Ni kweli mtumishi huyu anatumia mafuta ya mzaituni tokea Israeli? Ni kweli mtumishi uyu anatumia sabuni? kuwapa watu? vizuri umejitokeza hapa kusema unamfahamu mtumishi uyu! je kabla ya utumishi alikuwa wap anafanya nn? huduma ya utumishi wake ilianza lini kabla ya kuanzisha kanisa lake? mbezi? huko kigamboni alikuwa mtumishi kanisa gani? kutokana na watu kuwa na hofu ya kwamba siku za mwisho kutakuwa na manabii wengi wa uongo! kufuata mafuta yaliyopo kwa mafuta kwa mtumishi kwangu mimi sio dhambi! maana watu walimtafuta Yesu popote alipo! na ni kweli ufalme wa Mungu hutekwa na wenye nguvu.
Sina nia ya kumnyooshea kidole wala kumsema vibaya! ila nina maswali yangu naamini wengine pia wanayo! naamini mti wenye matunda unapigwa mawe na watu wabaya na watu wazuri tena! pengine ni kitu kigeni sana! hapa Tz kuona nabii mwanamke mwenye mafuta! tukirudi kule juu Mungu alisema tuichunguze kila roho! kabla ya kuiamini naamini pia si dhambi! ivyo kwa maneno hayo! je wewe mwenyewe binafsi kabla ya kuombewa na kufanikiwa je ulishachunguza ukajidhiririsha mtumishi uyu roho inayofanya kazi ya miujiza au uponyaji kweli ni ya Mungu?
kwann kumekuwa na negative sana kuusu uyu Mama nabii? tungejua historia ya mama huyu pengine ingesaidia kuondoa uzushi uliopo? watu wanamshutumu juu ya ngozi yake ya uso! wanamshutumu juu ya nguvu za kuponya na miujiza si za Mungu aliyehai! je ni sababu ya ngozi yake ya uso? je ni sababu anavyovaa! naamini sijaingia katika kumnyoshea kidole nipo katika ile inaitwa " zichunguzeni kila roho" kuna huduma moja ambayo anayo huyu mama ya "delivarence kwa kutumia damu ya Yesu" makanisa mengi yanajua lakini mengi hawayatilii maanani instead wanaanza kuombea kwanza kabla ya vifungo vyote vya nyuma kuachia! je ndo sababu ya kufanikiwa maombi yake! embu endelea kufunguka mdau!
Ninamjua Huyo MTUMISHI Wa Mungu Tokea Akiwa Kigamboni, Kisha Kwa Mzee Willy Pale Mbezi Beach Maguruwe Na Mpaka Alipoanzisha Kanisa Lake Salasala.
NINAMKUBALI 100% Kwani MAFANIKIO Yake KIMAOMBI Ni MAKUBWA Na Hayaelezeki Na Tokea NIMFAHAMU Sijawahi Kuona Mtu AKIENDA KWAKE NA ASIFANIKIWE. Lakini Pia TUSISAHAU Kuwa Dini Pia Ni IMANI Ya MTU Na Jinsi UNAVYOJIACHIA Kwa Mwenyezi Mungu au Yesu Kristo.
Kwa Mfano UNAKUTA MTU ANAENDA KUOMBEWA LABDA APATE MUME NA MTUMISHI WA MUNGU AKIMWOMBEA NA KUMTAKA AACHANE NA UMALAYA YEYE AKIRUDI TU KITAA MWENDO NI MDUNDO KWA WAUME ZA WATU Je Hapo UNATEGEMEA NINI MKUU?
Nabii Flora Peter Ni MTUMISHI Wangu Na Namkubali Hadi Sijui Nisemeje Na Nahisi Nina DENI La Kumlipa Kwa Maombi Yake Ya UHAKIKA Kwangu Na Jinsi Mambo Yangu Yanavyozidi KUNYOOKA.
Najisikia Mwenye Furaha Mno KUSALI Kwa Nabii Flora Peter Na Nichukue Nafasi Hii Murua Kuwakaribisheni Na Wengine Wote Ambao Mna IMANI HABA. Mtasikia Mengi Na Mtadanganyana Sana ILA Ushuhuda Wa Maombi Ya Nabii Flora Peter HAUELEZEKI.
Namalizia Kwa Kusema " Kwa Msaada Wa Mungu Tutatenda Makuu Kwa Maana Bwana Atawakanyaga Watesi Wetu Zaburi 60:12 Na 108:13 ".
kabisa mkuu naabudu hapo tangu yupo mbezi mpaka anahamia salasala
Me nilisha enda sana kwenye maomb lkn siamin ile stika yenye picha yake anayouza 5000 et utembee nayo au uweke chin ya mto uilalie au uweke kwenye maj uwoge iyo iman sikubalian nayo kabisa na unabii naoutoa pia sikubalian nao
Huyu ni Michael Jackson au macho yangu mabovu?
kwa mda mrefu nimekuwa nikisikia kuusu nabii flora na mambo anayoyafanya! Kabla ya kumreccomand mtu aende, waliowahi kwenda embu tupe ushuhuda ipo miujiza kweli? Upo uponyaji kweli?
Je ipo katika misingi ya mungu wa mbinguni! Yani yule mungu wa meshack shedrack na abednego? Toa maoni bila kutukana huduma ya watu bila kumtukana mtumish uyo! Nataka expirience tuu kwa walioenda kama hujaenda usijeandika mungu akakulaani.
Je ni kweli anatumia sabuni iliyoombewa kama njia ya kuleta uponyaji na miujiza? Je anatumia mafuta ya mzaituni kutoka israeli kama njia ya kuleta miujiza na uponyaji?
Kwa wanaojua je sabuni kutumika kulete miujiza au uponyaji kuna mtu mwenye maelezo juu ya ufunuo huo! Ingawa si wa kwako ndio lakini unaweza kuelewa! Katika bible lakini.
Mkuu akhsante kwa kuliona hili.Mimi binafsi sikuwa na shaka na huyu nabii mpaka pale nilipomsoma GENTA,nikaamini kabisa jinsi anavyoandika hapa JF,na uhusika wa huyo mama nabii katika maisha ya GENTA,napata mashaka sana ya uhalali wa huduma yake.
Mungu wangu..! Ndio huyu nabii mwenyewe?
Ni mikorogo kwa kwenda mbele...
ameolewa au bado bikra?