Nabii Penuel Mnguni aonja joto ya jiwe

Nabii Penuel Mnguni aonja joto ya jiwe

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,669
Reaction score
860,996
Chama cha EFF- Economic Freedom Fighters wamefanya jambo ambalo laweza kuwa tahadhari kwa wengine wote wenye tabia zisizokubalika katka Jamii.

Nabii Penuel Mnguni 23 amekuwa maarufu viunga vya Pretoria na Afrika kusini baada ya kuwa na ibada zenye utata mwingi, amekuwa akiwaamrisha waumini wake wale nyoka panya majani na nywele kuwa kimiujiza hivyo vyote hugeuka kuwa chakula.

1439441314387.jpg
hapa akimpa muumini toilet paper

1439441401811.jpg
hapa muumini akila majani.

1439441431627.jpg
hapa ni mhanga wa nabii Mnguni, binti aliyevamiwa na muumini wa Mnguni akaanza kunyofolewa nywele ili jamaa azile kama chakula.

Sasa baada ya EFF kuchoshwa na upuuzi wa manabii wa namna hii walivamia kanisa lake wakiwa na panya na nyoka ili wampe nabii ale kama anavyowaamrisha waumini wake.

Bahati mbaya au nzuri nabii alichezwa na machale akasepa kabla jamaa hawajamkata na hivyo kupelekea kulichoma moto kanisa lake.

Police wa Pretoria wamethibisha tukio hilo
Chanzo: BBC News
 
Nina wasiwasi na waumini wake. lazima watakuwa hawajielewielewi.
 
wamsake hadi yeye alishwe nyasi, nywele na nyoka.
 
Imani ikitumiwa vibaya ni hatari, kuna watu wanaamini watu wengine kama ni miungu, akili zao wanaweka pembeni,TUNATAKIWA TUWE NA FAITH AND REASONING
 
hao freedomfighters(wapagani?) wameonekana wakombozi wa utumwa wa kiroho...
 
wawaache waendelee kula hayo majani. hicho ndo kilichobora walichochagua.
 
shangaa na wewe, kwanza hizo nywele haupewi unavamia mtu anajipitia barabarani unanyofoa nywele unakula. angalia picha bidada anavyonyofolewa nywele.

Ujinga yaani unapewa nywele unakubali kula ili iwe nini hawa wakipewa mabomu wanajilipua ili waende pepo!
 
Huu ujinga si huko tu. Hapa tumeshawapata wengine wakitaka kwenda Ulaya bila tiketi, viza wala booking ya ndege! Wengine wanakosa fedha za kununua chakula, nguo na watoto wao hawasomi, lakini mapato yote wanawapelekea wachungaji, watumishi na matapeli wengine wa aina hiyo. Hizi dini hizi za kuanzishwa na binadamu wenye njaa na kiu ya utajiri jamani ni shida kweli kweli.
 
Na wa-Kenya wamemchelewesha mungu wanyinyi mpaka kafariki kwa mabaya yake.

Malema yuko vizuri kupinga udhalimu wa namna hiyo maana watu wakiwa na shida wanateswa kwasababu ya ujinga walio nao.
 
Na wakenya wamemchelewesha mungu wanyonyi mpaka kafa mwenyewe. Fake pastors wanatumia mianya ya ujinga shida za watu kuwatesa kama wanavyotaka.

Panuel Mnguni, Mungu wanyoni, black Jesus...
Life after death/ Wataenda wapi baada ya kufa?
 
Manabii wa siku hizi kanjanja sana na waamini nao wanageuzwa mazoba
 
ndo maana ulaya hakuna kitu kinachoitwa ukristo, imebaki Africa na kwa wamarekani weusi tu, huo ndo ukweli unaouma!
 
Na wakenya wamemchelewesha mungu wanyonyi mpaka kafa mwenyewe. Fake pastors wanatumia mianya ya ujinga shida za watu kuwatesa kama wanavyotaka.

Panuel Mnguni, Mungu wanyoni, black Jesus...
Life after death/ Wataenda wapi baada ya kufa?

Ni roho zitakazoendelea kusumbua ulimwengu
 
Back
Top Bottom