Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,700
- 1,857
Thread yenyewe ni mambo au vitu ulivyoviona/vijua ulipokuwa mdogo na sasa vimetoweka kabisa. Hii ni kwa sababu ya kujikumbusha, na pia kuwazindua wale waliokuwa bado hawajazaliwa. Naomba mwanzo uwe mwaka wa 1960. Wale wote waliozaliwa katika mwaka huo au baada ya mwaka huo waelezee mambo yaliyotoweka, mazuri na mabaya. Nadhani iko wazi sasa. Naanza....
Wakati nainukia miaka ya sabini, mambo haya na tabia hizi zilikuweko sasa hakuna tena.
1-Kulikuwa na viwarsha vingi vidogo vidogo mitaani: fundi cherahani, sonara, watengeneza sufuria, fundi viatu n.k.
2-Wake wengi wa nyumbani walikuwa hawaendi sokoni kwani vitu vilikuwa vinapitishwa mitaani na wafanyibiashara kama wauza samaki, mboga n.k.
3- Kulikuwa na waarabu tuliowaita washihiri. Hawa walikuwa wanatembeza nguo barabarani wakiuza (sasa ndio mabosi!)
4- Wahindi walikuwa wakijulika sana kwa viduka vya pembeni (corner shops) tukiwaita 'dukawalla' (hawakua na ubaguzi kama walionao sasa, kwani huwezi kumbagua mteja wako unayemtegemea kwa ulaji wako wa kila siku)
5-Wakati huo kuvaa shati au suruali iliyokwisha tengenezwa (ready made) ilikuwa jambo la aibu, mtu huchekwa kwa kuvaa 'tungua' (kwa vile mwuzaji huwa na fimbo ndefu ya kutungulia shati mahali lilipo). Nguo zilizothaminiwa ni zile zilizoshonwa na fundi cherahani!
6-Watu walikuwa wakiitana 'ndugu'
7- Dar kulikuwa na mabasi ya 'orofa' (double-deckers)
8- Kulikuwa na magari mengi ya ma-trailer yanayotoka Kenya kwenda Zambia
9-Kulikuwa na michezo iliyovutia maelfu kama East African Challenge Cup, mashindano ya mikoa ambapo Dar, Mwanza, Kilimanjaro na Tanga ilikuwa ikiwika sana. Wakati fulani fainali ilirudiwa kwa siku tatu ndipo alipopatikana mshindi!
10- Kulikuwa hakuna AIDS!
Sasa endelea.
Wakati nainukia miaka ya sabini, mambo haya na tabia hizi zilikuweko sasa hakuna tena.
1-Kulikuwa na viwarsha vingi vidogo vidogo mitaani: fundi cherahani, sonara, watengeneza sufuria, fundi viatu n.k.
2-Wake wengi wa nyumbani walikuwa hawaendi sokoni kwani vitu vilikuwa vinapitishwa mitaani na wafanyibiashara kama wauza samaki, mboga n.k.
3- Kulikuwa na waarabu tuliowaita washihiri. Hawa walikuwa wanatembeza nguo barabarani wakiuza (sasa ndio mabosi!)
4- Wahindi walikuwa wakijulika sana kwa viduka vya pembeni (corner shops) tukiwaita 'dukawalla' (hawakua na ubaguzi kama walionao sasa, kwani huwezi kumbagua mteja wako unayemtegemea kwa ulaji wako wa kila siku)
5-Wakati huo kuvaa shati au suruali iliyokwisha tengenezwa (ready made) ilikuwa jambo la aibu, mtu huchekwa kwa kuvaa 'tungua' (kwa vile mwuzaji huwa na fimbo ndefu ya kutungulia shati mahali lilipo). Nguo zilizothaminiwa ni zile zilizoshonwa na fundi cherahani!
6-Watu walikuwa wakiitana 'ndugu'
7- Dar kulikuwa na mabasi ya 'orofa' (double-deckers)
8- Kulikuwa na magari mengi ya ma-trailer yanayotoka Kenya kwenda Zambia
9-Kulikuwa na michezo iliyovutia maelfu kama East African Challenge Cup, mashindano ya mikoa ambapo Dar, Mwanza, Kilimanjaro na Tanga ilikuwa ikiwika sana. Wakati fulani fainali ilirudiwa kwa siku tatu ndipo alipopatikana mshindi!
10- Kulikuwa hakuna AIDS!
Sasa endelea.