mrefu maduka yote na biashara yakafungwa na hali ya mjini ikawa tete! Kilichonishangaza wakati niko na gari natoka nje ya mji nikakutana na lori la jeshi likiwa na askari wamevalia kivita na silaha linaingia mjini kwa kasi kuimarisha usalama, which implies polisi wamezidiwa nguvu.

Kwa sasa hali imetulia ila hofu imejaa mitaani.

My take:
Hivi jeshi la polisi litasukwa vizuri lini liweze kuhimili majukumu ya aina hii manake sidhani ni vizuri jeshi la wananchi kuingia mtaani hata katika mambo ambayo polisi wangeweza (labda pale inapobidi)-Hizi chokochoko za bodaboda vs polisi zitafutiwe ufumbuzi otherwise tutakujajilaumu baadae.

SOURCE: Mimi mwenyewe nimeyashuhudia leo hii mchana.
 
Kaka, hiyo nchi yako ...mabingwa wa kutatua na kuingilia migogoro ya nchi nyingine, kama jeshi la polisi tu ni weak ths much, nina mashaka sana na jeshi linalokimbilia kwenda 'kusafishia' jina kwa madreva bodaboda wenye mawe tu na petrol! Hii mikwara ya JW naombea iishie humu humu, tusijetia aibu ... wasiwasi wangu usjekuta hata MALAWI wakatupimia...
 
South spring ishapamba moto.
Maji maji war ilianza pole pole baadae ikasambaa kusini kote,wawe macho magamba.

Halafu sasa unaonyesha jinsi ulivyokuwa hauna ubunifu, sasa The South Spring inahusiana vipi na Mtwara? Ungekuwa makini kidogo na kufikiri tu kwa mbali ungetafuta jina ambalo linaleta maana, kwani Mtwara hakuna spring kwa maana ya matumizi ya neno lenyewe, hivyo The south spring haina maana kwenye mambo ya Mtwara!

 
Aise kila siku ni mpambano tu!!! Nchi inaelekwa wapi? Huo mkutano wa DAVOS2013 haujaisha wajameni? Tunataka tamko hapa ila mambo ya kamati chunguzi acha hazijawahi kufanya kazi ya maana ni kupeana ujiko tu!!! Yaani inachekesha unapounda kamati ya kukuchunguza wewe mwenyewe? Halafu kuwe na majibu ya wazi na ya utekelezaji!!! Danganya toto!!! Si mtwara tu, hali ni mbaya mikoa yote, wanangokea tu kamwanya katokee!!! Nchi haitawaliki tukubali!! Shida na umaskini umekithiri mno!! Wananchi wengi wamekataa tamaa!! Hata kama una kipato kama mshahara au biashara but inflation is at peak!!! (tusidanganye umma kwa figure za kupika)!!
 
Daaaah wana kusini kweli mnaweza!
 
Mkuu umeona mbali sana kwani ulichokiandika ni kweli tupu.
Kaka, hiyo nchi yako ...mabingwa wa kutatua na kuingilia migogoro ya nchi nyingine, kama jeshi la polisi tu ni weak ths much, nina mashaka sana na jeshi linalokimbilia kwenda 'kusafishia' jina kwa madreva bodaboda wenye mawe tu na petrol! Hii mikwara ya JW naombea iishie humu humu, tusijetia aibu ... wasiwasi wangu usjekuta hata MALAWI wakatupimia...
 
Halafu sasa unaonyesha jinsi ulivyokuwa hauna ubunifu, sasa The South Spring inahusiana vipi na Mtwara? Ungekuwa makini kidogo na kufikiri tu kwa mbali ungetafuta jina ambalo linaleta maana, kwani Mtwara hakuna spring kwa maana ya matumizi ya neno lenyewe, hivyo The south spring haina maana kwenye mambo ya Mtwara!


Kaka yupo sahihi..... contemporary hata gas inaweza kua gas spring...aha ahaahh hahah hah
 
halafu sasa unaonyesha jinsi ulivyokuwa hauna ubunifu, sasa the south spring inahusiana vipi na mtwara? Ungekuwa makini kidogo na kufikiri tu kwa mbali ungetafuta jina ambalo linaleta maana, kwani mtwara hakuna spring kwa maana ya matumizi ya neno lenyewe, hivyo the south spring haina maana kwenye mambo ya mtwara!


Nachingwea haipo mtwara ipo Lindi,so taharuki iliyoanzia Mtwara itakua ni chachu ya kusambaa kwa kusini yote,as far as Mtwara corridor is concerned..
Just comparison with the Arab spring which was spearheaded BY Tunisia.
 
Tanzania mwee wajameni! Siamini kama inaelekea kama Burundi, Rwanda, DRC nk. Huko nako mambo yalianza kidogo kidogo hivi hivi, kupuuza madai ya wananchi.
 
Afadhali sasa nina uhakika ajira kwa vijana walio chemka form four wata pata ajira.....
 
Back
Top Bottom