Nabii Flora wa Mbezi DSM ameumbuka Uchaguzi Arumeru!

Pamoja na huduma za kuombea wagonjwa ninatoa ushauri kwa manabii kuwakumbusha wateja wao kujikinga/kuepuka magonjwa yanayoepukika kwa mfano UKIMWI.
 
nimwamini nani nimkubali nani...wanasiasa vigeugeu,watumishi wengine wa mungu vigeugeu,madaktari vigeugeu,.......daa kumtumikia mungu tumbo ni nouma...haya twende huwezi changanya maji na mafuta yatajitenga tu.
 
Tapeli hiyu mganga njaa kwa pesa za wenye matatizo, wezi na mafisadi.
 
Haya siyo maneno yangu ni kutoka kwenye BIBLIA....

Mathayo 24:4, 5, 24-26 "
4-5:Yesu akajibu, akawaambia angalieni mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
24-26 Kwa maana watatokea wakristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. Basi wakiwaambia yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki."

2Wakorintho 11:4, 13-15 "
4; Maana yeye ajaye akihubiri Yesu Mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea au injili nyingine msiyoikubali mnatenda vema kuvumilia naye."
13-15 "Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watenda kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu. maana shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kuwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao."
 
Tangu lini mganga/mpiga ramli akakaa Mbezi beach? Watu kama hao wanakaa na kusimamisha himaya zao katika maeneo ya walala hoi.
.
 
Nabii Flora Wa Mbezi Beach aliwambia Waandishi wa habari kuwa ameoteshwa na miungu yake kuwa Mgombea wa CCM Sioni Summari Mkwe wa Edward Lowassa atashinda uchaguzi mdogo Arumeru.Habari hiyo iliandikwa Front page kwenye gazeti la Uhuru!!Kutokana na ushindi wa Mgombea wa Chadema Arumeru ni dhahiri kuwa Nabii Flora ni nabii wa uongo na tapeli!!!Hata hivyo juzi baada ya kutoa utabili huo alijitikeza kwenye vyombo vya habari na kusema kuwa ameombea watu UKIMWI na tayari watu 40 wamepona na kuthibishwa na madaktari. Tangazo hilo lilitolewa kwenye gazeti la tanzania Daima .

Hata yule babu wa loliondo alisema kuwa ameoteshwa na mungu kutoa ile 'dawa' yake ya kikombe.
Watu wote tunajua sasa kuwa ilikuwa ni wizi mtupu! na watu wengi sana walipoteza maisha yao kwa kuamini 'kikombe' kuwa ni 'dawa'.
Watanzania angalieni sana watu hawa wanaokuja kwa kutumia jina la mungu.
Isije kuwa watu wakaangamia tena kama walivyoangamia kwa babu wa loliondo.
 
Nimemuona Nabii Flora kwa macho yangu. Kwa mtazamo tu wa nje, hana sifa ya kuwa nabii wa Mungu. Amejichubua hadi anaboa. Ukisikiliza story kuhusu maisha yake ni utapeli mtupu.

Cha maana watu washikilie imani zao. Manabii wa uongo wamejaa kila kona. Simameni katika Neno la Mungu nalo litawaweka huru.
 
Nabii -watu wanadhani ni suala la kujiita tu kuwa nabii-basi ukawa. Hapo sasa ameonesha dhahiri kuwa si lolote wala chochote, tangu lini nabii akasema lile lisilo sahihi? Tunalazimika kutia shaka hata maubili yake sasa
:smile-big::rockon:
 
Mbona siku hizi watu hawamuogopi mungu kiasi hiki?

ivo vyeo mpaka kuwa nabii vinasomewa au mtu anajiamulia tu kujiiita!
 
