Nabii Flora (aliyeshika maiki) akiendesha maombezi kwa wenye matatizo.
Watu wenye matatizo wakishiriki maombi ya kuponywa kanisani kwa Nabii Flora.
WATU wengi wamekuwa wakifurika kutafuta uponyaji kwa njia ya maombezi kutoka kwa Nabii Flora ambaye mashuhuda wanasema anaponya magonjwa mbalimbali kama vile Ukimwi, kansa, kupoteza fahamu, magonjwa ya moyo, upofu, ulemavu na kadhalika.
Maombi hayo yaendeshwa na Nabii Flora huko Mbezi Beach maeneo ya Tangi Bovu jijini Dar es Salaam ambapo watu wenye kufuata huduma hiyo wamekuwa wakiwasiliana naye kwa kutumia namba za simu 0657 442699.
Zifuatazo ni picha zaidi za uponyaji katika kanisa la Nabii Flora:
Nabii Flora Wa Mbezi Beach aliwambia Waandishi wa habari kuwa ameoteshwa na miungu yake kuwa Mgombea wa CCM Sioni Summari Mkwe wa Edward Lowassa atashinda uchaguzi mdogo Arumeru.Habari hiyo iliandikwa Front page kwenye gazeti la Uhuru!!Kutokana na ushindi wa Mgombea wa Chadema Arumeru ni dhahiri kuwa Nabii Flora ni nabii wa uongo na tapeli!!!Hata hivyo juzi baada ya kutoa utabili huo alijitikeza kwenye vyombo vya habari na kusema kuwa ameombea watu UKIMWI na tayari watu 40 wamepona na kuthibishwa na madaktari. Tangazo hilo lilitolewa kwenye gazeti la tanzania Daima .
hako kadada na wenzake wanaojitangaza manabii na washirikina wa kutupwa.ona iyo picha wajinga walivyojazana kumsikiliza.wakienda hapo naigeria kwa t.b. Joshua kuchukuwa mazingaumbe basi watanzania tupendavyo maisha mazuri ya duniani tutajazana huko na maushuhuda ya uongo.yesu aliteseka mwanzo mwisho wewe unataka raha duniani.eti usiugue ,eti upate pesa,magari baada ya maisha ya hapa duniani vitakusaidia nini?nyie nendeni tuu.tena zungukeni kila anapoibuka tapeli mpya na mazingaumbe kabambe.siku ya mwinabii flora
wednesday, december 7, 2011
nabii flora akiwa kanisani kwake
akimtabiria mtu
hivi karibuni jijini dar es salaam kuna nabii mwingine mpya ambaye amekuwa maarufu kutokana na wingi wa watu wanaohudhuria kanisani kwake na kupata huduma za kiroho. Anajulikana kwa jina maarufu kama nabii flora, watu wamekua wakiongelea kazi na shuhuda zinazotokea mahali anapohudumu, kwamba watu wanaponywa magonjwa yote sugu, vipofu wanaona, uvimbe na kila aina ya magonjwa na matatizo mbalimbali.
mwaka 2011 pamekua na makanisa mengi ambayo watu wanakimbilia kupata huduma za kiroho na kimwili. Na nabii flora ni mmoja wa manabii ambaye amefanikiwa kupata watu wengi.
KAKOBE alitapatapa 95 kuwa Mungu wake amemwambia NCCR watashinda,ikala kwake!
2005 Kilaini alibwatuka kuwa JK ni chaguo la Mungu...ukweli unaonekana!
Jamani,NJAA HAINA ADABU!
Mhhh,.Kweli tunahitaji Roho wa Mungu kuwatambua wa ukweli na uongo.Na hii miujiza inachanganya watu sana.