Nimeanza kuuelewa kwa nini Karl Max ,yule mwanashosholojia na mkomunisti wa Kijerumani alikuwa akiuchukia sana ukristo.Akiamini katika umuhimu wa wanyonywaji kujitambua na kuchukua hatua ya kujikomboa, aliiona dini, hasa uktisto ,kama kikwazo katika kuleta mapinduzi (mabadiliko ya ghafla ya kiuchumi , kiutamaduni ,kijamii na kisiasa) .Aliamini kabisa kuwa dini ni 'bangi ya watu' akimaanisha,mara baada ya kukolea katika imani za dini zao,waamini hushindwa kuwa na uwezo wa kuwa na utambuzi sahihi wa vyanzo vya hali zao,hasa ufakara wao na hivyo kukosa uwezo wa kujua mbinu za kujikwamua kutoka katika hali hizo kama matokeo ya kwa kupandikizwa 'false consciousness' katika akili zao na viongozi wao wa kidini.Haishangazi ,basi,kuona makanisa ya leo yanajaa watu wanaodhaniwa ni wafuasi wa Yesu Kristo,wakati ukweli ni kuwa kinachowavutia kufanya hivyo ni kutafuta relief na / au utajiri wa haraka,wala kumpenda Yesu hakupo mioyoni mwao.Hawaelewi kuwa maombi pekee,kama tendo la kiimani, bila kuambatana na matendo,hayawezi kuleta mkate mezani, wala kuleta karo ya shule ya watoto.
Nabii huyu, huenda hakujua kuwa, kwa miaka mingi Wameru wamekosa maji na ardhi.Hata kama alijua, ni wazi kabisa naye ni mhanga wa 'faslse consciousness" inayomfanya asielewe kwa nini Arumeru walihitaji mabadiliko kwa kupata mbunge mwanabadiliko.Ninaamini,Yesu si mwanadamu na hasemi uongo kama sisi wanadamu wakiwemo wanaojiita Manabii wa Mbezi ambao hata hawavutiwi kwenda kufungua kazi zao Temeke Mikoroshini ama Tandale wanapoishi watu maskini.
Kwa kuwa uongo haukabaliki- maana ni dhambi mbele za Mungu - mtu huyu ana neema ya kutubu na kujutia kosa lake mbele ya wafuasi wake, jumapili ijayo.Akifanya hivyo,atambue kuwa ipo tofauti kubwa kati ya 'maono toka kwa Mungu' na 'matamanio ama ndoto za mwanadamu '.Asipofanya hivyo,adhabu muafaka ,ambayo waumini wake wanayo mikononi mwao ni kutafuta mahali kwingine pa kumwabudu Mungu.Lakini kama nilivyosema hapo awali, ile 'false consciousness' na 'bangi' wanayopandikizwa haiwaruhusu kufanya hivyo.
Yesu hakuwa na ushirika na watawala wa wakati huo kutokana na maovu yao.Watawala hao hawakufurahishwa na ujio wake duniani na ndio waliopanga na kuratibu mateso na kifo chake.Watumishi wa kweli wa Mungu wanapaswa kuwa upande wa wanaonyonywa na kugandamizwa.Kwa Arumeru ,walionyonywa na kugandamizwa walifahamika ,kama ilivyo kwa wagandamizaji na wanyonyaji.Aidha, mkombozi wa kweli wa Arumeru alikuwa anafahamika na tunafurahi amepatikana jana.
 
Sidhani kama hawa wanaojiita ni manabii kuna ukweli kwa hilo, nafikiri watu inabidi wajitahidi kumwamwini Mungu wao binafsi na kumuomba wao binafsi, na kutii sheria na taratibu zake kama maandiko yanenavyo ili Mungu ajidhihirishe kwenye mahitaji yao. Watu wengi ni wavivu kiasi kuwa hawana nafasi ya kumwabudu mungu na kufanya yawapasayo kabla ya Mungu kufanya sehemu yake badala yake hudhani kuwa Nabii au mtume au askofu anaweza kumshawishi Mungu kwa njia ya mkato pasipo sababu za msingi. Haya yote ni kutokana na uchanga wa kujua neno la Mungu.
 
Back
Top Bottom